Ni nini chanzo cha kijana wa kiume kusuka ama kuvaa hereni?

Ni nini chanzo cha kijana wa kiume kusuka ama kuvaa hereni?

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Nyakati hizi ni kawaida kumuona kijana wa kiume akiwa amesuka ama kuvaa hereni. Zamani tulikuwa tukiwaona wasanii ndio walikuwa wakivaa hivyo labda lengo likiwa ni kutaka kujitofautisha na wasio wasanii. Lakini bado kulikuwa na maswali ya kujiuliza.

Leo hii ata wasio wasanii, ni kawaida kabisa kumuona kijana wa kiume akiwa na muonekano huo.

Sasa najiuliza, chanzo cha haya yote ni nini, anakuwa na lengo gani? Inawezekana labda wao wanakuwa wanaiga tu bila kujua au wanajua wanacho kimaanisha?

Kukamatika kwa huyu mwanamziki wa huko marekani, kumenipelekea kufikiri zaidi katika chimbuko hili la wanaume kusuka pamoja na kuvaa hereni.

Kwa sababu hii tabia ilianzia kwa wasanii na sisi wengine tukawa tunaiga bila kujua; inawezekana walipokuwa wakishiriki zile sherehe (party), ziliwapelekea wao kutamani kuwa wanawake; ndio maana wakaanza kusuka na kuvaa hereni, wengine kubadili miondoko, kuvaa nguo za kike n.k

Sisi wa huku wa mbali tukajikuta tunaiga mionekano yao bila kujua chimbuko halisi ya hayo mabadiliko.

Bado sijahitimisha tafiti, Karibu tuumize kichwa ni nini chanzo cha kijana wa kiume kusuka ama kuvaa hereni?​
 
Nyakati hizi ni kawaida kumuona kijana wa kiume akiwa amesuka ama kuvaa hereni. Zamani tulikuwa tukiwaona wasanii ndio walikuwa wakivaa hivyo labda lengo likiwa ni kutaka kujitofautisha na wasio wasanii. Lakini bado kulikuwa na maswali ya kujiuliza...​
Kila nchi ina utamaduni wao. Kwa nchi nyingine ni kitu cha kawaida kabisa.

Kimbembe kinaanzia hapa kwetu, kwanza sio utamaduni wetu kabisa katika baadhi makabila.

Lakini wamasai boys wanasuka.

Tuishi kulingana na tamaduni zetu.
 
Kila nchi ina utamaduni wao. Kwa nchi nyingine ni kitu cha kawaida kabisa.
Kimbembe kinaanzia hapa kwetu, kwanza sio utamaduni wetu kabisa katika baadhi makabila.
Lakini wamasai boys wanasuka.

Tuishi kulingana na tamaduni zetu.
Kwa hiyo tunaiga tu kutokana na kinachoonekana huko kwingine? Kwa sababu pia, wapo wanaume wanaoshindana na dada zao katika kujiremba?
 
Kwani kuna shido?? Kikubwa huvunji amri kumi za mungu na sheria za nchi miaka ya kuish saiz ni 40 bado mnawapangia watu vya kufanya kwakwer mwili wao wakifa utaliwa na dumuz acha waufanye watakavyo
 
Kwani kuna shido?? Kikubwa huvunji amri kumi za mungu na sheria za nchi miaka ya kuish saiz ni 40 bado mnawapangia watu vya kufanya kwakwer mwili wao wakifa utaliwa na dumuz acha waufanye watakavyo
Inawezekana ni matatizo ya magonjwa ya akili; lakini ngoja tuendelee kufanya tafiti
 
Mentality tu
Kuna makabila yanasuka au tamaduni zinasuka. Mfano Rasta au Wamasai ziko nyingi duniani

Cha kushangaza mashiga asilimia kunwa hawasuki wala hawavai hereni

Kusuka hakuingiliani na ushababi wako.

Mtazamo wangu.
 
Daaah, ni ufahamu mdogo na ushamba unachangia mkuu, mimi naamini kuna namna nzuri ya kuvaa ukapendeza sio mpaka uvae macheni sijui maeleni sijui usuke, hebu kuwa smart kuna namna ya kuvaa mtu unapendeza
Najaribu kufikiria kinachowasukuma huko mwilini ni nini?
 
Kwa hiyo tunaiga tu kutokana na kinachoonekana huko kwingine? Kwa sababu pia, wapo wanaume wanaoshindana na dada zao katika kujiremba?
Kujiremba ni kwa wasanii wakati wa kufanya kazi zao ili video kama wanaendelea baada ya hapo kuna shida mahali.
 
Back
Top Bottom