Ni nani aliyepandikiza Sumu hii isiyo ya Kiutu ndani ya Mioyo ya Waswahili (Watanzania) wengi hasa hasa Siku hizi?

Ni nani aliyepandikiza Sumu hii isiyo ya Kiutu ndani ya Mioyo ya Waswahili (Watanzania) wengi hasa hasa Siku hizi?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Unakuta Ndugu au Rafiki yako kabisa labda amepatwa na Msiba wa Mzazi wake lakini Wewe ambaye pengine kwa sasa anakuona huna Kipato (Pesa) hakutaarifu au unakuja Kusikia kutoka kwa Watu wengine. Na kama haitoshi hapo hapo tena unakuta Ndugu yako kabisa labda anauguza Mzazi wake lakini hakutaarifu ila Ndugu wengine wenye Pesa na Mali wameshataarifiwa.

Hii tabia ya Watanzania (Waswahili) wa Siku hizi imetoka wapi? Ni nani aliyewadanganya Watu kuwa Thamani ya Mwanadamu na Utu wake huwa unapimwa na ama Yeye kuwa na Kazi, Mali na Pesa? Na cha Kukera kama siyo Kusikitisha zaidi ikitokea Mgonjwa amefariki ndiyo utasikia Simu au Meseji ya Kutaarifiwa Msiba.

Kwahiyo unaponitaarifu Mimi kuhusu Msiba wa Mzazi wako unamaanisha kwamba GENTAMYCINE nimeumbwa tu kuja Kuaga Maiti na Kubeba tu Jeneza lake Marehemu ila alipokuwa Mgonjwa sikutakiwa Kuambiwa ili nami basi hata kama sina Hela lakini huenda Dua yangu (Maombi yangu) yangesikika haraka kwa Mwenyezi Mungu kuliko hata hao wenye Pesa uliowathamini?

Na unakuta Rafiki yako mwingine Kafiwa na Mzazi wala hajakuambia ila Wewe Kiustaarabu tu ukampigia Kumpa pole na kumuomba akupe updates za Maziko (Mazishi) anakujibu sawa lakini unaona Kimya na ukijitahidi Kumuuliza huoni Ushirikiano hadi unakata Tamaa ya Kwenda. Na ikitokea asipokuona Msibani baada ya Msiba ataanza Kukupiga Majungu na Kukuona hufai.

Namalizia Kuuliza ni nani aliyewadanganya Waswahili (Watanzania) kuwa thamani ya Mwanadamu ni mpaka tu awe na Pesa, Kazi nzuri pamoja na Mali nyingi? Hivi mnadhani Mwenyezi Mungu alikuwa hajui ni kwanini ametuumba Masikini akina GENTAMYCINE na Matajiri akina Sky Eclat, Bila bila, Chakaza, Mokaze na mama D? Tuache Kudharauliana hapa duniani.
 
Inasikitisha sana......
Ngoja nitarudi
 
Tatizo ni wewe mwenyewe umeshajiwekea psychology kwamba ukipigiwa simu katika hizo situation ni lazma uombwe hela, ikitokea huna ndo kama hivi unaanza kujihami. Wewe kuwa free tuu watu kama nyie ni viboko vichache tuu vinahitajika kurekebisha mindset zenu
 
Hata michango, kuna wale majina yao yanakua printed pamoja na card, wengine majina yao yanaandikwa kwa mkono na wengine wanapewa card isiyo na majina wanaambiwa watajaza majina yao.
 
Nisipoambiwa au ndiyo kutaarifiwa wala silalamiki nakaa kimya kwamaana ule ukapuku wangu anakuwa kanipunguzia stress, wala silazimishi kutaarifiwa, kama kashindwa kunidhamini basi nitadhaminiwa na Mungu na wengine!
 
Ukiona hivyo tambua kwamba una kasoro, kuna wale pia wenye pesa lkn hawajulishwi pia na kasoro zenyewe;

1. Wagumu sana kutoa michango ya msaada kwa ndugu na jamaa.

2. Wanakuchallenge sana bila kujali hali uliyonayo kwa wakati huo yaani KUUGUZA na hivyo unazidi kuchanganyikiwa mara mbili.

3. Pia wapo ambao wametunza Visasi vya tangu enzi ukimpigia Simu anaanza kufukua makaburi ya Ugomvi na huenda akamuombea Mgonjwa afariki upesi, hata kama ulinyimwa Ufutio tangu unasoma umeweka kifuani hadi leo, nadhani GENTA yuko hapa! Am kiding

4. Wapo wale ambao wanajifanya Uzungu mwiiiingi, Wasomi! Wajuaji! Wazungu weusi yaani, yaani Maisha yake ni yeye na Mke na Watoto wake tuuu hataki ndugu wala jamaa zaidi ni marafiki zake wenye level yake wengine wooote mnaitwa Masikini. Ukimpigia simu kwaaanza ndio unaulizwa leo mna shida gani huko. Shiiiit.

Kabla hujalaumu twambie wewe kwanza mfumo unaotumia kuishi na ndugu zako, isije kuwa wewe mwenyewe ndio chanzo. Hakika wakati wa shida ndugu hashindwi kumjulisha ndugu yake mwenye msaaada wowote hata wa kupiga naye stori tu kwake ni msaada, ukiona hujulishwi jitafakari wewe ndie tatizo.
 
Hivi kama hauna Hela si unakuwa tu MTT jamani. . sasa upewe taarifa ili uweje uanze kuomba ama kukopa nauli uje kumuona mgonjwa na huku kwako hata mlo mmoja ni shida ndugu.

MIE hii naona INA logic hata kuna jamii moja hapa kwetu kama hauna Hela mzazi wako anafariki haupewi taarifa ujue.
Ukiwa nyumbani hata uwe mkubwa mdogo wako akitoka town ana Hela wewe ndiye unayekimbia kukamata kuku ili kaka ako achinjiwe.
Pia usipoangalia na maji bafuni wampelekea. MIE huwa naona wako sawa
 
Ukiona hivyo tambua kwamba una kasoro, kuna wale pia wenye pesa lkn hawajulishwi pia na kasoro zenyewe;
1. Wagumu sana kutoa michango ya msaada kwa ndugu na jamaa.
2. Wanakuchallenge sana bila kujali hali uliyonayo kwa wakati huo yaani KUUGUZA na hivyo unazidi kuchanganyikiwa mara mbili.
3. Pia wapo ambao wametunza Visasi vya tangu enzi ukimpigia Simu anaanza kufukua makaburi ya Ugomvi na huenda akamuombea Mgonjwa afariki upesi, hata kama ulinyimwa Ufutio tangu unasoma umeweka kifuani hadi leo, nadhani GENTA yuko hapa! Am kiding
4. Wapo wale ambao wanajifanya Uzungu mwiiiingi, Wasomi! Wajuaji! Wazungu weusi yaani, yaani Maisha yake ni yeye na Mke na Watoto wake tuuu hataki ndugu wala jamaa zaidi ni marafiki zake wenye level yake wengine wooote mnaitwa Masikini. Ukimpigia simu kwaaanza ndio unaulizwa leo mna shida gani huko. Shiiiit.
Kabla hujalaumu twambie wewe kwanza mfumo unaotumia kuishi na ndugu zako, isije kuwa wewe mwenyewe ndio chanzo. Hakika wakati wa shida ndugu hashindwi kumjulisha ndugu yake mwenye msaaada wowote hata wa kupiga naye stori tu kwake ni msaada, ukiona hujulishwi jitafakari wewe ndie tatizo.
Mkuu naamini mleta mada hajakurupuka, jamii tunamoishi kwa sasa imebadilika sana! Isipokuwa na vitu vitatu alivyotaja mleta mada tarajia unyanyapaa ktk angle mbalimbali za maisha, hiyo ndio hali halisi.
 
Nisipoambiwa au ndiyo kutaarifiwa wala silalamiki nakaa kimya kwamaana ule ukapuku wangu anakuwa kanipunguzia stress, wala silazimishi kutaarifiwa, kama kashindwa kunidhamini basi nitadhaminiwa na Mungu na wengine!
Mkuu amini usiamini kuwa hii post yako nimeipenda ile mbaya na kwamba ulichokiandika ( ulichokiwasilisha ) hapa ndiyo ukweli wenyewe mtupu.
 
Back
Top Bottom