Padone EPM
JF-Expert Member
- Jul 17, 2020
- 604
- 882
We cndo upo kwenye mfumo tunakutegemea ww mkuuLeteni Ronja wajuba
We cndo upo kwenye mfumo tunakutegemea ww mkuu
Wewe huna Roho ya uvumilivu kabisa mkuu.....Nakumbuka niliwahi kuwa Skaut shule ya msingi, sasa kuna kipindi tukatangaziwa kwenda kambi wiki nzima, nikamwambia mshua akasema nenda akanipa na pesa ya mchango 2500/=, kumwambia bimkubwa akakaza hamna kwenda, na mie nilikua napenda kweli mambo za skauti tulikua tushapewa skafu za kuvaa shingoni hapo nafukuzia kupata gwanda la kaki,na bellet na kupata gwanda lazima uhitimu mafunzo.
Nikasema usinitanie wewe, nikatoroka hom, na kibegi kina,sahani, kikombe, kijiko, boxer mbili, Mswaki, dawa ya meno, pensi na sweta. Kufika kambini ilikua jioni, tukaimba chenja za kutosha, tukala ubwabwa halafu tukalala madarasani, maana kambi ilikua kwenye eneo la shule . Kesho yake asubuhi wakatakiwa watu kumi wakalete kuni na mie nikachaguliwa miongoni mwao. Tukaondoka kuleta kuni saa 12 alfajiri, mwendo mrefu kidogo.
Kurudi Jua limeshachomoza ilikua mida ya saa nne asubuhi Kamishna akasema tumefanya uzembe, na adhabu kali itatolewa kama fundisho kwa wengine. tukapewa adhabu ya kukimbia kuzunguka bendera ya ile shule nonstop, kamishna akaingia zake ofisini.Tukaanza adhabu chap.Tulikimbia kuzunguka ile bendera tukaloa jasho na vumbi la kutosha miguuni,Hatukula asubuhi wala mchana kila mmoja anasonya tu. Kuna jamaa mmoja alikua muoga kweli akawa anatukataza kusonya anasema Kamishna akisikia tutaongezewa adhabu. kamishna anakuja kutoka saa nane mchana anakuta bado tunakimbia kuzunguka ile bendera Jamaa anajifanya kutushangaa eti " Ah bado mnakimbia tu, niliwasahau aisee haya nendeni mkale " Tukaitikia asante mkuu, wakati tunajua fika watu washakula cha mchana hivo ni kusubiri cha usiku, mda huo nishaanza kumkumbuka maza alivokua ananikataza kwenda kambini.
Mpaka hapo nikawa nishaingiwa kinyongo na Uskauti wenyewe, nikajisemea ikitokea kazi nyingine naenda halafu natoroka, maana mazingira pale kambini yalikua hayaridhishi, vyoo vya shule matundu machache, hakuna maji,kulala kwenye madawati ama ukikosa unalala chini, maana tulikua wanafunzi shazi. mbu nao wakutosha.Haikuisha hata siku jioni ya siku ileile nikasikia wanahitajika vijana wa kwenda kuchota maji, nikasema fursa ndo hii sasa ya kuondoka Guantanamo.
Nikaenda chap tukahesabiwa watu 20, Tukapewa ndoo za lita kumikumi kila mmoja na yake, nikaanza kuwaza kuhusu kibegi changu, niko nacho mgongoni saa hiyo, natokaje nacho getini sasa. na getini kuna skauti wanoko hatari yaani wanajikuta makomando mixer kutembea juu ya kamba na kuruka moto. nikasema sio kesi Tulivokaribia getini nikamshtua jamaa mmoja ambaye tulikua pamoja kwenda kuchota maji, nikamuomba anishikie ndoo yangu ili nikaweke begi halafu nakuja. na wale maskauti wa getini wakaona tunavokabidhiana ndoo, na nilifanya makusudi ili nitakaporudi wazinizuie kutoka nje.
So nikampa jamaa ndoo yangu halafu nikakimbia kwenye darasa tuliokua tunalala nikaingia nikaenda mpaka kwenye madirisha ya upande wa nyuma nikalidondosha begi kwa nje halafu nikarudi mbio kuwahi getini, kufika pale nikakuta wenzangu washatoka nje, kwakua wale maskauti walishaniona nilivokua nakabidhi ndoo kwa mwenzangu hawakunitilia shaka wakaniruhusu nitoke. nilivotoka nje mzeeee. nilikula kona chaap, mpaka nyuma ya ile shule nikaokota kibegi changu halafu nikala kona kwenda hom.
Kufika Hom jioni ileile nakuta maza kakaa nje anachambua mchele namuamkia haitikii. ananiangalia miguuni nilivopauka, nikajua leo lazima kiwake usiku dingi akirudi. nikaingia chumbani kwangu nikajifungia humo, usiku mshua karudi nikaitwa mezani maza anasoma mashtaka anadai nitafute pa kwenda kuishi, kijana wa darasa la tano naenda kuishi wapi sasa. nikaomba msamaha pale na Nikawasimulia kilichonikuta, Maza alinicheka kinoma, so kambi ya wiki nililala usiku mmoja tu. Sijui huko rts itakuaje.
Hhhhh, Skauti MottoWewe huna Roho ya uvumilivu kabisa mkuu.....
Mimi mwenzako nilikuwa skauti tangu niko darasa la 4 mpaka namaliza kidato cha 6 na nilikuwa napenda sana kuwa skauti na darasani nilikuwa vizuri sana...
Ila katika uskauti wangu sitakaa nikasahau kambi ya KALANGASA huko SUMBAWANGA vijijini wakati huo niko kidato cha 5 pale KANTALAMBA BOYS na nilikuwa Troop Leader(TP) nakumbuka nimeandika barua kwa mkuu wa shule ya kuomba ruhusa ya siku 7 basi tukapewa ruhusa na share ya chakula kwa kila skauti.....
Basi nikaondoka na jeshi langu la vijana kama 25 hivi hapo najikuta mkuu wa majeshi flani hv na ukijumlisha zile gwanda na buti basi nikaona maisha nimeyamaliza maana skauti wote pale shule mimi ndiye nilikuwa mkubwa wao kwa maana hiyo kauli yangu ni amri na kama unavyojua skauti wanatii sana viongozi wao kuliko hata mwalimu 😄
Basi bwana tukaripot kambini hiyo siku nakumbuka ilikuwa mida ya jioni na kambi yyt pale sumbawanga bila vijana wa Kantalamba ilikuwa haijakamilika.....
To cut short the story ni kuwa ile depo ilikuwa na maajabu mengi sana hasa baada ya mmoja kati ya wanafunzi kutoka shule moja pale manispaa alikuwa mshirikina na alikuwa anawatesa sana wenzake nyakati za usiku🥺
Jamani uchawi upo mpk camp za jeshi ilikuwa ni kiangazi sasa siku moja tukiwa tumelala around saa 8 hv za usiku maana tulikuwa tunalala saa 6 usiku tukasikia filimbi kila mtu akatoka nje maana tulifundishwa kutii filimbi....kwenda kwenye pared hata viongozi nao wanashangaa waliokuwepo zamu ya ulinzi nao hawaelewi...ilitokea kama mara 3 hv....bado kulikuwa na mauza uza mengi sana yaani mpk mafunzo yanaisha daah tulikuwa hoi sana
Ila SUMBAWANGA 🙌💔
nimewahi pia kukabwa na wachawi camp X ya jeshi hukohuko rukwa nilipokuwa mujibu wa sheria
Swali Zuri sana usahili safari hii kwakuwa wanataka watu nyomi unaweza kuwa ni tofauti na usahiri wa siku zote nazani itakuwa dodoma afu watakao pita ndo utapangiwa kwa kwenda kam ni kihangaiko,orj au zenji. Ila sina uhakika japokuwa kuna Mkuu kasema ni Kihangaiko usahili ko Tusubiri tu.Jw Usaili ln wakuu au mpka September na usaili wao unafanyiwa wap?
Mi niliiskia ni dodoma lkn sina uhakika asilimia 100 tuvute subra tutajua tuSwali Zuri sana usahili safari hii kwakuwa wanataka watu nyomi unaweza kuwa ni tofauti na usahiri wa siku zote nazani itakuwa dodoma afu watakao pita ndo utapangiwa kwa kwenda kam ni kihangaiko,orj au zenji. Ila sina uhakika japokuwa kuna Mkuu kasema ni Kihangaiko usahili ko Tusubiri tu.
Na majina yatatoka linSwali Zuri sana usahili safari hii kwakuwa wanataka watu nyomi unaweza kuwa ni tofauti na usahiri wa siku zote nazani itakuwa dodoma afu watakao pita ndo utapangiwa kwa kwenda kam ni kihangaiko,orj au zenji. Ila sina uhakika japokuwa kuna Mkuu kasema ni Kihangaiko usahili ko Tusubiri tu.
Saw mkuu na vp majina c yanaweza kutoka September maana nackia waliotuma wengi kinyama au process za kuchambua maombi zitakua fupi tu?Swali Zuri sana usahili safari hii kwakuwa wanataka watu nyomi unaweza kuwa ni tofauti na usahiri wa siku zote nazani itakuwa dodoma afu watakao pita ndo utapangiwa kwa kwenda kam ni kihangaiko,orj au zenji. Ila sina uhakika japokuwa kuna Mkuu kasema ni Kihangaiko usahili ko Tusubiri tu.
Subiri.Saw mkuu na vp majina c yanaweza kutoka September maana nackia waliotuma wengi kinyama au process za kuchambua maombi zitakua fupi tu?
Majina sept kwny tareh 16---30 ukoSaw mkuu na vp majina c yanaweza kutoka September maana nackia waliotuma wengi kinyama au process za kuchambua maombi zitakua fupi tu?
Utabeba dunia damu ihamie kwenye ubongo.Naona utatoroka wiki ya kutolewa urai wewe kule zoezi jepesi ni push up tu kuna mapenzi ya nyoka kutundika ni zoezi nalichukia zaidi na adhabu ya batakanya
Wale waliosema sms kwanzia 21st-25th n kamba za mafarijiano?Majina sept kwny tareh 16---30 uko
Hatuwezi jua tarehe kamili wote tuna Tabiri tu ila yoyote yanawezekana ila mwezi huu sms ni uongoWale waliosema sms kwanzia 21st-25th n kamba za mafarijiano?
Mtachanganywa na hizi lonjaAnayejua lonja yoyote please?
Kuna mtu anajua lonja alafu kusema aaaAnayejua lonja yoyote please?
Daah kwer make yunapoelekea so powMtachanganywa na hizi lonja