Ni mwezi wa tano sasa mtoto Warda haonekani

Ni mwezi wa tano sasa mtoto Warda haonekani

Maria Nyedetse

JF-Expert Member
Joined
Apr 24, 2021
Posts
661
Reaction score
1,501
Ni miezi mitano imepita tangu Mwanafunzi wa kidato cha pili Nyumbu Secondary, Kibaha Mkoani Pwani Warda Mohamedi(15) atoweke nyumbani alipokuwa anaishi April 19,2023 na hadi sasa hajulikani alipo licha ya juhudi za Familia kumsaka huku Polisi ikisema inaendelea na uchunguzi.

Mwandishi wa @AyoTV_, Bakari Chijumba amefika Yombo Vituka, Dar es salaam nyumbani kwa Dada yake Warda aitwaye Sophia na kuongea nae pamoja na Mama Warda ambapo wamesema Warda amepotea akiwa anaishi nyumbani kwa Mwalimu Wema Msanya wa Bokotimiza Primary, Kibaha “Majirani wanasema Mwalimu Wema na Mwanae walimpiga Warda kwa mti wa kusukumia chapati hadi ukavunjika, alilia sana akaondoka”

“Mwalimu alianza kuishi na Warda akiwa Shule ya Msingi aliomba aishi nae kwakuwa anafanya vizuri darasani akaishi nae kuanzia Kibiti, akahamia nae Ubungo kisha Kibaha hadi anaanza Sekondari, April 17 nilimpigia Mwalimu nikamsikia Mtoto analia nikamuuliza shida nini akasema usijali ni makuzi tu, April 19 akatoweka na hajarudi hadi leo”

“Mwalimu anasema Warda aliondoka baada ya kumpiga kwakuwa Walimu wa Warda walimwambia ana simu lakini Walimu wanasema sio kweli, Walimu waliomba Wanafunzi waandike wanayofahamu kuhusu Warda na wote waliandika kuwa Warda alikuwa anawaambia anateswa na Mwalimu Wema, barua za Wanafunzi ninazo, Mwalimu mpaka sasa yupo uraiani anaendelea na kazi na anatutishia tusifuatilie kesi, anatuambia hamuwezi fanikiwa kwasababu Mimi nafahamiana na Vigogo Serikalini”

“Nimeshahangaika Polisi Kibaha bila mafanikio hadi sasa, nimefika hadi kwa DC Kibaha kote wanamuita Mwalimu Wema wanamuhoji bado sijafanikiwa, Serikali inashindwa kupata ufumbuzi kweli juu ya hili!?”

Namba za Familia ni 0715446930 (Mama Warda) 0656520998 (Dada yake Warda) ….. Video nzima kuhusu kutoweka kwa Warda ipo Youtube ya millardayo
 
Nikikumbuka series za BEHIND THE MANSION WALLS ..... Kuna kila dalili ameuliwa na kuzikwa sehemu....

Haiwezekani akawa hai
 
Nikikumbuka series za BEHIND THE MANSION WALLS ..... Kuna kila dalili ameuliwa na kuzikwa sehemu....

Haiwezekani akawa hai
Hapo kuna serikali kuanzia kijiji hadi Wilayani, Kuna Polisi, kuna USALAMA, Kuna TAKUKURU lakini mpaka yanafika kwa Miladi Ayo meaning No one CARES

Ifike wakati tusikie WANATUMBULIWA kuanzia TAKUKURU, DC, OCD, DSO na kufikishwa Mahakamani......

Hatuwezi kuwa na NCHI AMBAYO majibu ya CHANGAMOTO MPAKA aje RAIS, MAKAMU WA RAIS na WAZIRI MKUU ndiyo waelekezwe na kufanyia kazi...

Watusaidia nini WATANZANIA??? Ni bora tukabaki na waandishi wa HABARI wawe wanatufikishia MATATIZO yetu!!!!

RAIS wetu MPENDWA upole na KUWAHURUMIA hawa watu WATANZANIA wengi WANAUMIA na kuharibikiwa!!! Leo WATENDAJI wengi wa UMMAH wanafanya biasha na kujipa TENDA kwenye maeneo yao wanayoyasimamia KINYUME na MIIKO ya UTUMISHI wa UMMA lakini HAKUNA KINACHOFANYIKA!!!

Hii inefficiency inasababishwa na NINI!!!??? na Kodi zetu WANALIPWA??? Mpaka RAIS afike????

NAPENDEKEZA ADHABU YA KIFO IONGEZWE KWENYE MAKOSA YA RUSHWA NA UHUJUMU UCHUMI NA ITEKELEZWE
 
  • Thanks
Reactions: apk
Nikikumbuka series za BEHIND THE MANSION WALLS ..... Kuna kila dalili ameuliwa na kuzikwa sehemu....

Haiwezekani akawa hai
Atakuwa hai, kimbilio la kwanza kwa mabinti ni kwa vijana
 
Hapo kuna serikali kuanzia kijiji hadi Wilayani, Kuna Polisi, kuna USALAMA, Kuna TAKUKURU lakini mpaka yanafika kwa Miladi Ayo meaning No one CARES

Ifike wakati tusikie WANATUMBULIWA kuanzia TAKUKURU, DC, OCD, DSO na kufikishwa Mahakamani......

Hatuwezi kuwa na NCHI AMBAYO majibu ya CHANGAMOTO MPAKA aje RAIS, MAKAMU WA RAIS na WAZIRI MKUU ndiyo waelekezwe na kufanyia kazi...

Watusaidia nini WATANZANIA??? Ni bora tukabaki na waandishi wa HABARI wawe wanatufikishia MATATIZO yetu!!!!

RAIS wetu MPENDWA upole na KUWAHURUMIA hawa watu WATANZANIA wengi WANAUMIA na kuharibikiwa!!! Leo WATENDAJI wengi wa UMMAH wanafanya biasha na kujipa TENDA kwenye maeneo yao wanayoyasimamia KINYUME na MIIKO ya UTUMISHI wa UMMA lakini HAKUNA KINACHOFANYIKA!!!

Hii inefficiency inasababishwa na NINI!!!??? na Kodi zetu WANALIPWA??? Mpaka RAIS afike????

NAPENDEKEZA ADHABU YA KIFO IONGEZWE KWENYE MAKOSA YA RUSHWA NA UHUJUMU UCHUMI NA ITEKELEZWE
Nikwambie ukweli?

Nyumba yenye baba/mama dhaifu hata watoto watafanya vituko.

Sasa hivi hakuna uwajibikaji hata kidogo
 
Uko hao, kwa nini mwanao alelewe na mtu mwingine?
 
Duuh, kwahiyo alipopogwa na mti alikuwa salama, maana isije kuwa hali ilibadilika na wameficha ushahidi?!

Binafsi ningemteka huyo mwalimu na kumtesa hadi aseme ukweli! Ningemminya chuchu kwa pliers hadi aseme, acheni masikhara aisee
 
Back
Top Bottom