Ni nafasi adhimu kwa Zanzibar kuitumia kutatua kero za Muungano

Ni nafasi adhimu kwa Zanzibar kuitumia kutatua kero za Muungano

WINGER_TEREZA

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2015
Posts
242
Reaction score
450
Ndugu zangu, kwanza nitoe pole kwa wote kufuatia kifo cha Raisi wetu mpendwa. Sasa nijielekeze moja kwa moja kwenye mada, kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 37(5) Makamo wa raisi, mama Samia, ndiye atakaye kuwa raisi wetu kwa kipindi chote kilichobakia kuelekea 2025.

Hii itapelekea kuwepo kwa viongozi wakuu wawili ambao kwa mujibu wa katiba zetu (katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na katiba ya Zanzibar) ndio wanamamlaka makubwa yanaihusu Taifa letu kwa ujumla wanaotoka upande mmoja wa Muungano yaani Zanzibar.

Kwa kuangalia hapo utaona upande mmoja wa Muungano (Zanzibar) utakuwa umetoa viongozi wakuu wenye mamlaka za juu kabisa hivyo wanaweza kutumia "fursa" hii kutatua kama sio kumalizia kabisa kero za Muungano hasa zile zilizo dumu miaka nenda rudi.

Nawasilisha, Wasalam.

PIA SOMA
- Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?
 
Tumetoka kwenye matatizo, na wewe unashauri tuendelee na matatizo! Ngoja kwanza tuyaponye haya majeraha ya mgawanyiko baina yetu. Baadae tutalifikiria hilo suala lako.
 
Ndugu, tuomboleze kwanza, hapa duniani tunapita tu! Mungu aiweke mahala pema penye pumziko la milele baada ya kazi ngumu ya kuwatetea wanyonge!
 
Ndugu, tuomboleze kwanza, hapa duniani tunapita tu! Mungu aiweke mahala pema penye pumziko la milele baada ya kazi ngumu ya kuwatetea wanyonge!
Ni kweli hapa duniani tunapita ila kwa Wanaobaki maisha lazima yaendelee na hivyo ndivyo ilivyo.
 
Samia atapata wapi muda wakutatua kero za muungano wakati majibwa ya ccm yataanza kupigana vikumbo kumendea kiti 2025?
Huyu mama anaweza kuyumba sana
Sema shida ndio inaanzia hapo badala ya kujikita katika kujibu kero wao watajikita katika kupanga safu kuelekea 2025
 
Samia atapata wapi muda wakutatua kero za muungano wakati majibwa ya ccm yataanza kupigana vikumbo kumendea kiti 2025?
Huyu mama anaweza kuyumba sana
Ile vita kuu ya tatu ya dunia na tuliyo itabiri, huenda ikatokea hata kabla ya ule muda ulio tarajiwa (2025 iwapo mzee angemudu kufika na kuachia ngazi kwa hiyari)

kati ya CCM ASILI vs ccm makinikia! Hakika vyuma vitaumana!!!

Ni suala tu la muda kuanzia sasa.
 
Sema shida ndio inaanzia hapo badala ya kujikita katika kujibu kero wao watajikita katika kupanga safu kuelekea 2025
Kweli kabisa.
Wasiwasi wangu team JK ita win kwani za chini chini walishaanza kujipanga kwa ajili ya 25
 
Huyu Samia atapata shida sana, mijibwa ya Lumumba itakua ikimbwekea tu masaa 24, Team JK na timu Majaaliwa watakua mapambanoni, Hataweza kufanya chochote kihuru.
 
Samia anatakiwa awe mkali na atembelee dira aliyoiacha Magufuli, na Akamilishe miradi hiyo, asijidanganye kupendwa eti apendwe na kila mtu , huwezi ukawa Rais uka pendwa na kila mtu lasivyo nchi ita mshinda.
 
Samia atapata wapi muda wakutatua kero za muungano wakati majibwa ya CCM yataanza kupigana vikumbo kumendea kiti 2025?
Huyu mama anaweza kuyumba sana.
Fisi waliomfanya mwamba akawa mbogo wangalipo na kamwe hawawezi achia mkate uwaponyoke.
Ukikumbuka kilichompata Mzee Jumbe utajua kwanini Mzee Mwinyi hakuhangaika na muungano!!!
 
Back
Top Bottom