Unadhani hata hizo scholarships wanatoa hovyo hovyo tu eti kisa una GPA ya 5?! Trust me, mtu mwenye Upper Second ya UDSM au SUA anaweza kupaar scholarships kirahisi kuliko mwenye First Class kutoka baadhi ya vyuo nchini. Wewe ukitaka kujua vyuo ambavyo wanafunzi wanapata scholarship kirahisi basi angalia tu education background ya lecturers wa vyuo husika! Ukiona Department imejaa lecturers wenye Bachelor hadi PhD wamesomea Bongo basi fahamu chuo husika kina ukame wa kupata scholarships ingawaje pia ni kweli baadhi ya vyuo/vitivo kutokana na expected impact yake basi unakuta wao ni rahisi sana kupata scholarships ukilinganisha na vyuo/vitivyo vingine. Mfano mzuri ni SUA, nilifanya kazi pale miaka 3, na majority ya lecturers wao wamesoma Masters na PhD Canada, Australia na UK hususani kwenye commonwealth universities. Sikuwahi kuuliza sababu ni nini lakini logic tu inaonesha kwa nchi maskini kupata scholarship ya masomo ya kilimo inaweza kuwa rahisi zaidi kuliko, kwa mfano kupata scholarship ya mambo ya accounts.