Ni nani mwingine mwenye shauku kujua kuhusu mwendelezo wa ligi kuu wiki hii

Ni nani mwingine mwenye shauku kujua kuhusu mwendelezo wa ligi kuu wiki hii

changaule

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2020
Posts
6,039
Reaction score
10,151
Baada ya heka heka za kalenda ya FIFA kwa michezo ya mataifa mbali mbali kuisha, wiki hii ligi kuu Tanzania bara itaendelea tena. Binafsi nilimisi sana soka la timu ya Yanga ya msimu huu hasa likitangazwa na Mpenja.

Nani unautaka, Bangala. Nani unautaka, 'Mwamnyeto.'Nani anautaka 'Aucho dokta wa mpira'. Nani anautaka, 'Kibwana' Nani anautaka, 'Dickson Job.' Nani anautaka 'Feisal.' Nani anautaka 'Yacouba.' Nani anautaka 'Djuma shabani,' nani anautaka Aucho, nani anautaka 'Yacouba.' Nani anautaka, 'Mayele.' Nani anautaka. Yaani zinagongwa pasi za maana na soka safi kabisa.

Wiki hii ni Namungo vs Yanga, natamani kuona kama "nani unautaka" itaendelea hadi huko lindi mbele ya Namungo FC au ndio Yanga itarudi kwenye butu butu? Je, hiyo kama butu butu watarudi na point 3 au ndio wataacha point kadhaa? Na je kama ni mwendelezo wa soka safi je watarudi na point 3 au ndio kufungwa ila chenga twawala?

Tuje upande wa pili, Simba ambao walianza ligi kwa performance mbaya, wiki hii wanarejea uwanjani wakiwa na mabadiliko ya kocha mkuu na kocha wa viungo. Ni mechi yao ya kwanza wakiwa kwenye benchi la Simba. Washabiki wa Simba wanashauku ya kupata mwanga je lile biriani lililokuwa linawanukisha msimu uliopita je Pablo Franco atairejesha? Au ndio limeshindikana kurejea kwavile wapika biriani wamesepa wamebakia wakaanga miogo tu?

Vipi ile hali ambayo ilikuwa hawaipendi ya kufunga tu goli tumoja moja tena kwa tabu itakuwa imeanza kupata muarobaini au ndio yale yale

Yote kwa yote mechi ijayo ya Simba na Ruvu haiwezi kutoa majibu kuhusu uwezo wa kocha mpya kwasababu bado sana kuijenga timu atakavyo lakini kunaweza kutoa kamwanga mwanga hivi kwa mbaali, naam kwa mbali hivi.

Tusubiri tuone je lile soka la Yanga la 'nani anautaka ' litaendelezwa ndani ya lindi na kuendelea kuwa kileleni au kushindwa kufua dafu mbele ya Namungo.

Au point 3 za butu butu?

Vipi na jirani nae anarudi katika soka alilotamba nalo kwa misimu zaidi ya mitatu au ndio hali itakuwa ile kama alivyoianza ligi. Na vipi kuhusu matokei, je watapapasa au watapapaswa.
 
Skia kaka, Namungo hakuna timu pale! Timu bora msimu huu ukitoa Yanga, Basi ni Polisi Tz, Dodoma Jiji, Ruvu Shooting, Biashara Utd na Mbeya kwanza tu! The rest hakuna kitu.
 
Wananchi popote utakapowapeleka wanakupelekea moto tu,tena timu pinzani wakiwa kamili 11
 
Skia kaka, Namungo hakuna timu pale! Timu bora msimu huu ukitoa Yanga, Basi ni Polisi Tz, Dodoma Jiji, Ruvu Shooting, Biashara Utd na Mbeya kwanza tu! The rest hakuna kitu.
Naona vyura mmeamua kujipatia ubingwa hahaaaa
 
Skia kaka, Namungo hakuna timu pale! Timu bora msimu huu ukitoa Yanga, Basi ni Polisi Tz, Dodoma Jiji, Ruvu Shooting, Biashara Utd na Mbeya kwanza tu! The rest hakuna kitu.
Nyie baadae mnyama akiwapelekea moto mnaanza kulaumu marefa sijui wameongeza dakika 5 na karia TFF

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Skia kaka, Namungo hakuna timu pale! Timu bora msimu huu ukitoa Yanga, Basi ni Polisi Tz, Dodoma Jiji, Ruvu Shooting, Biashara Utd na Mbeya kwanza tu! The rest hakuna kitu.
Timu ndogo ndogo zinatabia za kukamia timu kubwa
 
258183618_398604755120441_7123871448545595352_n.jpg
 
Naam nalisubilia kwa hamu game la jmosi huko Lindi. Unfortunately Sogne ni mgonjwa
 
Muwe mnarudi baada ya game
Naam mdau tumeona Yanga kama vile wanataka kurudi kwenye asili yao kama walivyokuwaga misimu ya nyuma. Na Simba nao wameonesha wako serious kurejea asili yao ya msimu kadhaa nyuma. Yanga leo imetepeta shukrani kwa refarii kwa kuwapa penati ya uongo. Pia shukrani kwa Shiza Kichuya
 
Naam mdau tumeona Yanga kama vile wanataka kurudi kwenye asili yao kama walivyokuwaga misimu ya nyuma. Na Simba nao wameonesha wako serious kurejea asili yao ya msimu kadhaa nyuma. Yanga leo imetepeta shukrani kwa refarii kwa kuwapa penati ya uongo. Pia shukrani kwa Shiza Kichuya
Shiza kichuya ashukuliwe kwa vipi
 
Back
Top Bottom