Ni lini Kamishna msaidizi Tabora utamaliza mgogoro wa ardhi Nzega karibu na stendi kuu ya mabasi?

Ni lini Kamishna msaidizi Tabora utamaliza mgogoro wa ardhi Nzega karibu na stendi kuu ya mabasi?

Druggist

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2010
Posts
439
Reaction score
528
Habari wadau wa JF.

Natoa wito huu kwa Kamishna Msaidizi wa Ardhi Tabora, maofisa wengine wa kitaalam, na viongozi wa kisiasa, akiwemo Waziri mwenye dhamana ya Ardhi, Mkuu wa Mkoa, na Mkuu wa Wilaya.

Mwaka 2009, kulifanyika zoezi la upimaji wa ardhi katika eneo la Kitongoji cha Sagara, pembezoni mwa barabara inayotoka roundabout ya Singida kuelekea Uchama.

Viwanja vingi vilipimwa na kuuzwa kwa wananchi kwa kufuata taratibu zilizopo.

Kwa wamiliki wa ardhi wa kimila, walitakiwa kulipwa fidia au kupewa viwanja sita kati ya kumi, huku viwanja vinne vikichukuliwa na serikali kwa ajili ya kuuza.

Hata hivyo, eneo lenye ukubwa wa takriban ekari 50, lililopo karibu na stendi, limekumbwa na changamoto kubwa. Eneo hili lilipimwa, hati zikatolewa zikiwa na majina ya wamiliki (wengi wakiwa maofisa wa ardhi na halmashauri ya Wilaya ya Nzega), lakini wananchi hawakulipwa fidia.

Kutokana na hali hii, wale waliopatiwa hati hawakuweza kuendeleza maeneo hayo kwa sababu ya upinzani kutoka kwa wananchi, ambao wakijaribu kupita maeneo hayo hukutana na upinzani wa kutumia silaha za jadi.

Wananchi wameendelea kulima mpunga kwenye eneo hilo kwa miaka mingi, huku mgogoro huu ukiendelea. Mwaka 2015, serikali iligawa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega kuwa halmashauri mbili: Halmashauri ya Wilaya na Halmashauri ya Mji. Mgogoro huu ulibaki kuwa urithi wa Halmashauri ya Mji.

Eneo hili, ambalo lingekuwa na thamani kubwa kutokana na ukaribu wake na stendi, limebaki katika hali ya sintofahamu. Kutokuendelezwa kwake kumeleta changamoto zifuatazo:
  1. Usalama: Eneo limekuwa hatarishi, hususan nyakati za usiku, kwa sababu ya matumizi ya wavuta bangi na watumiaji wa mihadarati.
  2. Thamani ya Ardhi: Kutokuendelezwa kwa eneo hilo kumeathiri thamani ya maeneo jirani ambayo tayari yameendelezwa.
Maswali kwa Kamishna Msaidizi wa Ardhi Tabora:
  • Lini mtaandaa kliniki za ardhi ili kutatua mgogoro huu?
  • Lini haki itatendeka kwa wananchi waliostahili fidia?
  • Kwa kuwa masharti ya hati yanahitaji eneo kuendelezwa ndani ya miaka mitatu, kwa nini hati za umiliki kwa waliokosa kutimiza masharti hayo zisisitishwe?
Nikiwa mmoja wa watu wenye ardhi katika maeneo hayo, nilishuhudia hali hii nilipokuwa Nzega kwa kazi kati ya mwaka 2013 na 2018. Sasa ni mwaka 2024, zaidi ya miaka 15 tangu mgogoro huu uanze, lakini ardhi hiyo bado ipo kwenye hali ya majaruba kana kwamba mamlaka zimesinzia.

Amkeni! Ni wakati wa kuchukua hatua!

IMG_20241202_102127.jpg
 
Habari wadau wa JF.

Natoa wito huu kwa Kamishna Msaidizi wa Ardhi Tabora, maofisa wengine wa kitaalam, na viongozi wa kisiasa, akiwemo Waziri mwenye dhamana ya Ardhi, Mkuu wa Mkoa, na Mkuu wa Wilaya.

Mwaka 2009, kulifanyika zoezi la upimaji wa ardhi katika eneo la Kitongoji cha Sagara, pembezoni mwa barabara inayotoka roundabout ya Singida kuelekea Uchama.

Viwanja vingi vilipimwa na kuuzwa kwa wananchi kwa kufuata taratibu zilizopo.

Kwa wamiliki wa ardhi wa kimila, walitakiwa kulipwa fidia au kupewa viwanja sita kati ya kumi, huku viwanja vinne vikichukuliwa na serikali kwa ajili ya kuuza.

Hata hivyo, eneo lenye ukubwa wa takriban ekari 50, lililopo karibu na stendi, limekumbwa na changamoto kubwa. Eneo hili lilipimwa, hati zikatolewa zikiwa na majina ya wamiliki (wengi wakiwa maofisa wa ardhi na halmashauri ya Wilaya ya Nzega), lakini wananchi hawakulipwa fidia.

Kutokana na hali hii, wale waliopatiwa hati hawakuweza kuendeleza maeneo hayo kwa sababu ya upinzani kutoka kwa wananchi, ambao wakijaribu kupita maeneo hayo hukutana na upinzani wa kutumia silaha za jadi.

Wananchi wameendelea kulima mpunga kwenye eneo hilo kwa miaka mingi, huku mgogoro huu ukiendelea. Mwaka 2015, serikali iligawa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega kuwa halmashauri mbili: Halmashauri ya Wilaya na Halmashauri ya Mji. Mgogoro huu ulibaki kuwa urithi wa Halmashauri ya Mji.

Eneo hili, ambalo lingekuwa na thamani kubwa kutokana na ukaribu wake na stendi, limebaki katika hali ya sintofahamu. Kutokuendelezwa kwake kumeleta changamoto zifuatazo:
  1. Usalama: Eneo limekuwa hatarishi, hususan nyakati za usiku, kwa sababu ya matumizi ya wavuta bangi na watumiaji wa mihadarati.
  2. Thamani ya Ardhi: Kutokuendelezwa kwa eneo hilo kumeathiri thamani ya maeneo jirani ambayo tayari yameendelezwa.
Maswali kwa Kamishna Msaidizi wa Ardhi Tabora:
  • Lini mtaandaa kliniki za ardhi ili kutatua mgogoro huu?
  • Lini haki itatendeka kwa wananchi waliostahili fidia?
  • Kwa kuwa masharti ya hati yanahitaji eneo kuendelezwa ndani ya miaka mitatu, kwa nini hati za umiliki kwa waliokosa kutimiza masharti hayo zisisitishwe?
Nikiwa mmoja wa watu wenye ardhi katika maeneo hayo, nilishuhudia hali hii nilipokuwa Nzega kwa kazi kati ya mwaka 2013 na 2018. Sasa ni mwaka 2024, zaidi ya miaka 15 tangu mgogoro huu uanze, lakini ardhi hiyo bado ipo kwenye hali ya majaruba kana kwamba mamlaka zimesinzia.

Amkeni! Ni wakati wa kuchukua hatua!

View attachment 3167287

Wizara ya Ardhi
 
Back
Top Bottom