Ni muhimu mnoo sasa Tanzania kuingia vitani kuilinda DRC na kuwafurusha waasi wa M23.

Ni muhimu mnoo sasa Tanzania kuingia vitani kuilinda DRC na kuwafurusha waasi wa M23.

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Ama kwa hiari (kupenda) au kwa lazima (shuruti) ni wakati muafaka sasa kwa majeshi ya Tanzania kuingia moja kwa moja uwanja wa vita (Full scale) huko DRC ili kurejesha amani na kuwafutilia mbali waasi wa M23. Sababu za kufanya hivyo zipo na kwa uchache sana nitaziweka hapa.

1. DRC ni jirani muhimu wa Tanzania akiwa mdau mkubwa zaidii wa Tanzania kibiashara kupitia bandari ya Dar. Hivyo kuzorota kwa amani ya DRC ni kuzorota kwa biashara ya bandari hapa Tz.

2. DRC ni mwanachama kamili wa jumuiya ya Africa mashariki, jumuiya ambayo kuwepo kwake kumechangiwa na juhudi za Tanzania huku jumuiya ikiwa na mikataba inayotamka kila mwanachama kusaidiwa kulindwa dhidi ya adui yoyote anayevamia au kuteteresha amani ya nchi mwanachama. Ni muda wa vitendo sasa.

3. Kwa kuwa hakuna mgongano wowote wa kimaslahi kama Tanzania itaingia kuisaidia DRC (Mpaka sasa hakuna nchi yoyote iliyokiri kuwasaidia waasi wa M23 (Japokuwa sote tunajua Rwanda ndio mhusika mkuu) na wakati huo huo Tanzania hatufungamani na waasi wa M23), hivyo uwanja upo wazi.

4. Historia ya Tanzania kujiingiza kwenye mizozo ya namna hii na kufanikiwa iko wazi. (Tanzania ilifanya hivyo 2013 huko huko DRC kwa kufurusha hao M23, na ilifanya pia hivyo kule kwenye visiwa vya Comoro).

5. Tayari askari kadhaa wa Tanzania wanaolinda amani huko DRC wanaripotiwa kutekwa na kuuwawa na waasi wa M23 katika kipindi hichi cha uchukuaji wa mji wa Goma. Tuna sababu ya kuchukua hatua!

6. Utawala wa DRC tangu kuondolewa kwa dikteta Mobutu mwaka 1997 mpaka leo hii umekuwa ni utawala rafiki na ndugu katika nyanja zote muhimu za kiserikali. Kama Tanzania itaamua kukaa kimya wakati huu DRC ikiteketea basi hakutakuwa tena na maana ya kuendeleza undugu na urafiki na DRC. Utakuwa ni unafiki kwa 100%.
 
Sawa, kesho tutaenda na mgambo kwa hatua za awali
 
Hao M23 wataita maji mmaa muda si mrefu..
 
DR Congo mnaweza kuwafurusha hao M23 bila kutegemea Watanzania!
Madini mnayo,mnalo Jeshi zuri.
Kwa nini msaidiwe?
 
Niliona viongozi wa SADC wamekutana kujaza jeshi la pamoja, muda si mrefu wahuni watarudi kwao Rwanda
 
hahah watanzagiza bhana, sijui kwa nini wanaliamini saaana jeshi lao, kwa lipi haswa? acheni kuchochea mambo na kuingilia msioyajua wala yasiowahusu, mtaaibishwa na kudhalilishwa buuure, nyie endeleeni kupiga raia na kusaka sare basi, isitoshe hiyo unayoichochea vita nani atalipia?
 
Ama kwa hiari (kupenda) au kwa lazima (shuruti) ni wakati muafaka sasa kwa majeshi ya Tanzania kuingia moja kwa moja uwanja wa vita (Full scale) huko DRC ili kurejesha amani na kuwafutilia mbali waasi wa M23. Sababu za kufanya hivyo zipo na kwa uchache sana nitaziweka hapa.

1. DRC ni jirani muhimu wa Tanzania akiwa mdau mkubwa zaidii wa Tanzania kibiashara kupitia bandari ya Dar. Hivyo kuzorota kwa amani ya DRC ni kuzorota kwa biashara ya bandari hapa Tz.

2. DRC ni mwanachama kamili wa jumuiya ya Africa mashariki, jumuiya ambayo kuwepo kwake kumechangiwa na juhudi za Tanzania huku jumuiya ikiwa na mikataba inayotamka kila mwanachama kusaidiwa kulindwa dhidi ya adui yoyote anayevamia au kuteteresha amani ya nchi mwanachama. Ni muda wa vitendo sasa.

3. Kwa kuwa hakuna mgongano wowote wa kimaslahi kama Tanzania itaingia kuisaidia DRC (Mpaka sasa hakuna nchi yoyote iliyokiri kuwasaidia waasi wa M23 (Japokuwa sote tunajua Rwanda ndio mhusika mkuu) na wakati huo huo Tanzania hatufungamani na waasi wa M23), hivyo uwanja upo wazi.

4. Historia ya Tanzania kujiingiza kwenye mizozo ya namna hii na kufanikiwa iko wazi. (Tanzania ilifanya hivyo 2013 huko huko DRC kwa kufurusha hao M23, na ilifanya pia hivyo kule kwenye visiwa vya Comoro).

5. Tayari askari kadhaa wa Tanzania wanaolinda amani huko DRC wanaripotiwa kutekwa na kuuwawa na waasi wa M23 katika kipindi hichi cha uchukuaji wa mji wa Goma. Tuna sababu ya kuchukua hatua!

6. Utawala wa DRC tangu kuondolewa kwa dikteta Mobutu mwaka 1997 mpaka leo hii umekuwa ni utawala rafiki na ndugu katika nyanja zote muhimu za kiserikali. Kama Tanzania itaamua kukaa kimya wakati huu DRC ikiteketea basi hakutakuwa tena na maana ya kuendeleza undugu na urafiki na DRC. Utakuwa ni unafiki kwa 100%.
M23 huwa wakizidiwa wanasogea mpakani mpaka wanaingia Rwanda na kujipanga upya
 
M23 tuliwashinda kipindi kile lakini sasa wamejipanga. Ni lazima tuangalie na hasara tutakayopata. Wale jamaa moto wao safari hii sio wa kitoto. Kipindi kile tulipoteza askari wengi wenye rank ya juu katika medan za vita. Japokuwa tuliwashinda lakini kwetu pia maumivu yalikuwa ni makubwa.

Awamu hii wana support kubwa kutoka rwanda na makampuni ya kigeni yanayotaka madini. Wana silaha za kisasa na mafunzo ya hali ya juu.

Nadhan ni afadhali jeshi letu likae kijanja liusome mchezo kwanza. Afrika kusini wamepeleka jeshi lao. Nafikiri njia bora kwa sasa ni ile ya "mjomba lianzishe mi bado nakunja shati" majeshi ya nchi zingine yalianzishe jwtz wataenda kumalizia kazi
 
M23 huwa wakizidiwa wanasogea mpakani mpaka wanaingia Rwanda na kujipanga upya
Safari hii inapaswa hao M23 wapigwe mpaka kwenye vichaka vyao (Rwanda). Tunataka PK ateme bungo.
 
M23 huwa wakizidiwa wanasogea mpakani mpaka wanaingia Rwanda na kujipanga upya
Safari hii inapaswa hao M23 wapigwe mpaka kwenye vichaka vyao (Rwanda). Tunataka PK ateme bungo.
 
Ama kwa hiari (kupenda) au kwa lazima (shuruti) ni wakati muafaka sasa kwa majeshi ya Tanzania kuingia moja kwa moja uwanja wa vita (Full scale) huko DRC ili kurejesha amani na kuwafutilia mbali waasi wa M23. Sababu za kufanya hivyo zipo na kwa uchache sana nitaziweka hapa.

1. DRC ni jirani muhimu wa Tanzania akiwa mdau mkubwa zaidii wa Tanzania kibiashara kupitia bandari ya Dar. Hivyo kuzorota kwa amani ya DRC ni kuzorota kwa biashara ya bandari hapa Tz.

2. DRC ni mwanachama kamili wa jumuiya ya Africa mashariki, jumuiya ambayo kuwepo kwake kumechangiwa na juhudi za Tanzania huku jumuiya ikiwa na mikataba inayotamka kila mwanachama kusaidiwa kulindwa dhidi ya adui yoyote anayevamia au kuteteresha amani ya nchi mwanachama. Ni muda wa vitendo sasa.

3. Kwa kuwa hakuna mgongano wowote wa kimaslahi kama Tanzania itaingia kuisaidia DRC (Mpaka sasa hakuna nchi yoyote iliyokiri kuwasaidia waasi wa M23 (Japokuwa sote tunajua Rwanda ndio mhusika mkuu) na wakati huo huo Tanzania hatufungamani na waasi wa M23), hivyo uwanja upo wazi.

4. Historia ya Tanzania kujiingiza kwenye mizozo ya namna hii na kufanikiwa iko wazi. (Tanzania ilifanya hivyo 2013 huko huko DRC kwa kufurusha hao M23, na ilifanya pia hivyo kule kwenye visiwa vya Comoro).

5. Tayari askari kadhaa wa Tanzania wanaolinda amani huko DRC wanaripotiwa kutekwa na kuuwawa na waasi wa M23 katika kipindi hichi cha uchukuaji wa mji wa Goma. Tuna sababu ya kuchukua hatua!

6. Utawala wa DRC tangu kuondolewa kwa dikteta Mobutu mwaka 1997 mpaka leo hii umekuwa ni utawala rafiki na ndugu katika nyanja zote muhimu za kiserikali. Kama Tanzania itaamua kukaa kimya wakati huu DRC ikiteketea basi hakutakuwa tena na maana ya kuendeleza undugu na urafiki na DRC. Utakuwa ni unafiki kwa 100%.
Fungal safari nenda kajiunge na jeshi la serikali au moja ya vikundi vya wanamgambo wanaoiunga nkono serikali ya Congo upigane.

Hoja zako ni mufilisi sidhani kama hata uliwahi kupiga kwata.

Vita sio tamithilia wengine wanapigana na wengine wanaangalia.

Kukusaidia tu endekea kubonyeza key board huku ukijudanganya kuwa serikali itafuata ushauri bogus kama huu.

Kila member wa EAC akipigana vita basi Tanzania iingie kupigana kwa niaba yake ndivyo unavyosema.

Vita ya Uganda pengine ulikuwa hujazaliwa ndio maana unaota vita, uliza waliyoiona wakuelezee athari tulizobeba watanzania.
Congo inapakana na,nchi zingine nane zote hizo unafikiri hazifanyi biashara na Congo ni Tanzania pekee!
 
Tz hatuna jesh tunajuwa vita vya mdomo iko waz majiran zetu Kenya 🇰🇪 wanajeshi imara kuliko tz
 
Safari hii inapaswa hao M23 wapigwe mpaka kwenye vichaka vyao (Rwanda). Tunataka PK ateme bungo.
Halafu unaiambia jumuiya ya kimataifa, mara Rwanda hajakushambulia na hajasema ana tatizo na wewe
 
Ambacho haufahamu KP ni kibaraka wa Tanzania na M7. Maana wamepata mafunzo tz. Na msaada wa kijeshi kundoa serekali za kidemokrasia za kipindi hicho.... hivyo hawa ni watoto tuliowalea tujiulize tuliwalea vip
 
Back
Top Bottom