Ni sahihi Kabisa Mawaziri kusema Kila Kitu Cha Maendeleo kinafanywa na Rais Samia siyo Wao Kwa sababu Rais ndiye Mamlaka Kuu!

Kwamba hatujui ni sifa za kichawa? Huu upuuzi ulishaka kasi kwa kiwango cha juu chini ya utawala wa dhalimu magu.
 
Ni uchawa tu na uchumia tumbo hawana lolote
 
Subiri oktoba tutauliza wao wamefanya nini?
 
Kwani wakiisema vizuri Serikali hawajamsema vizuri Rais?, Kwa mtazamo wangu huko ni kujipendekeza kwenye mamlaka kwa ajili ya kuendelea kuwepo hapo walipo,nadhani hivi sasa kuna chombo kinachopima ni nani aliemtaja sana Rais na kumsifia sana ili aendelee kuwemo kwenye Serikali,wengi wao ndio wanaomwangusha kwa kutimiza wajibu wao na kubaki kumsifia kwenye vyombo vya habari
 
Kodi za wavuja jasho watanzania ndyo maendeleo unayoyaona we masikini wa akili na Mali vinginevyo Bado hiyo Kodi maccm yanaiiba yananeneapa na kuvimbiana mashavu
 
Kwani wakisema maendeleo yanaletwa na serikali ya ccm itakuwa vibaya?
 
si sahihi as if rais ana POWER kama MUNGU i.e Omnipotent & Omnipresent😎
 
Watanzania aisee! Huo ni mkakati wa kichama kumtangaza Samia kwa watanzania ili ajulikane. Before nani alimjua hata wanaccm baadhi walimjulia kwenye mgongo wa JPM
Sasa ili ajulikane kwa wapiga kura wakaja na hiyo Katoa Rais samia.
Kila pesa atoe ana pesa gani? Pesa ni za kwetu.
Ilikuwa sahihi serikali imetoa kama ni kwa maswala ya maendeleo,lakini kama ni misaada huki kwa yatima, makanisani, misikitini au mtu mmoja mmoja sawa hapoa Samia katoa.
 
Ni utamaduni mpya,, ambao nina hakika ni mbaya unaohafifisha fikra pevu. Wakati wa Nyerere, Mwinyi, Mkapa mpaka Kikwete, watu walisema serikali imefanya, lakini ghafla kwa jiwe, Magufuli watu wakaanza ibada kwa Magufuli na kwa Samia imepitiliza zaidi. Kama ni Rais tu amefanya kodi zetu zina kazi gani, na watumishi wanapokea pesa bila kufanya lolote kwa vile Samia ndiye tu anafanya ????? !!!!!!!!! Mwafrica ni ugonjwa. Sifa zingine hata Samia akisikia anashangaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…