Ni lazima mwanangu akikua ajue coz ninajuta kumpenda baba yake

Kihere here kimekuponza (kwa mujibu wa hotuba ya rais), Wewe unakaaje na mwanaume miaka 6 halafu bado unajiona sio mke wake? Au mpaka upewe cheti cha ndoa?,

Najua kinachokupa hasira zaidi ni tuhuma ya kutembea na mke mwingine!, usikasirike kwani huna uhakika sana kwani mara nyingine mwanamke anaweza kuwa alikua anamuwinda sana bila mafanikio akapanga kuwasambaratisha kwa hila za kutumia simu!, vuta subila!

Kuhusu kuja kuona mtoto, wala sio kosa!, hata mimi nisingekuja kwani wewe sio mke wake bado!, anaogopa kupewa ndoa ya mkeka! Pia inategemea kama kazini wanaweza kumpa ruhusa!

Nitarudi baadae niwape za uso!
 
Atarudi tu huyo dadangu!!!..
Usiongelee baya kuhusu baba yake mtoto, hiyo italeta siyo hasira tu, bali simanzi kwa mtoto.
Move on!!, ukizoea utaenjoy mapenzi yake mtoto, He's the one missing out.
Keep your head up sis, and that dude(the dad) was just a waste of semen!!
 
Miaka sita - Mnakaa kinyumba - and yet - hujui TABIA na MIENENDO ya mwenza wako? Kweli kupenda KUBAYA!
 

Waswahili hunena "asiyefunzwa na ***** hufunzwa na ulimwengu".

Nna uhakika ***** alifanya kila njia azijuazo kumfikisha mwanae chuoni, ili iwe nini? Ili mwanae asitegemee kwa mtu, awe na elimu yake na awe wa kutegemewa sio kutegemea. Yeye akaona ***** hana jipya akaifata mihogo badala ya masomo, mihogo kwa wingi huvimbisha tumbo. Halafu anakuja kujisifu kuwa atamwambia mwanae kuwa sijui babake alikuwa nini. Kama si ujinga huu ni nini? Watu kama hawa huwa wana laana za wazee wao. Hujui hao wazee wake walihangaika vipi mpaka kumfikisha chuoni, leo roho zao zinawauma kuona jasho lao limepotea bure. Hii iwe fundisho kwake na kwa wengine na atubu sana kwa Mungu wake na kwa wazee wake na arudi akasome. Hana zaidi ya kuwa omba omba na kutegemea mihogo kwa aliyojitakia, cha kumuokoa ni kutafuta elimu ili imuokoe, hakuna zaidi. Ama mihogo ama elimu, aamue moja na akome uzinzi la sivyo ataongeza mwingine.
 
Pole mdada kwa matatizo yaliyokupata.Lakini mbona hasira nyingi sana?katika maisha mambo mengi utokea,na mara nyingi muhusika ndio anataka mwenyewe kuwa hivyo kama wewe ulivyokuwa na huyo jamaa,ni uamuzi wako,kumpenda,uamuzi wako, kushika mimba uamuzi wako,kuacha chuo uamuzi wako! hata kama yeye aliku-influence kidogo,lakini binadamu tumepewa akili tufikili,hivyo ungeweza kuamua lipi litendeke na lipi ulikatae!.Sielewi kabisa uamuzi wako wa kuacha chuo kwa ajili ya mwanamme!katika maisha ya sasa,am sorry dadangu huo ni upuuzi sio mapenzi.Alafu huo mpango wa kuzaa mlikaa chini kuamua pamoja?,uliamua mwenyewe ukadhani jamaa ata support? au ilitokea bahati mbaya? Inawezekana wewe ulitaka kuzaa lakini jamaa hakuwa tayarie!.Kweli jamaa kachemsha kukuacha na mtoto peke yako,lakini wanawake mnalalamika sana wakati vitu vingine inabidi muwe makini toka mwanzo wa mahusiano.kila siku story kama hizi zipo nyingi tu! inabidi u take responsibility kwa maisha yako!.huwezi kuzaa na mwanamme bila kua na uhakika mchango wake utakuwa upi katika malezi,na wewe utahishi vpi wakati umeacha kusoma ili uzae! yaani unanikera kila ninaposoma kuwa umeacha chuo ili kuzaa,maisha gani uliyokuwa unategemea?? kukaa ndani na kutegemea mwanamme! kwa nini usisubiri umalize ndio uzae? afadhali angekuwa kakuoa,lakini boyfriend tu ndio na wewe unajiachia hapo hapo kama mzigo.Cha msingi endelea na maisha yako,achana na huyo **** na matatizo yako usimuwekee mwanao,kama jamaa ka break your heart,ni mzigo wako kuubeba sio mtoto,yeye hausiki.Na ukikutana tena na mwanaume mwingine akikisha anajali na kusupport malengo yako,na rudi chuo utafute kazi umlee mwanao,sometimes you fall down so you can learn how stand!.take care
 
lakini mbona hajatangaza kukuacha? kama vp we si utie timu tu dar halafu mambo mengine utajua huko huko? Jifunze kupigania kile unachokitaka na kukipenda ktk maisha yako. Komaa kama vipi utanyang'anywa hata 'underwear zako'

Ndyoko nadhani umemshauri dada yetu vizuri, apiganie kilicho chake, afterall jamaa anakana kuhusu kuwa na mwanamke mwingine, kwa nini yeye ndiye anakuwa mrahisi ku-surrender?
 
heeee yamekuwa haya tena loool
we ni mtu mzima ndo ushauri wako huu
mmmh



 
mimi mwanaume hawezi nihangaisha hata kidogo
ikiwa nina nguv ya kufanya kazi nimejifungua
salama. kwanza mwanaume kama huyu
si mwaminifu ukimwi njenjekwanini
nihangaike na jitu linalohatarisha maisha
yangu?
sepa achana nalo huyo yaelekea si muoaji
mapenzi ukilazimisha mwisho ni kifo
lets say unakuja dar,mnarudiana
then analala nje,wanawake wanakutusi
hakujali,wewe waala kitoto chenu
?????????????? atakutesa kimwili
kiroho na kisaikolojia.mwisho utashindwa
kufanya kazi kumlea mwanao
lea mtoto na umshukuru mungu kwa kukupa zawadi
hyo,mwanaume kitu gani bwana'



tafakari na uchukue hatua ukimwi unaua
usijemwacha mwanao duniani ajili
ya mapenzi
jipe moyo utashinda
wala usikwazike na kipato chake
wewe una chako
wamama wangapi wana watoto wa5 na wametelekezwa na
waume zao na na wanafagia barabara na watoto wanaishi
hiyo ni changamoto,ipokee piga moyo konde na ufurahie maisha


wanaume si kitu na wewe unaweza!!!!!!!!!
 
mkuu mimi figganigga nakushauri kiutu uzima umesikia?.kwanza pole na yanayokukuta.pili tambua sisi wanaume hatujui kuacha.tatu kubaliana na hiyo hali coz hadi uende nyanda za juu uliona kuna msaada.nne usiwe unampigia mmeo mida ya bar.tano bwana ako kakuambia hakuna mtu aliepokea simu yako hiyo inaashilia bado anakupenda na kakuambia mtoto atamuona ukija dar so anataka uje.sita be strong.nakuomba ututunzie mwanetu mambo ya wivu mtayamaliza ukija.mmeo ni wako ukiwepo.
hongera kwa kujifungua salama.mia
 
ACHANA NA HY BWEGEANAYEKATAA MTOTO LEA MTOTO WK tn KM VIP MPE MTOTO LAST NAME YA BABA.
 
ACHANA NA HY BWEGEANAYEKATAA MTOTO LEA MTOTO WK tn KM VIP MPE MTOTO LAST NAME YA BABA YK MZAZI
 
Dada Pole sana kwa yote yaliyokusibu.
ni kwamba...
Hili lililotokea nadhani ni muendelezo wa mengine ambayo hukutaka kuyaweka wazi hapa JF.Nadhan kuna msuguano baridi uliokuwepo kati yenu hivyo wewe kuondoka Dar kuja kaskazini ilikuwa tiketi ya yeye kupata nafasi ya kutimiza jambo alilokuwa amedhamiria siku nyingi. Ukweli ni kwamba hakuwa na upendo na wewe kama ulivyoeleza hapo juu. inawezekana kabisa hakuridhishwa na wewe kuishi nae kama mke hivyo aliishi na wewe tuu kwa vile imetokea ila alitamani siku moja kila mtu aishi kivyake. Umesema pia ulikosana na ndg zako kwa ajili yake..hii ni wazi kwamba uhusiano wako na yeye umewahi kuwa na migogoro mingi iliyosababisha hata ndg zako waingilie japo wewe uliona kama wao ndo wabaya. funguka sasa utafakari sababu za kutoelewana na ndg zako. kitendo cha kuacha chuo kwa ajili ya mwanaume sio jambo la kuwafurahisha ndg zako...nadhan walikushauri sana lakin ulipuuzia ushauri wao. usemi usemao 'majuto ni mjukuu ndo utauelewa maana yake kwa sasa.
Kumueleza mtoto ubaya wa baba yake haitakuwa busara kwan itamuathiri mtoto kisaikolojia, anapaswa kujua tuu ulitengana na baba yake lakini sio kwa sababu zipi. japo ni mapema kusema mmetengana..ni mapema sana...huenda kuna chembechembe za ujana zinamsumbua....nafasi yako kama mzazi mwenzake itabaki kuwa pale pale hata kama ataoa mke mwingine, Kila jambo linalotokea lina maana yake...kuwa mvumilivu, ni kipindi kifupi sana kwako kusema wewe na yeye basi. Ulikuwa unapenda sana ghafla sasa unamchukia sana, elekeza nguvu zako kumlea mwanao mchanga kwa sasa.

Nitarudi badae
 
AND THATS Y NASEMA MTOTO WANGU AKIKUA LAZIMA NIMPE KISA CHA BABA YAKE.COZ AMENITENDA HASWA.

Pole sana kwa mkasa mzito!

Lakini pia nikuase kama wachangiaji wengine walivyosema; usitende kosa hilo hapo juu ni sawa na kuua; wewe na baba mtu mtalingana kimakosa! Mtoto anayo haki ya kuwatambua wazazi wake hata kama ni mahayawani kiasi gani hiyo ni haki yake ya kuzaliwa na sio sehemu ya mali yako kwamba unawea amua namna gani uiendeshe hivyo pia sehemu yako kuanza kumtenganisha mtoto na babaye.

Familia nyingi zimekumbwa na haya na hasa tunapowatumia watoto kumaliza hasira zetu...............si vizuri na Mungu hapendi; Lea mwanao kwa upendo mwache Mungu aseme naye na sio kuanza kupanga kumpandikiza chuki na unayajuaje ya baadaye ? hata kama umejiapiza kutosamehe huyo ni mzazi mwenzio tu!
 
Wanawake mkihakikishiwa kuwa munaolewa maisha munaleta mauzi makubwa ndani ya nyumba. Hakuna mwanaume alipanga kuoa zaidi ya mwanamke mmoja, ila mauzi yenu ndo yanayopelekea nyumba dongo. Hamfundishiki, humuelezwi mkaelezeka. Mimi nimewaona wengi?
 
Tunapotaka kutoa ushauri, tungepata na upande wa pili wa shilingi. Kwa mambo ya ndoa ninavyoyajua mimi kuna tatizo ambalo limepelekea huyu bwana kunywa pombe. STress za mwanamke
 
pole sana-ila uliofanya mistake sana kuacha chuo-by the way bado una nafasi ya kurudia chuo
Pili unaweza kumchukia sana mtu-wakati yeye yupo na mambo yake,yani hata hana fikra juu yako-cha kufanya-wewe fanya mambo yako ya maisha-kama yatamkuta ya kumkuta,atakutafuta mwenyewe
 

Pole sana kunta....., katika vyote hapo kwenye bluu ndo uliharibu zaidi, ila majuto ni mjukuu na ninaufahamu uchungu unaoupata kwa muda huu, POLE SANA.

Ushauri.
1. Jaribu kuachana nae, na uconcentrate na jinsi utakavyomlea mwanao kwani huyo ndio mwenzio kwa sasa.
2. Acha mawazo hayo ya kuwa utakuja kumwambia mwanao ya kuwa babake alikutenda hivyo sababu huwa inafika wakati mtoto anakuwa na hamu sana ya kuwa karibu na baba.
3. Haina haja ya kumpigia simu na kuomba hela ya matumizi kwani umeshajua ya kuwa si muaminifu kwako.
4. Je uliooana nae kwa ndoa takatifu? Kama ni ndio, peleka haya madai kwa wazee wenu wa dini yako husika wakakusaidie katika hili.
5. Je unafahamiana na ndugu zake ambao ni watu wazima? Nenda kwao na ukaeleze hali halisi anayokufanyia huyo baba mtoto wako, wanaweza kukusaidia.
6. Punguza mawazo, kula vizuri na umuhudumie mwanao vizuri huyo ni kila kitu kwako kwa muda huu.
7. Muombe sana Mungu wako, yeye ndiye faraja na tumaini letu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…