Kiukweli ni jambo liliniumiza kichwa baada ya wachezaji kadhaa kutangazwa kuachwa au kuruhusiwa waende wapendapo.
Yannick bangala - Huyu tuwe wakweli alikuwa bora sana msimu uliopita licha ya makosa kadhaa ya kibinadamu lakini fundi huyu anaecheza namba zaidi ya mbili uwanjani nachelea kusema alikuwa bora sana.
Djuma Shabani - Huyu naye alikuwa ni beki tegemeo sana haswa ule msimu wa kwanza kiasi cha kuaminiwa zaidi akaingia kwenye mfumo msimu unaofuata na kuipeleka Yanga fainali kwenye kombe la shirikisho. Japo unene wake ulianza kumfanya awe mzito uwanjani.
Feisal Salum - Huyu ni fundi ni kiungo wa kisasa kabisa, hata baada ya kuanza kuiringia Yanga na kuisumbua na mambo kibao, niwe mkweli; roho iliniuma lakini sikuwa na cha kufanya hata maboss wake hawakutaka kumuachia kirahisi lakini dogo alipata baada ya kutetewa na mama.
Fiston Mayele - Huyu sina maelezo mengi ya kusema zaidi ya kumuombea afanikiwe huko alipo,ila bado yupo kwenye mioyo yetu wanayanga. Siku Yanga akitoa sare au kufungwa lazima jina la Mayele litatajwa.
Nikirudi kwenye heading ni kwamba injinia mwenye jicho la mwewe, Hersi Said, anajua mpaka anajua tena .halafu ukimuangalia hata akiwa jukwaani utagundua ndiye mwenye uchungu na timu kuliko yeyote yule.
Wachezaji wapya kama Max, Yao, wenye miili midogo na wembamba,binafsi sikuwa na imani nao kabisa,lakini kumbe hawa jamaa ni hatari mno tena hawaridhiki. Pacome zouzou sina shida naye ni mchezaji tegemeo kabisa bonge moja la mtu.
Hafidhi konkon bado kidogo haswa kutokana na namba anayocheza ni namba yenye presha ila akipewa muda najua atafunga tu.
Hakika hii ni maana ya kikosi kipana hata fitina za Fabrice ngoma wanayanga tunaanza kuzisahau.
Viva Yanga, Viva injinia kwa kazi nzuri.