Ni nani alikuwa bora zaidi, Drogba Au Eto'o?

Kitambi chakufutia tachi

JF-Expert Member
Joined
Jun 16, 2019
Posts
1,063
Reaction score
2,566
Upinzani katika kandanda ni miongoni mwa mambo yanayoufanya mchezo huu kuwa kipekee.

Mfano ni nani bora kati ya Cristiano Ronaldo na Lionel Messi, kati ya Pele na Maradona au Patrick Vieira na Roy Keane?
Achana na hao bara la Afrika limebahatika kuwa na mashujaa ambao wamefanya mambo makubwa kwenye mchezo wa Kandanda.

Leo tuzungumzie moja kati ya magwiji na vipaji maridhawa kuwahi kutokea barani Afrika nao ni Samuel Eto'o na Didier Drogba ni nani asielikumbuka lile goli la kichwa dakika za lala salama dhidi ya Bayern Munich? Au ile kombinesheni matata ya Eto'o na Diego Milito au Eto'o, Messi na Henry?

Ndugu wanajamvi, kwa mtazamo wako unafikiri ni nani mshambuliaji matata wa Kiafrika kati ya Didier Drogba na Samuel Eto'o?
 
Uzuri wamecheza kwa wakati mmoja na umri hawajatofautiana sana na wanatoka bara moja kwa hiyo mwenye tuzo nyingi za uchezaji bora kutoka bara lake ndie mchezaji bora zaidi. Etoo alikuwa bora zaidi.
 
1. Etoo
2. Yahya Toure
3.Mudy Abutrika
4. Ndio labda huyo mbanaa nywele

But jamaa kucheza EPL na ni Chelsea isiokuwa na legend ndio kummemfanya awe maarufu
 
Kinachombeba Etoo ni bahati ya kucheza kwenye timu kubwa zenye uwekezaji maridhawa hivyo ni rahisi zaidi kupata mafanikio. Kama Drogba angecheza Barcelona au Inter Milan huenda angekua na record zaidi ya Etoo.

Binafsi nampa Drogba kwa fighting spirit aliyokua nayo, Etoo pia sio mchezaji mbaya ila mazingira yalimbeba zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Drogba hata kombe la mataifa africa hata timu yake ikilemewa akiingia wachezaji na mashabiki wanapata nguvu
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwahiyo Chelsea kulikuwa Hakuna wachezaji wazuri wa kumbeba drogba?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…