Ndugu wana JF, kuhamishwa kwa Mkuu wa Kitengo cha Kuzuia Dawa za Kulevya, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Godfrey Nzowa, kwenda ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Charles Mkumbo kwenda makao makuu na pia kuhamishwa kwa makamanda wa Shinyanga, Arusha, Morogoro na Kinondoni kuna uhusiano na uchaguzi au ni malalamiko ya Mengi yamefanyiwa kazi? source IGP Mwema apangua makamanda
Hili la Matei Inaweza kuwa inatokana na mchakato wa kutangazwa matokeo. Ni yeye ndiye aliyeforce matokeo yatangazwe kama yalivyo, kutokana na umati wa watu uliofurika kusubiri matokeo kuwa vijana wake wasingeshindana nao. Hata hivyo, indeep Matei ni mwanamageuzi.
Mungi, jibu limejitosheleza kiasi. Nifahamishe kidogo, uanamageuzi wake ni kwa sura hiyo moya ya shinikizo la watu wengi kudai matokeo yatangazwe mara moja kama yalivyo au kuna na data nyinginezo za kuweza kukolezea utamu walau??