Ni namna gani naweza kufuatilia kupata Hati ya Kiwanja?

Ni namna gani naweza kufuatilia kupata Hati ya Kiwanja?

Ndugu zangu naomba mnipe mwongozo pa kuanzia mimi nimenunua kiwanja kutoka kwenye kampuni inayouza viwanja lakini wao walikuwa bado hawajavirasimisha ila walikuwa waneshavipima wao tu tukuvikata zen wakauza. Nilinunua nikawa na document za mauziano kupitia seeikal za mtaa lakini nahitaji kukata lessn ya umiliki kwa hiyo naomba mnielekeze pa kuanzia
Ili uweze kupata hatimiliki.....labda tuanze kupeana short summary ktk umiliki wa viwanja.....Guys umiliki wa viwanja upo ktk nyanja mbili ambao Ni umiliki wa kumila na umiliki wa kiserikali....

Umiliki wa kimila n vile unaandikiwa mkataba wako wamauziano ukielezea ukubwa kwa kuzingatia physical feature zinazoonekana ardhini Kama sehemu ya mipaka mfani mti,mnazi,mto,mkuza etc...na unakuwa umesainiwa na pande zote mbili baina ya muuza na muuziwa mbele ya mashaidi wao.......

Umiliki wa kiserikali n ule umiliki ambao unatambulika kikatiba na uliosajiliwa na wizara husika ya maswala ya ardhi.

Tunavyotaka kupata umiliki wa kiserikali apa Kuna vitu vyakuzingatiwa ambapo Tp (Mchoro wa mipango miji),survey plan (Ramani yenye kuonyesha plot number ya kiwanja ambayo inatambulika na wizara ya ardhi) na afusa ardhi....na moja ya vitu muhimu Sana ila vikisindikizwa na atribute nyengine Kama mkataba wa umiliki apa kutaka kujua ulipataje kiwanja chako,kitambulisho Cha nida na vinginevyo....

Hivyo basiii ili uweze kupata hatimiliki ya kiserikali inatakiwa utengenezewe Mchoro wa mipango miji unaoonyesha matumizi halisi ya kiwanja chako kupitia kwa afisa mpango miji(wa serikali au Binafsi wote wanaweza kufanya hii kazi kwa Bei mtayoafikiana)...mpango miji ukiwa umekamilika mpima aka Surveyor atakuja kutekeleza Mchoro wa mpango miji ardhini ikiwemo na kukupa Ramani yenye plot number ambayo itakuwa imesajiliwa na wizara,apa pia mpima Binafsi au wa serikali wote wanaweza kulifanyia hii kaziiii.....

Baada ya Mchoro wa mpango miji na Ramani ya upimaji kuwa zimekamilika hapo utaandika barua ya maombi kuanzia ngazi ya serikali ya mtaa kwenda kwa manispaa au wilaya husika kwa Afisa ardhi ili uweze kukadiliwa Kodi na gharama za uchapwaji wa hatiiii...kutoka Apo hatimiliki yako inaweza kupatikana kutoka kwa wizara kupitia kwa ofisi za Kanda ya mkoa husikaaaa
 
Utaratibu uko hivi:
1. Unatakiwa kupata kampuni itakayofanya kazi ya kupima.
2. Kampuni hiyo itaenda ardhi kuangalia kwenye ramani iwapo eneo hilo limepangiwa matumizi.
3. Kutokana na majibu yatakayopatikana toka ardhi. Kampuni ya upimaji itaenda ofisi ya halmashauri kuomba kibali cha kupima. Wakati mwingine unaweza kuhitajika kuomba kubadilisha matumizi ya eneo husika.
4. Kiwanja kitapimwa na kuwekewa mawe.
5. Mawe yataenda kusajiliwa ardhi ili yaingie kwenye ramani rasmi.
6. Utakabidhiwa michoro ya eneo lililopimwa au unaweza kuiruhusu kampuni iendelee na hatua zinazofuata.
7. Hatua inayofuata ni kwenda halmashauri kwa ajili ya kuomba hati.
8. Mwanasheria atajaza fomu za kuhalalisha umiliki wako.
9. Ardhi watamtuma mthamini kwa ajili ya kutathmini thamani ya eneo husika.
10. Thamani hiyo itatumika kukadiris gharama za transfer fees (inalipwa halmashauri) na gharama za capital gain tax (inalipwa TRA).
10. Ukishalipa kodi TRA utapewe certificate ya kuthibitisha kuwa kodi imeshalipwa.
11. Unarudi halmashauri kwa ajili ya kujaza ombi la kupewa plot number na hati.

Mlolongo wake kama unavyoona sio mdogo, ndio maana watu wenye kiwanja kimoja huwa ni ngumu kufuata utaratibu huu. Utaratibu huu ni rahisi iwapo watu wengi mashirikiana au ukiwa na viwanja vingi kwenye eneo moja.
Umeelezea vizuri Ila Apo kuanzia namba 9 na kuendelea umeelezea taratibu itayofanyika endapo mtu atanunua kiwanja kilichomilikiwa tayari kwaio ukihitaji kufanya transfer ndio unazihusisha izo taratibu kuanzia 9 na kuendelea.....
 
Utaratibu Wa Urasimishaji Ndiyo Nimeona Kamati Iliyoteuliwa Inafanya Kazi Kwa Niaba Ya Watu Wote Wenye Uhitaji Wa HATI Japo Nao Janjajanja Nyingi Sana
Wanachukua Muda Mrefu Sana Miaka Tele
 
Back
Top Bottom