Ni Muda muafaka sasa Tanzania tuwe na Senate "Bunge la mabwanyenye"

Ni Muda muafaka sasa Tanzania tuwe na Senate "Bunge la mabwanyenye"

Stroke

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2012
Posts
37,630
Reaction score
47,434
Wingu la siasa za nchi yetu limechafuka kwa mijadala mbali mbali kuhusiana na maswala muhimu ya kitaifa yaliyoibuliwa na ripoti ya CAG pamoja na comments za wadau mbali mbali kuhusiana na ripoti hiyo.

Ripoti hiyo imegusia unaosemekana ni ufisadi uliotokana na mambo yanayohusiana na mikataba iliyopelekea ujenzi wa miradi ya maendeleo na ununuzi wa mali mbali mbali.

Kwa nyakati tofauti viongozi mbali mbali wa mihimili ya dola na vyama vya upinzani wametoa maoni yao kuhusiana na ripoti hiyo pamoja na maswala mengine ya kitaifa.

Maoni hayo yamepelekea kuibuka kwa mijadala mizito ambayo kwa ufupi nimeona suluhisho lake ni kuwa na Senate au Bunge la Mabwanyeye ambalo litasaidia kupunguza lawama lukuki inazotupiwa serikali na viongozi wakuu wa nchi.

Senate ni Bunge la juu ambalo wawakilishi wake hutokana na mikoa na sio majimbo ya uchaguzi.

Bunge hili huwa na majukumu yaliyogawanyika katika sehemu kuu tatu.

1. Kuidhinisha au kutoidhinisha mikataba iliyoingiwa na Rais kwa niaba ya Nchi.

2. Kuidhinisha au kutoidhinisha wateule wa Rais.

3. Kufanya uchunguzi na kutoa adhabu kwa viongozi wa serikali ambao wamefanya makosa mbali mbali dhidi ya nchi.

Mara nyingi senate hutumika kama mhuri kwa maamuzi yaliyofanyika na bunge la kawaida, na pia hupewa hadhi ya kikao cha bunge kinachochuja na kutolea maamuzi maazimio ya bunge kawaida.

Ukiangalia mambo yanayotajwa kama mapungufu katika ripoti ya CAG utaona kwamba kuna umuhimu wa kuwa na bunge hili ambalo litakua likichuja maazimio ya bunge la kawaida, kupitia tena miswada ya sheria, kupitia tena bajeti za wizara mbali mbali na kutoa ushauri kwa Rais.

Aidha lingekuwa jambo la heri kwa Taifa letu kama tungeweka sifa za kielimu ambazo zitawafanya maseneta kuwa na ubobevu katika maeneo flani ili kutoa michango na maamuzi yenye tija kwa Taifa.

Mfumo huu wa Bunge la Senate unatumika na nchi takriban 64 hapa Duniani na naimani kwamba kama tukiutumia utatusaidia sana na kupunguza lawama kwa serikali na viongozi wa kitaifa.
 
Hii Miradi, halafu ukaiongezea na Mradi wa wa Bunge la Mabwanyenye, hii Nchi lazima inaenda kucollapse.
Nimewaza tu kwamba tunahitaji kuwa na mawazo mbadala ya bunge lililopo sasa,

Hata hivyo kwakua nchi nzima hatuna mikoa zaidi ya 35 bajeti yake nayo haitakua kubwa kwani maseneta hawatazidi idadi ya mikoa.
 
Umeleta mjadala mzuri tu. Bunge la Tanzania libadilishwe sheria za namna ya kugombea.

1. Uwe na angalau accomplishments kadhaa kwenye jamii katika sekta yako. Sio unafyatuka uko kama Babu Tale unagombea.

2. Uwe na exposure na sekta flani walau moja na uwe expert uko. Musukuma anajua nini kwa mfano, muda mwingi anautumia kuchekesha sijawahi ona mchango wake mzito.

3. Uwe na uwezo wa kifedha kuanzia kiasi flani, yani usiwe na njaa. Sio unakuja kuwa kama Lijualikani mwanaume mzima na kende zako unalia mbele ya camera, alafu wewe ndio ulikuwa unatunga sheria bungeni.

Tukirekebisha mambo mengi na sheria bunge linajitosheleza. Senate kwa nchi za Kiafrika ni kutengeneza instability na kuzidisha usumbufu. Kama kule Congo DR kuna viongozi wa majimbo hawaguswi hata na serikali kuu.
 
Umeleta mjadala mzuri tu. Bunge la Tanzania libadilishwe sheria za namna ya kugombea.

1. Uwe na angalau accomplishments kadhaa kwenye jamii katika sekta yako. Sio unafyatuka uko kama Babu Tale unagombea.

2. Uwe na exposure na sekta flani walau moja na uwe expert uko. Musukuma anajua nini kwa mfano, muda mwingi anautumia kuchekesha sijawahi ona mchango wake mzito.

3. Uwe na uwezo wa kifedha kuanzia kiasi flani, yani usiwe na njaa. Sio unakuja kuwa kama Lijualikani mwanaume mzima na kende zako unalia mbele ya camera, alafu wewe ndio ulikuwa unatunga sheria bungeni.

Tukirekebisha mambo mengi na sheria bunge linajitosheleza. Senate kwa nchi za Kiafrika ni kutengeneza instability na kuzidisha usumbufu. Kama kule Congo DR kuna viongozi wa majimbo hawaguswi hata na serikali kuu.
Kwa mfumo wa nchi nyingine huko wanaingia elites tu ambao watakua wanachuja maazimio ya Bunge la kawaida na kuyaboresha ili maamuzi yatayotoka yanakua bora zaidi.
 
Kwa pesa ipi mkuu.!???? Unaongeza utitiri wa taasisi ambazo zinaenda kula pesa zetu bure tu...

Hii nchi hata huu mfumo uliopo bado hatujautumia inavotakiwa.. Ufisadi kila sehemu..

Acha tupoe kwanza mkuu
 
Kwa yanayoendelea sasa nadhani tunahitaji kuwa na kitu kama hiki.

Sioni kama ni gharama kwa tija itakayotokana nalo,

Hata kama sio sasa huko mbeleni litahitajika tu.
Huoni kama ni gharama? You can’t be serious!!

Hiyo tija unayoizungumzia inaweza kupatikana na muundo huu huu tulionao sasa!
 
Kwa pesa ipi mkuu.!???? Unaongeza utitiri wa taasisi ambazo zinaenda kula pesa zetu bure tu...

Hii nchi hata huu mfumo uliopo bado hatujautumia inavotakiwa.. Ufisadi kila sehemu..

Acha tupoe kwanza mkuu
Ni wazo tu sio sheria tayari.

Ila ingefaa kama tungekua nao.
 
Huoni kama ni gharama? You can’t be serious!!

Hiyo tija unayoizungumzia inaweza kupatikana na muundo huu huu tulionao sasa!
Gharama ipi kama itasaidia kuokoa mabilioni yanatotokana na baadhi ya maamuzi ??

Hizo nchi nyingine 64 wao ni wajinga kiasi gani kuwa na mfumo kama huu??

Unataka kusema kua UK, Germany, US nao ni wajinga kiasi hicho ??

Lazima wameona faida yake zaidi ya fedha unazosema wewe.
 
Gharama ipi kama itasaidia kuokoa mabilioni yanatotokana na baadhi ya maamuzi ??

Hizo nchi nyingine 64 wao ni wajinga kiasi gani kuwa na mfumo kama huu??

Unataka kusema kua UK, Germany, US nao ni wajinga kiasi hicho ??

Lazima wameona faida yake zaidi ya fedha unazosema wewe.
Unajilinganisha na hizo nchi? Seriously?

Na nchi zingine ambazo hazina bicameral legislatures ni ngapi?
 
Unavamia tu vitu, hujui lolote. Senate sio bunge la mabwanyenye . US, Nigeria na nchi nyingine zenye bicameral system senate sio bunge la mabwanyenye! Ndio kwa UK, house of lords ndio bunge la mabwanyenye na house of commons ni bunge la makabwela, sasa sio kila nchi yenye two houses/ chambers wana tafsiri hiyo.
 
Unajilinganisha na hizo nchi? Seriously?

Na nchi zingine ambazo hazina bicameral legislatures ni ngapi?
Huo mfumo hawajauanza wakiwa tayari matajiri wameuanza kitambo.

Linapokuja swala linalohusiana na maslahi ya taifa swala la gharama sio hoja ya kutolifanya.

Hapa kila mara unasikia mkoa , jimbo la uchaguzi au wilaya imeongezwa.

Mikoa haizidi 35; Senators hawatazidi 35;

Tunaondoa DC's hizo gharama zitatoka wapi ??

Nachoona hapa ni faida tu kuliko hasara.

Labda hujalipenda wazo tu, ila kuna Umuhimu tukawa na senate.
 
Unavamia tu vitu, hujui lolote. Senate sio bunge la mabwanyenye . US, Nigeria na nchi nyingine zenye bicameral system senate sio bunge la mabwanyenye! Ndio kwa UK, house of lords ndio bunge la mabwanyenye na house of commons ni bunge la makabwela, sasa sio kila nchi yenye two houses/ chambers wana tafsiri hiyo.
Kuna aina mbali mbali za mabunge ya senate kama ulivyotaja.
 
Back
Top Bottom