Hakika hapa kumejaa ujinga mtupu!Ujinga tu
Ubora utoke wapi mkuu zaidi ya kuongoza kwa kujipendekeza na kusimamia matakwa ya muhimili mkuu!Anaongoza kwa ubora? Maana kipimo halisi ni namna anavyoendesha bunge letu.
Uchawa ndio ndio unakusumbua mkuu, uwezo wa tulia ni kawaida sana..Kwa sifa za ulimwengu wa Sasa
Tulia Akson anamuacha Mbali Sana Sugu.
Naona juzi umepigiwa debe hapa kuwa unafaa kuwa muandishi wa habari wa ikulu, naona umepagawa kabisa. Sasa ni uchawa mwanzo mwenga😂Kwa sifa za ulimwengu wa Sasa
Tulia Akson anamuacha Mbali Sana Sugu.
Ajaye ni Mlawi, JG.Baada ya Samia ,Rais ajaye ni Tulia
Kwa Hapa Tanzania Wanawake weñye kiwango cha Tulia Akson ni wachache sana
Sasa waweke pàmoja Wapewe mdahalo na Tulia Akson alafu utaelewa nazungumzia kitu gani.
Pale bungeni ni wabunge wachache Sana wenye uwezo wa kumpa challenge Kwa hoja huyo Tulia.
Nje ya mdahalo wenye kinga ya madaraka yake ni wa kawaida tu. Inshort hatishi hivyo. Ni kweli ana uwezo fulani, lakini hatishi kwa kiwango unachotaka tuamini.
“Kwa mwanaume mwenye upeo mdogo lazima amwone Tulia kama Mjuaji, hasa pale atakaposhindwa kwa Hoja.” Mwanaume mwenye maoni tofauti na yako ana upeo mdogo! Nikukumbushe kuwa tuna Prof. Anna Tibaijuka aliyewahi kuongoza UN HABITAT, Getrude Mongela aliyekuwa mwenyekiti wa mkutano wa UN wa wanawake, na Asha Rose Migiro, kwa uchache. Hao wanawake unaowataka kudai haki zao bila usaidizi mmewapa jukwaa la kufanya hivyo? Huoni manyanyaso wanayopitia baadhi ya wanawake wanaojitokeza kudai haki zao, au za wengine, hasa pale madai hayo napokinzana na matakwa ya watawala?Habari za Sabato!
Sijawahi kumfahamu Mwanamke yeyote kwa hapa Tanzania mwenye uwezo kama Tulia Akson. Sisemi ili wengine wamuonee Wivu, wala sisemi ili yeye awe na Kiburi. Ila naongea kila ambacho ninaokiona Kwa Tulia mwenyewe.
Kama utapata Nafasi ya Kumsikia Tulia Akson akizungumza iwe kwa kuhojiwa au kuhutubia, utagundua kuwa hana tofauti na kina Kamala Harris au kina Hilary Clinton.
Utulivu!
Kujiamini!
Umahiri!
Hoja!
Ubobevu!,
Nimeona Watu wengi wanapokutana na Tulia katika mijadala wakimshindwa kwa Hoja. Unapozungumzia hoja Unazungumzia uwezo wa akili ya mtu kujenga mantiki, yaani kitu kieleweke. Wakati mwingine kwa lugha rahisi.
Tulia sijawahi kumsikia akijali uanamke wake au maumbile yake kama sehemu 6a kikwazo katika kazi zake.
Tena yeye hupendelea changamoto anapokutana na sisi wanaume.
Tulia hatajali kama wewe ni Waziri au Mheshimiwa, ukiwa bungeni kama ataona kuna jambo hujalitolea maelezo yaliyonyooka au hakuna hoja anauthubutu wa kukukosoa au kutaka kukuweka Sawa.
Kujadiliana na Tulia Akson itakupasa uwe na uwezo mkubwa kama yeye au umzidi ili usije ukaaibika.
Kwa mwanaume mwenye upeo mdogo lazima amwone Tulia kama Mjuaji, hasa pale atakaposhindwa kwa Hoja.
Tunaposema Wanawake wapewe nafasi tunahitaji wanawake wa mfano wa Tulia Akson. Wanawake wenye uwezo.
Sio Mwanamke anayelalamika hajapewa haki yake. Tunahitaji Wanawake wenye uwezo wa kudai haki zao wenyewe bila kusaidiwa. Hao ndio watakuwa na uwezo wa kuongoza.
Tulia Akson anauwezo wa kushika nafasi ya Urais katika nchi yetu na sio hivyo tuu hata kuongoza Nchi yoyote hapa Duniani. Kwa sababu anasifa za level za kimataifa.
Nimemaliza
Ni nani mwenye akili timamu hawezi kuwa rais wa nchi hii?Upo sahihi.
Ila ninachozungumzia ni kuwa Tulia kwa uwezo wake anauwezo wa kuwa Rais wa nchi hii.