Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
pia umenikumbusha mechi hii:
Nusu Fainal World Cup 1990. Argentina 2-1 Italy
Mechi ilipigwa Stadio San Paolo, Uwanja wa nyumbani wa Napoli.
Ikumbukwe Maradona alikuwa anachezea Napoli, hivyo katika mechi hii alikuwa kama yupo Nyumbani.
Baada ya Waitaliano kuona timu yao imeelemewa, Waitaliano wengi wakiongozwa na mashabiki wa Napoli waliojaa uwanjani kumuona shujaa wao Maradona akiwa na timu yake ya Argentina wakaanza kuishangilia Argentina haswa Maradona.
Mechi ikaisha kwa mwenyeji Italia kutolewa na Argentina ambayo ilienda kufungwa na Ujerumani kwenye Fainali.
portugal vs nethelands worldcup 2006
Mkuu Mussolin5, baada ya game Kuisha magazeti ya kitaliano asubuhi yake yakatoa sababu tano za wao kuondolewa. Kumbuka Italia ndio ilikuwa mwenyeji.
Walisema ni mkosi. Sababu nilikuwa 5
1. Mchezaji aliyekosa penalt alivaa jezi no 17
2. Mchezaji aliyekosa penalti ilikuwa mechi yake ya 17 akiwa ndani ya Uzi wa Azzuri
3. Ilikuwa ni mechi ya 17 kwa Italia kucheza kwenye uwanja huo waliofungwa.
4....
5....
Sababu nyingine mbili kidogo nimesahau. Mourinho unaweza kuja kunisaidia hapa.
chelsea hakucheza na bayer fainal uefa
Unaikumbuka mechi hii?
Ac Milan 4-1 Derpotivo
Mechi ya Marudiano, Ac Milan akiwa bingwa mtetezi anakula 4-0.
Derpotivo laCoruna ilikuwa na watu kama Walter Pandiani, Diego Tristan, Roy Makaay.
Man utd vs arsenal 1999 -2000 ilikuwa final nadhani ya kombe la FA mpaka dk 90 bao 1 kwa 1 exrtra time Giggs alianza kuwahesabu toka nje ya mstari wa kati walikuwa kina viera unapigwa chenga unawahi mbele unakuja kupigwa nyingine, jamaa mpaka akafunga bao David seaman ndio alikuwa golini nakumbuka arsenal ilikuwa ya kina Bergkamp, wiltord, kanu mechi ilikuwa tamu sana ile mwisho man 2 arsenal 1
Naikumbuka sana. Kama sikosei ilikuwa 2004 final akachukua Porto ya Mourinho wakikipiga na Monaco ilikuwa balaa akina Evra na Ibara
Arsenal vs Man U kwenye ligi mechi ya pili msimu wa 2003/2004 ambayo iliisha kwa droo ya bilabila huku Van Nestrooy akikosa penalt. Hiyo mechi ilikuwa na ubabe sijawahi ona. Viera, R. Kean, Kewon, Phil Nevelle, na wengineo hatareee
hakika uko sahihi mkuu...Msimu ule ulikuwa na maajabu yake.
Na mwingine aliyetisha kwa upande wa Monaco alikuwa Nonda Shaban akifunga goli dhidi ya Chelsea ya Ranieri kweye nusu/robo final sikumbuki vizuri
Taifa Stars vs Ethiopia uwanja wa Taifa mgeni rasmi baba wa taifa....stars walicheza nusu uchi na kupigwa saana wahabashi mbele ya baba wa taifa...ikiwa mwisho wake kwenda mpirani
Simba vs Yanga......nyamagana mwanza dk ya 90 yanga anasawazisha 1-1 extra time yanga anaongeza moja anachukuwa kombe.