Ni Mfumo Gani Huu wa Uendeshaji Ndani Ya Yanga?

Baba Kiki

JF-Expert Member
Joined
May 31, 2012
Posts
1,544
Reaction score
943
Nimepokea kwa mshangao taarifa ya kusudio la kukodishwa kwa klabu ya Yanga kwa M/ kiti wake Yusufu Manji, uamuzi ambao umepitishwa kwa kauli moja na mkutano mkuu leo hii tarehe 6 Agosti 2016. Kwa umri wangu huu wa utu uzima wa kati sijawahi kusikia mfumo wa namna hii kwa uendeshaji wa klabu ya mpira wa miguu duniani. Naomba kwa yeyote mwenye kuufahamu mfumo húu anielezee na mm, ili tujifunze kwa pamoja ufanisi wa mfumo huu huko duniani. Lkn pia nataka kujua huu mkutano ulioitishwa kwa dharura ulikuwa ni kwa ajili ya ukodishwaji huu pekee au kulikuwa ni kitu kingine cha msingi?
 
Leo wanachama wa Yanga wamechekesha sana. Wamenikumbusha mikataba ya ukodishaji mashamba inayofanyika vijijini kati ya wakulima na madalali. Hivi na Yanga nao wanakodisha timu?
 
Wewe kama shabiki wa yanga umeifanyia nini yanga mpaka muda huu.na mpaka sasa tajeni vitega uchumi vya yanga ambavyo vinaipatia yanga pesa.

Tunajadili aina hii ya mfumo mpya wa uendeshaji, sio mchango wa mashabiki ktk maendeleo ya klabu.
 
Leo wanachama wa Yanga wamechekesha sana. Wamenikumbusha mikataba ya ukodishaji mashamba inayofanyika vijijini kati ya wakulima na madalali. Hivi na Yanga nao wanakodisha timu?
Kesho Yanga watainunua mikia ili iwe academy yao
 
Okey hujawahi kuusikia, basi huu ni mfumo mpya ndiyo umeusikia sasa.
 
Jibu zuri sana. Waswahili kila kitu hadi kiwe kimefanyika ulaya. Nonsense. Yanga tumeanza wengine waje kujifunza!
Kuna mchambuzi mbuzi moja anajifanya kujua kila kitu lakini hamna kitu.

Okkk. Unaweza kuingia ndani zaidi kuuelezea jinsi mfumo huu unavyofanya kazi?
 
Leo wanachama wa Yanga wamechekesha sana. Wamenikumbusha mikataba ya ukodishaji mashamba inayofanyika vijijini kati ya wakulima na madalali. Hivi na Yanga nao wanakodisha timu?
Tanzania ni mashabiki mandazi,
Nilidhani usimba na uyanga unaishia kwenye mechi tu kumbe hadi kwenye maendeleo ya vilabu mnaombeana mbaya?
 
Okey hujawahi kuusikia, basi huu ni mfumo mpya ndiyo umeusikia sasa.

Lengo la kwanza limefikiwa, wengi mnajibu humu kuwa ndio umeasisiwa Yanga, well and good. Kama kuna mtu anaufahamu atupe maelezo zaidi tujue unavyofanya kazi. Wakati ule wa mfumo wa hisa na kampuni umezoeleka huko duniani lkn huku kwetu bado ndio tunajifunza, ningetamani kuujua huu nao unavyofanya kazi, faida na hasara zake
 
Jibu zuri sana. Waswahili kila kitu hadi kiwe kimefanyika ulaya. Nonsense. Yanga tumeanza wengine waje kujifunza!
Kuna mchambuzi mbuzi moja anajifanya kujua kila kitu lakini hamna kitu.
Watu wengine,wamezoea kuiga kuiga tu,hawawezi kubuni vyao..hapa Manji kafanya kozi
1..lile jengo la mtaa wa Mafia Yanga hana hati nalo 'hati'iko kwa mtu..
2..jengo la club kaishakarabati sana hkn jipya pia nalo hati iko znz ,karume family
3..uwanja wa kaunda ujenzi wa kibali utata mpk leo..
NDIO MAANA KAWAACHIA MAJENGO YAO..

Plan B..ya Manji
1..kuichukua nembo ya Yanga kuifanyia biashara
2..kuichukua timu na kuihudumia maana ndio 'roho' yenyewe (Km anavyofanya sasa)
.
PLAN C
1..kuhakikisha Yanga inafanya vzr ktk mashindano ili aitambulishe logo vzr,afanye biashara
2..kuihudumia timu ili lengo namba 1,litimie (sasa staff wote wa yanga watakua wafanyakazi wa Manji)

Naendelea kuwaza NDANI na NJE ya BOX
 
Subiri mfumo uanze kufanyakazi kwanza then utajifunza faida na hasara.
 
Subiri Jerry Muro atakupa maelezo ya ziada usiwe na haraka.
 
Reactions: bdo
Katika hali ya kawaida ni vigumu sana kuuelewa huu mfumo anao utaka manji,ngoja tu subiri siku atayopenda kuuelezea.
Maana hakuna mwenye ubavu kumuuliza manji,ukiuuliza tu anakufuta uanachama.yanga oyeeee zidumu fikra za mwenyekiti manjiii
 

Asante, wewe ndio angalau umujua kinachoongelewa hapa. Naamini wengi watakuwa wamejifunza kwa bandiko lako hili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…