Ni ngumu sana kumpata Mwanamke kama Tulia Ackson. Ana uwezo mkubwa, anafaa kuwa Rais

Tulia na bunge Zima wanashindwa kujua IGA ya DP world ni BATILI na wanashindwa kuifuta.

Mtu wa aina hiyo aliyeshindwa kuisaidia Nchi KUTAFSIRI ubatili uliokuwamo kwenye mkataba fake na BATILI ndiye useme anafaa Urais?

Kuwa na akili usizitumie, ni sawa tu na kutokuwa nazo kabisa.
 
Ananieli Nkiya unamjua wewe yuko rula na anasimamia anachoamini hana unafiki wala uchawa
Tulia ni chawa tu mmoja hiyo inampunguza maksi kwenye sifa ulizompa

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Unaweza kuandika kitu hapa JF ukajikuta unadhalilika milele
Dkt Tulia Acksoni Mwansasu ni kama maji usipoyanywa utayaoga tuuu.nyota yake haizimwi kwa maneno ya chuki binafsi.uwezo wa dkt Tulia ni mkubwa sana na ndio maana wanambeya wameamua kumpa hati miliki ya jimbo la Mbeya mjini.ndio maana hata Dunia kwa kutambua uwezo wake wa kiuongozi iliamua kumuomba kwa magoti ili akaongoze umoja wa mabunge Duniani kama Rais wake.
 
Ananieli Nkiya unamjua wewe yuko rula na anasimamia anachoamini hana unafiki wala uchawa
Tulia ni chawa tu mmoja hiyo inampunguza maksi kwenye sifa ulizompa

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile ap

Nkya nilimuona Juzi nafikiri kwenye mjadala wa wabunge wa viti maalum.
Ni mzuri lakini bado hatoshi kumlinganisha na Tulia
 
Aaaaaah MTIBELI tulishapitisha humu katika katiba yenu na jina lililopita kwa mambo hayo ni la Lucas Mwamshamba The big chawa in town sasa wewe nani kakupa kibali ? Hii Lucas Mwamshamba akiona ataumia sana moyo kwamba alikuwa wapi hata asianzishe yeye hiyo mada
 
Kuongoza nchi si suala la kujua kuongea kwani ikulu anaenda kushindana debate? Sifa za raisi ni kujua kuongea vizuri??
Ungesema amefanyia Nini nchi katika sekta kadhaa mfano
1.) Aloweza liunganisha bunge lenye upinzani au alilipasua?
2.) Anapokea hoja bila ubaguzi au anajibu vibaya na kiujuaji wale wenyehoja tofautii
3.) Analinda katiba mfano hoja ya chadema na COVID wao?
4.) Ameshirikiana vema kazi za kimataifa au nikama mwendazake alotutenga namataifa?
5.)Ameijali elimu,afya,ajira,kilimo nakuanzisha program au nimatamasha kuimba nakina Rayvany wasafi.
6.) Ameonesha hana ukabila au yeye na mwamwamwa kilaleo hatuwezi msikia mwanza,Arusha nk. kama spika!
7.) Anaguswa na maskini na kuchukia umaskini? Amewahi hata kushiriki program kusaidia wazee/maskini/walemavu kujikwamua? Nk. Nk.
Leta hoja anuwai kuelezea uhodari wa mtu kwenye nyanja Pana sio kujipendekeza kwako kwakijinga uhisi wote humu ni machawa!!
 
Ubunge wake tu hakupata kwa haki, ni matokeo ya Magufuli kuiba kura

Bado Mbeya mjini walikua wanamtaka Sugu wa chadema
 
Alishinda ubunge?
 
CCM imefanikiwa Sana kutengeneza wajinga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…