Ni nini kitatokea iwapo nitashindwa kumaliza kulipia Kiwanja?

Ni nini kitatokea iwapo nitashindwa kumaliza kulipia Kiwanja?

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Kwa miaka ya karibuni kumeibuka Kampuni kadhaa zinazojihusisha na uuzaji wa Viwanja kwa njia ambayo wanamruhusu Mnunuaji kulipia kwa awamu au kidogokidogo.

Wengi watakwambia ulipe kiasi fulani mwanzo kisha utaendelea kulipia kiwango kilichobaki ndani ya miezi sita au mwaka au kwa makubaliano mtakayojiwekea.

Ambacho sijawahi kusikia kutoka kwenye Kampuni hizi ni nini kitatokea iwapo Mnunuzi atashindwa kumalizia malipo au kuchelewesha kupita kiasi.

Na je ni kwa nini Wakopeshaji hawa wasiweke wazi kwenye matangazo yao kile watakachokifanya iwapo Mtu atashindwa kumaliza kulipa, kama ni kupelekana kwenye vyombo vya kisheria, kunyang'anywa hicho Kiwanja, au iwapo watarudisha pesa uliyokwisha walipa na haikutimia?.
 
Kwa miaka ya karibuni kumeibuka Kampuni kadhaa zinazojihusisha na uuzaji wa Viwanja kwa njia ambayo wanamruhusu Mnunuaji kulipia kwa awamu au kidogokidogo.

Wengi watakwambia ulipe kiasi fulani mwanzo kisha utaendelea kulipia kiwango kilichobaki ndani ya miezi sita au mwaka au kwa makubaliano mtakayojiwekea.

Ambacho sijawahi kusikia kutoka kwenye Kampuni hizi ni nini kitatokea iwapo Mnunuzi atashindwa kumalizia malipo au kuchelewesha kupita kiasi.

Na je ni kwa nini Wakopeshaji hawa wasiweke wazi kwenye matangazo yao kile watakachokifanya iwapo Mtu atashindwa kumaliza kulipa, kama ni kupelekana kwenye vyombo vya kisheria, kunyang'anywa hicho Kiwanja, au iwapo watarudisha pesa uliyokwisha walipa na haikutimia.
Mkuu kulipia kidogo kidogo hua kunaendana na time frame na kiasi cha fedha.
Na mara nyingi mnaandikishiana kwa mkataba kwamba mpaka muda fulani inabidi uwe umekamilisha.
Mkataba ukiwa na clause inayosema ukishindwa kulipa hela hairudishwi basi hutopewa.
Kama mkataba uko kimya....mtaingia makubaliano mapya na bila shaka utakatwa kiasi fulani kufidia muda uliowapotezea kwa kuhold hicho kiwanja.
 
Utanyanganywa kiwanja na pesa yote uliyolipa ni halali yao
Sidhani kama ipo hivyo maana huo utakuwa ni dhuluma na unyang'anyi.

Kiwanja cha 3m nilipe 2.8 ninyang'anywe Kiwanja kisa laki mbili?.
 
Mkuu kulipia kidogo kidogo hua kunaendana na time frame na kiasi cha fedha.
Na mara nyingi mnaandikishiana kwa mkataba kwamba mpaka muda fulani inabidi uwe umekamilisha.
Mkataba ukiwa na clause inayosema ukishindwa kulipa hela hairudishwi basi hutopewa.
Kama mkataba uko kimya....mtaingia makubaliano mapya na bila shaka utakatwa kiasi fulani kufidia muda uliowapotezea kwa kuhold hicho kiwanja.
Sidhani kama wanaweka hicho kipengele....nadhani wanaogopa kuwatisha Wateja kwani na hii biashara imekuwa na ushindani mwingi.
 
Na je kutokuweka kwao baadhi ya masharti hadharani ina maana hakuna wanaoumia kimya kimya?.
 
Sidhani kama wanaweka hicho kipengele....nadhani wanaogopa kuwatisha Wateja kwani na hii biashara imekuwa na ushindani mwingi.

Achana na kudhani-dhani, soma angalau mkataba unavyokuwa…. tafuta taarifa usiishie kudhani tu.
 
Weka picha kama sio porojo.
Picha kwa page ngapi maana ina page 5.

Pia kumonekano tu Wahusika wanaweza wakaona na wasifurahishwe kuona doument yao mtandaoni.
 
Sidhani kama ipo hivyo maana huo utakuwa ni dhuluma na unyang'anyi.

Kiwanja cha 3m nilipe 2.8 ninyang'anywe Kiwanja kisa laki mbili?.
Kweli kabisa huwa haiwi hivi, zipo taratibu hususan kukatwa kiasi fulani
 
Kwa miaka ya karibuni kumeibuka Kampuni kadhaa zinazojihusisha na uuzaji wa Viwanja kwa njia ambayo wanamruhusu Mnunuaji kulipia kwa awamu au kidogokidogo.

Wengi watakwambia ulipe kiasi fulani mwanzo kisha utaendelea kulipia kiwango kilichobaki ndani ya miezi sita au mwaka au kwa makubaliano mtakayojiwekea.

Ambacho sijawahi kusikia kutoka kwenye Kampuni hizi ni nini kitatokea iwapo Mnunuzi atashindwa kumalizia malipo au kuchelewesha kupita kiasi.

Na je ni kwa nini Wakopeshaji hawa wasiweke wazi kwenye matangazo yao kile watakachokifanya iwapo Mtu atashindwa kumaliza kulipa, kama ni kupelekana kwenye vyombo vya kisheria, kunyang'anywa hicho Kiwanja, au iwapo watarudisha pesa uliyokwisha walipa na haikutimia?.
Kasome mkataba mlioingia achana na matangazo yao ya biashara. Kunakuwaga na mikataba ambayo ni kila hatua za kufanya pindi utakapokiuka mkataba
 
Watakutoza riba, pia utaruhusiwa kujenga baada ya kumaliza deni
 
Back
Top Bottom