Uchaguzi 2020 Ni mpambano kati ya muweka msingi wa maendeleo ya kweli kwa miaka mingi ijayo dhidi ya mkurupukaji mwenye malengo mafupi yanayotegemea uwepo wake?

Uchaguzi 2020 Ni mpambano kati ya muweka msingi wa maendeleo ya kweli kwa miaka mingi ijayo dhidi ya mkurupukaji mwenye malengo mafupi yanayotegemea uwepo wake?

CreativityCode

Senior Member
Joined
Aug 8, 2020
Posts
158
Reaction score
653
Habari ya asubuhi wanachama wa JamiiForums,

Ukiwafuatilia kwa makini wagombea wawili wenye ushindani mkali Tundu Lissu dhidi ya John Magufuli kwenye uchaguzi wa Tanzania wa mwaka 2020 utagundua yafuatayo:
  1. Tundu Lissu ni mgombea mwenye maono ya mbali na mwenye malengo ya muda mrefu wakati John Magufuli ni mgombea mwenye maono mafupi na malengo ya muda mfupi.
  2. Tundu Lissu anaitazama Tanzania ya miaka 100 ijayo wakati hata yeye hatokuwepo duniani wakati John Magufuli anaitazama Tanzania ya miaka 5 mpaka 10 ijayo na kwamba anataka awepo hai yote yakifanyika kitu ambacho hakina uhakika.
  3. Ukitazama hotuba za Tundu Lissu na maongezi yake na wahariri wa habari utagundua akitaja upeo wa mbali zaidi mfano kuhusu maendeleo ya kilimo na maisha ya vijijini aligusia miaka 50 ijayo kwa John Magufuli utagundua maamuzi yake ya hapo kwa hapo bila kujali uendelevu wake mfano alipoamuru kujengwa kwa barabara huko Geita na kwamba nyumba za watu zinaweza kubomolewa.
  4. Anayeweza kuifanya Tanzania kuwa Ulaya ni Tundu Lissu na siyo John Magufuli kwa maana Ulaya hawakurupuki bali hukaa na kuweka malengo ya muda mrefu kwa zaidi ya miaka 100 bila kujali kuwa waweka malengo watakuwa waliisha kufa. Huu ndiyo uzalendo halisi kwa nchi. Maana unataka vizazi vingi vijazvyo vinufaike.

UAMUZI NI WAKO NDUGU, MIMI NIMEAMUA KUMCHAGUA TUNDU LISSU MAANA NI MZALENDO WA KWELI NA MWENYE MALENGO YA KUWEKA MISINGI IMARA YA NCHI YETU.
 
Kuchora picha ya Ghorofa sio kumiliki ghorofa.

Huyo unayemuita mwenye maono ya mbali anafaa awe mshauri tu wa Rais tena apunguze jazba arudi chini amsadie Rais sababu yeye hana sifa za kuwa Rais atakayewaletea wananchi maisha bora.

Tanzania na Africa nzima tunahitaji marais watakaotuondoa kwenye utumwa wa kutegemea misaada huku tukiuza utu wetu na kufanywa masikini kwa kudhulumiwa maliasiri zetu.
 
Nyie kama machizi fulani, Kila siku mnalaaani eti nchi haina miundo mbinu takribani 60yrs,
leo hii tunajenga mnatuambia tusubiri mawazo ya miaka 100 ijayo ya Tundu Lisu ?
Eti ana maono ya mbali...acha asubiri maono yake atachaguliwa tu baada ya miaka 100 ijayo.
Yaonekana una ufinyu wa uelewa. Ulaya mnayoitamani haijengwi kwa kukurupuka kama afanyavyo "mungu" wenu
 
yaonekana una ufinyu wa uelewa. Ulaya mnayoitamani haijengwi kwa kukurupuka kama afanyavyo "mungu" wenu
Ulaya imejengwa haraka mno, UAE imejengwa haraka mno, Singapore imejengwa haraka mno, China imejengwa haraka mno, South Korea imejengwa haraka mno, hazikusubiri maono ya baadae ni pale pale. Unapopata nafasi ya kufanya jambo usikawie, lifanye pale pale.
 
Mmh kwani naenda wapi?
Umejitwisha ajenda za ufipa wakati wewe umelelewa Lumumba, nyinyi ndo mnaopataga laana. Ila tunajua utarudi. Tunajua huwezi kubomoa nyumba uliosaidia ujenzi hata kama katika ujenzi huo ulichangia kokoto moja tu.
 
Kuchora picha ya Ghorofa sio kumiliki ghorofa.

Huyo unayemuita mwenye maono ya mbali anafaa awe mshauri tu wa Rais tena apunguze jazba arudi chini amsadie Rais sababu yeye hana sifa za kuwa Rais atakayewaletea wananchi maisha bora.

Tanzania na Africa nzima tunahitaji marais watakaotuondoa kwenye utumwa wa kutegemea misaada huku tukiuza utu wetu na kufanywa masikini kwa kudhulumiwa maliasiri zetu.
Hata Mugabe alikuwa na fikra kama ulizoziandika kwenye paragraph ya mwisho hapo juu..... aliishia wapi?

Hiyo US yenyewe haiwezi kuendelea bila ya mashirikiano/msaada kutoka nchi nyengine, seuze banana republic zetu hizi?
 
Nyie kama machizi fulani, Kila siku mnalaaani eti nchi haina miundo mbinu takribani 60yrs,
leo hii tunajenga mnatuambia tusubiri mawazo ya miaka 100 ijayo ya Tundu Lisu ?
Eti ana maono ya mbali...acha asubiri maono yake atachaguliwa tu baada ya miaka 100 ijayo.
Hao jamaa wamekaa kitapeli tapeli Sana,usiwaamini kabisa.
Hawa ndo wale wakikwambia nje Giza basi toka ukaangalie maana huenda wamekudanganya.

Hivi tumtangaze mtu fisadi karbu miaka 10 Kisha tumpokee awe mgombea wetu wa Urais?
Asee 2015 tuliona ngozi halisi ya Hawa viumbe.
 
umejitwisha ajenda za ufipa wakati wewe umelelewa Lumumba, nyinyi ndo mnaopataga laana. Ila tunajua utarudi. Tunajua huwezi kubomoa nyumba uliosaidia ujenzi hata kama katika ujenzi huo ulichangia kokoto moja tu.
Hizi ni dua za kuku...kama sikurudi ccm ujanani basi sahau..sina ndimi mbili wala sina rivasi.
 
Jamaa limetuharibia nchi..Tanzania ilikuwa nchi yakukimbiliwa.Leo watu wamekuwa wakimbizi ref.Roma,Gurumo e.t
 
Kuchora picha ya Ghorofa sio kumiliki ghorofa.

Huyo unayemuita mwenye maono ya mbali anafaa awe mshauri tu wa Rais tena apunguze jazba arudi chini amsadie Rais sababu yeye hana sifa za kuwa Rais atakayewaletea wananchi maisha bora.

Tanzania na Africa nzima tunahitaji marais watakaotuondoa kwenye utumwa wa kutegemea misaada huku tukiuza utu wetu na kufanywa masikini kwa kudhulumiwa maliasiri zetu.
Kama taahira linakuwa na sifa za urais Tundu Lissu atakosaje?
 
Miaka 59 ya mipango ya muda mrefu...bado mnapanga tu?

Heri mtu mpya wa malengo ya muda mfupi yenye matokeo kuliko matapeli wanayoua nchi na kizazi chacke, pole pole kwa miongo mimgi...
 
Miaka 59 ya mipango ya muda mrefu...bado mnapanga tu?

Heri mtu mpya wa malengo ya muda mfupi yenye matokeo kuliko matapeli wanayoua nchi na kizazi chacke, pole pole kwa miongo mimgi...
kuiendeleza nchi siyo sawa na kujenga nyumba ya ukoo, nchi inahitaji mipango endelevu, ya muda mrefu, nikisema mipango ya muda mrefu namaanisha manufaa yatakuwepo vizazi na vizazi...yaonekana una ufinyu wa uelewa, ufahamu wako ni mdogo sana
 
Back
Top Bottom