Ni mke wa mtu, ni mzuri, ANANITAKA nifanyeje?

Hayo majaribu madogo sana wee mwambie ukweli tu!!!kwamba una commitment na huwezi kutoka naye!!!kuwa mwanaume kama humtaki au kumtamani mwambie!!!mapema,manake sio ooh sikupokea simu ooohh nikamkuta kituoni be brave n telll her the truth from your heart!!!
 
Mimi mwenyewe hata sikuelewi sijui umepata sehemu mpya ya uwekezaji maana hauonekani

nhahaha, una macho lakini huoni, una masikio lakini husikii sasa wacha nimtafutie sweetie PA mwengine,..lile jimama la hapo kijiweni naona linakupeleka pabaya
 
Nawaripoti kwa PAW sasa hivi, mambo gani kujadili mabiashara yenu hapa na kuharibu mtiririko wa mada ya mwenyewe?
 
nhahaha, una macho lakini huoni, una masikio lakini husikii sasa wacha nimtafutie sweetie PA mwengine,..lile jimama la hapo kijiweni naona linakupeleka pabaya
Hahaha!!!! Mimi naepuka vishawishi banaa hapa nampa hint Elia asiingie majaribuni maana naona ameishaanza kuchonga mzinga
 
Nawaripoti kwa PAW sasa hivi, mambo gani kujadili mabiashara yenu hapa na kuharibu mtiririko wa mada ya mwenyewe?

hivi B, huyo PAW anasali kanisa gani?
 

Wee kashakuingiza mtegoni kaka! Sasa hapa unatuuliza sisi ni kama umekojoa kitandani halafu unauliza nani kakojoa wakati kitandani unalala pekee yako. Huyo ni malaya kabisa ukiona mwanamke anajilengesha namna hii ujue nimalaya ogopa ukimwi
 
Mwambie mchumba wako amejua huwa unampa lift na imesababisha ugomvi mkubwa, hivyo mwambie aache kukupigia na kutuma meseji.
 
Mwambie mchumba wako amejua huwa unampa lift na imesababisha ugomvi mkubwa, hivyo mwambie aache kukupigia na kutuma meseji.
Sasa uongo wa nini? Kutoa lifti si hiyari bana. Akatae tu basi, hakuna longolongo hapa. 'usinipigie wala kuniandikia ujumbe kwenye simu yangu'
 
HTML:

Ningekuwa Dar ungenipigia pande hilo, dawa yake ninayo, mwenyewe angetoka baru immediately.
 
maumivu ya kichwa huanza pole pole...na ndilo lifuatalo kama utandelea kum-entertain huyo dada...
 
Kama mchumba wako huwa analala nyumbani kwako mara moja moja.................
Mwite aje kulala.............mweleze kila kitu..................asubuhi hakikisheni mnampa lifti huyo ibilisi mtu.....................ikiwezekana text itumwe na mchumba wako(ya kumwambia akusubiri utampitia hapo kituoni).........

Akishaingia ndani ya gari.............toa utambulisho hivi;
1: Babe...........huyu ni yule dada niliyekueleza habari zake................(atabaki na maswali akijiuliza ulimweleza kipi na uliacha kipi....umeacha kipi....)

2: Dada (jina lake)....huyu ndiye mchumba wangu kipenzi niliyekuambia........(usimtajie jina la mchumba wako).

Hakikisheni anaanza kushuka yeye...................baada ya hapo kamwe usipokee call zake wala kujibu texts.
Fululiza kupita na mchumba wako kama mara 3..4 hivi.....tena muda ambao mnajua lazima anakuwepo.......HAKUNA KUMPA LIFTI TENA!

1. Utakuwa ameepuka balaa linalokunyemelea
2. Mtakuwa mmemsaidia kusogeza siku mme wake arudi..............na kama anamshipa wa haibu.....hatakaa ajaribu kwa mwingine tena.
 

Wapi hapo da Asha?
 
Mwambie mchumba wako amejua huwa unampa lift na imesababisha ugomvi mkubwa, hivyo mwambie aache kukupigia na kutuma meseji.
Mwajuma bana, hivi kwa nini watanzania huwa waoga kusema maamuzi yao. Yaani aanze kuhangaika kumdanganya ili iweje hasa. Kama mimi nikishaona unanizingua nakupa black and white period. Mkuu Elia mimi nadhani itakuwa busara sana kama ukimweleza tu kuwa hufurahishwi na huyo dada na hutopenda kuendelea kumpa lifti. Yeah naelewa kwa wengi wetu ni ngumu lakini ili kushinda majaribu yanayokusibu nadhani hii ni njia muafaka. Na zaidi kama unaona ni ngumu hebu mshirikishe mchumba wako pia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…