Ni sahihi kulaumu upande wa pili?

Ni sahihi kulaumu upande wa pili?

SnowBall

JF-Expert Member
Joined
Sep 13, 2011
Posts
3,052
Reaction score
2,842
Poleni na mfungo kwa wale waislam!

WanaJamvi..ni kawaida katika Mahusiano ya Mapenzi kuwa na rabsha za hapa na pale. Na mara nyngi rabsha hizi huwa zinatokana na hisia za uwepo wa udanganyifu katika Mapenzi (Cheating). Mara nyingi kumekuwa na hatua nyingi ambazo wanaNDOA ama wapendanao huchukua kulinda mapenzi yao pale inapohiswa kuwa mmojawapo sio mwaminifu. Mojawapo ni ile ya ku'attack the other side'!

Mfano..inakuwaje wewe mwanaume um'attack' mwanaume mwenzio kwa sababu tu umesikia anamtongoza au anatembea na mtu wako? wakt mwingine hadi na vitisho vya kuwaua tunawapa. Alikadhalika wewe mwanamke kwa nini na wewe um'attack' mwanamke mwenzio kwa vile umesikia anatongozwa au anatoka na mtu wako??..Kwa nini tuwe na mtazamo wa kuwaona wenzi wetu kuwa they are 'innocent' ispokuwa.. they are put in bad ways by others?

Je, ni sahihi kuwa na mtazamo huu wa kudhani 'wenzi wetu hawana makosa..bali wenye makosa ni wale wanaowafuata'?. Hebu tusaidiane hapa wanajamvi ni kwa mazingira gani tuapply hii theory na yepi tusiiapply??
 
Mimi kwa kweli niki prove mpenzi wangu anatembea na mwanamke flani.. Kwa kweli sitakuwa na muda wa kupoteza na kujiaibisha kwenda kugombana na huyo bi dada maana sijui mpenzi wangu kamweleza nini mpaka akamkubali.. Nita deal na huyo mpenzi wangu mwenyewe..!
 
unajuwa uelewa wako na wangu haviwezi kulingana kabisa nikweli wengi huanza na vitisho, ila kwa mtazamo wangu namaamzi yangu siwezi anza na upande wa pili bali nitaanza na upande wangu. itakuwa kunasababu iliyo msukuma mtu wangu afanye vile na itabidi nimuulize kwa upole ili nipate hasa yaliyo moyoni mwake.
 
Mimi kwa kweli niki prove mpenzi wangu anatembea na mwanamke flani.. Kwa kweli sitakuwa na muda wa kupoteza na kujiaibisha kwenda kugombana na huyo bi dada maana sijui mpenzi wangu kamweleza nini mpaka akamkubali.. Nita deal na huyo mpenzi wangu mwenyewe..!

Umesomeka!
 
unajuwa uelewa wako na wangu haviwezi kulingana kabisa nikweli wengi huanza na vitisho, ila kwa mtazamo wangu namaamzi yangu siwezi anza na upande wa pili bali nitaanza na upande wangu. itakuwa kunasababu iliyo msukuma mtu wangu afanye vile na itabidi nimuulize kwa upole ili nipate hasa yaliyo moyoni mwake.

Sababu huwa ni nini? hapo kwenye red
 
SnowBall huwa ipo sana
Kwani unajikuta wewe umemwamini sana mwenzako na unajiaminisha kabisa kuwa sio yeye kwa hiari yake ameenda upande wa pili
Yaani unajiambia kabisa kuwa alitongozwa na sio yeye aliyejipeleka
Ile imani yako kwa mwenzako ndio inakufanya ujiamini na kumuona mwenzako hana makosa makosa makosa yako kwa yule wa upande wa pili hata kama mtu wako ndio alijitongozesha mwenyewe
 
Last edited by a moderator:
SnowBall huwa ipo sana
Kwani unajikuta wewe umemwamini sana mwenzako na unajiaminisha kabisa kuwa sio yeye kwa hiari yake ameenda upande wa pili
Yaani unajiambia kabisa kuwa alitongozwa na sio yeye aliyejipeleka
Ile imani yako kwa mwenzako ndio inakufanya ujiamini na kumuona mwenzako hana makosa makosa makosa yako kwa yule wa upande wa pili hata kama mtu wako ndio alijitongozesha mwenyewe

Sasa kwa maoni yako mkuu unaona ni sawa?...when do we need to sue our partners?
 
Maumivu ya moyo hushinda akili za kichwa sababu hauko tayari kumpoteza umpendaye.
 
Watu wanaona mabadiliko, kwa vyovyote mtu wako akibadilika lazima kuna kinachombadilisha (haijalishi amekifata au kimemfata). Kuattack upande wa pili ni muhimu wakati ushaattack upande wa kwanza (kwa kistaarabu).
 
Sasa kwa maoni yako mkuu unaona ni sawa?...when do we need to sue our partners?
SnowBall hadi hapo utakapokubaliana na moyo wako kuwa hata partner wako nae ni mdhaifu hapo ndio unaweza kuutoa ukweli wako moyoni
Wengi tunakimbilia kutoa lawama bila kujiuliza about our partner na hilo ni kosa sana
 
Last edited by a moderator:
Watu wanaona mabadiliko, kwa vyovyote mtu wako akibadilika lazima kuna kinachombadilisha (haijalishi amekifata au kimemfata). Kuattack upande wa pili ni muhimu wakati ushaattack upande wa kwanza (kwa kistaarabu).

Kwa hiyo ni vizuri kuanza na upande wako?..then akikuambia kuwa ni 'shetani' tu..then ndo unaenda the other side??
 
Kwa hiyo ni vizuri kuanza na upande wako?..then akikuambia kuwa ni 'shetani' tu..then ndo unaenda the other side??
SnowBall sometime shetani tunamsingizia mambo mengine ambayo hata yeye anaona aibu kutuambia kuwa tunamsingizia
Mwanaume amekuona akakusemesha, mkasemeshana, mkapeana contact, akawa anakutumia sms na kukupigia na unapokea na kumjibu vizuri tuu, akakutoa lunch may be na dinner one day or several time, akakuletea zawadi na ukazipokea bila hata kuuliza, kakuchombeza ukakaa kimya au ukajifaraguza aahhh nina mtu wangu bana, bado akaendeleza sera zake wewe bado una kamsimamo kako japo hakana nguvu, one day isiyo na jina ukamwambia aise twende sehem ila unaiba nina mtu wangu then umalize mambo zako huko uje useme shetani alinipitia
Hakuna cha shetani bana alikuwa na every right to tell the guy stop what u r doing as i have my man
Kukubali kila alichokuwa anakupa bila kuonyesha resistance yoyote ni udhaifu mkubwa mno
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom