Ni mechi zipi za soka hutozisahau kamwe?

Sikumbuki mwaka vizuri lakini ilikuwa kati ya 1997-2000 mechi kati ya wakimbizi wa Burundi na wale wa DRC (zamani Zaire).

Mechi ilichezwa kwenye uwanja wa TTC Kasulu, mpaka mpira unaenda dakika ya 80 bado bila bila na kila goli linalindwa kwa nyuma ili watu wasitegue ndumba.

Dakika kama ya 85 Burundi walipata goli na katika purukushani za kushangilia kuna jamaa wa DRC walirusha vitu kwenye goli la Burundi na muda huo huo goli likarudi. Mpaka dakika ya 90 1-1, nyogeza 30 haikuzaa goli.

Kimbembe penati, kila timu ilipata 5 za kwanza, kila wakipiga goli linaingia, sasa DRC wakakosa penati ya 14, ilikuwa kama Burundi akifunga ndio basi ameshinda, lilipigwa shuti golikipa akalala huku mpira badala ya kuingia golini ukaganda na kudondoka chini bila kuzuiliwa na kitu.

Hapo si refa wala kamisaa alijua cha kufanya, ilikuwa mzozo mpaka mpira ukaisha bila mshindi.
 
Arsenal vs Barcelona champion league final, Arsenal anafungwa kuanzaia hapo ni full majanga hadi leo
 
Cameroon vs Columbia, kutokea kifo cha Marc Vivien foe dah achen jaman
 
The dream team ya ufaransa1998. Play maker zizzou. Babu alikua anacheka miracle yule nilikua high school kocha alikua anatukalisha na kitu fun dish kupitia mechi zile.
Ghana 2010 gian alivokosa penalty.
Kuna mechi finally man u na chelsea. Mpaka dakika ya 80 Chelsea tunaongoza 3 bila. wale mashetani walivopiga 4 sielewi.
Niko wa high school team ya shule tu lichen a na timu ya watoto waki jerumani. Mazafantaz walicheza kabumbu ya akili sana maana nasi tulikua wabishi sio mchezo. Nilitamani tucheze siku nzima maana Ilikua mashindano ya akili zaidi ya mpira.
 
Duh una link ya hii mkuu?
 
Duh una link ya hii mkuu?

Link gani mkuu, hii mechi niliiona live na kulikuwa hakuna replay eti muone slow motion, ilikuwa kwenye sherehe ya Siku ya Mkimbizi duniani, na kipindi kile Kasulu kulikuwa na kambi kubwa mbili za wakimbizi, DRC walikuwa Nyarugusu (Makere), na Burundi walikuwa Mtabila (kijiji jirani na Kanazi).

Jamaa walikuwa vizuri kisoka ila ndumba ilikuwa noma zaidi, nakwambia wakati huo mpira wa penati ulioganda katikati ya goli bila kuonekana nani aliuzuia ilikuwa gumzo Kasulu nzima, hata refa na kamisaa ilibidi wakubaliane kusitisha zoezi la penati na jamaa wakagawana zawadi!
 
Mechi zote nilizotaja hazifikii nazoenda kutaja sasa, hizi ndio zilikuwa msingi wa mapenzi yangu kwenye soka leo hii.

Ndiki-ndikika, mkiitana ma-star wengi timu moja jamaa wanagoma kucheza. Mwenye m'pira (wa makara sana sana) lazima aitwe mwanzoni.

Kipa na ndani.

Magoli madogo. Hapa kuna wazushi wanalala golini, ile hata kupaki bus ni understatement.

Juu na Chini, wenye njumu inabidi m'vue la sivyo hawachezi jamaa, au wanacheza na sendeu, dakika kadhaa m'pira umetoboka.

One touch, hapa lazima ujue keepy-uppies ili uwe safe.

Tobo mangumi. Dah!

Late 90's na early mpaka mid 00's, those were legendary moments. Sitasahau kamwe.
 
Jiunge na group la whatsap la betting lenye members zaidi ya watu 130 upate mikeka ya uhakika na ushauri mzuri kuhusu mechi na company za betting. Kujiunga ni bure na ushauri na mikeka yote ni bure. Linki iyo hapo chini.<br /><br /><br /><br />Betting only
 
1. Mechi ya uturuki na Croatia euro 2008 bonge ya mechi uturuki alisawazisha dk 90 ngoma ikaenda extra time alipingwa dk118 akachomoa dk120 akashinda kwa matuta kwenda semi final
2. Afcon 2010 angola vs Mali mechi ya ufunguz wanatoka NNE kwa NNE Mali alisawazisha goli ndan ya dk 10
 
Aisee sitasahau uefa 2011-2012 kipindi ambacho timu yangu(THE BLUES)walivyo ichapa barca na kisha kuichapa bayern final kwa mikwaju ya penalt sijui lini tena tutazifunga hizo timu

Hiyo ilikuwa "bahatisha" Msahau tena mkuu.
 
Argentina and Chile final copa america ×2, chile wakabeba ndoo nlitamani nilie aise..

Argentina and Germany final W/C, ujerumani wakabeba nlitamani nilie aise.
 
Haa haa haa aiseee hapa
Uturuk walipambana haswa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…