Ni nini upya wa Katiba Mpya?

Ni nini upya wa Katiba Mpya?

Kwa hivyo 2014 wananchi walielewa umuhimu wa katiba mpya wakati huo ila leo 2023? Kwa sababu hiyo leo linatakiwa fungu la kutoa elimu?

Hapa chini ni Uzi wako:

Rais Samia, kuhusu Katiba Mpya sisi wasomi tupo tayari kukusaidia kazi ili tupate Katiba nzuri na bora

Huku si ndiko kutega kunguru Kwa maharage makavu mjomba?

Wananchi wanataka katiba mpya wala hawatachuuzwa na wenye nia ovu nyie.
Mkuu Fungu lazima maana wananchi wanahitaji Elimu kwanza na wengi hawajui umuhimu wa Katiba maana watz wengi hawana Elimu na maswala ya kiutawala , kuwapa watu katiba ya Mwaka 2014 bila ufafanuzi nakataa kata Kabisa. Pia Pesa sio vitu vya kuonea Huruma katika kuliletea Taifa Maendeleo .
 
Mkuu Fungu lazima maana wananchi wanahitaji Elimu kwanza na wengi hawajui umuhimu wa Katiba maana watz wengi hawana Elimu na maswala ya kiutawala , kuwapa watu katiba ya Mwaka 2014 bila ufafanuzi nakataa kata Kabisa. Pia Pesa sio vitu vya kuonea Huruma katika kuliletea Taifa Maendeleo .

Huu ulikuwa uzi wako?

Rais Samia, kuhusu Katiba Mpya sisi wasomi tupo tayari kukusaidia kazi ili tupate Katiba nzuri na bora

Soma between the lines. Watanzania si wajinga ki hivyo. 🤣🤣
 
Demokrasi ina gharama zake, na mojawapo ni hiyo ya kurudia uchaguzi ili yule aliyeshindwa ajue kuwa alishindwa kiuhalali. Kenya waliwahi kurudia Uchaguzi wa rais, na najua Marekani kati ya Al-Gore na Bush ilichukua miezi miwili kabla ya ya uchaguzi kuamuliwa ingawa uliamuliwa kiitikadi lakini upande ulioshindwa ulielewa umeshindiwa wapi kikatiba.
Kwetu kuna atakaekubali kushindwa? Tutajikuta kila chaguzi tunatumia miwzi mitatu kubishana. Ila tuache ije hiyo katiba mpya tujifunze kwa vitendo
 
Tatizo lako unaiangalia katiba kwa jicho la CHADEMA ukidhani CHADEMA itakuwepo miaka yote, ukijadili katiba angalia vizazi vijavyo, maana unachokidharau Leo utakuja kukihitaji kesho. Jadili katiba kwa kuangalia manufaa sio CHADEMA.

Kuhusu Kenya, uchaguzi ulikuwa mgumu, waliachana kwa tofauti ya kura laki mbili, Sasa kura laki mbili ni eneo moja la bungoma huko magharibi ndio zilimpatia Ruto ushindi, Sasa unaweza kudispute hizo kura na Uchaguzi ukaenguliwa. Kenya wapo mbali usimuangilie odinga, Kuna vizazi vinakuja vitahitaji kupinga matokeo wakati odinga hayupo.

Nakushauri, unapojadili suala la Katiba usiingize vyama au personalities utaharibu, Bali angalia mambo ya manufaa yanayohitajoka kwenye katiba. Kwa mfano katiba yetu Ina mahakama ya katiba Constitutional Court, lakini hiyo mahakama haijawahi kufanya kazi kwa sababu haitoi locus standi na procedures za kufungua mashauri kwenye hiyo mahakama. Hivyo unaweza kupendekeza katiba mpya iweke hayo mambo muhimu kwenye mahakama ya katiba, lakini kuanza kudai CHADEMA haitashika madaraka au odinga nk, haitasaidia.
Haya yote watanzania hawayaelewi. Ninapoisemea chadema nimamaanisha hata wao hawafanyi kwa maslahi ya taifa bali kwa matumbo yao hata kwa asilimia chache. Hii sio rahisi kunielewa ila nasema tuache katiba mpya ije tujifunze kwa vitendo🤝
 
Back
Top Bottom