pombe kali
JF-Expert Member
- Jun 28, 2014
- 282
- 561
Ni Jambo la kusikitisha na la hatari sana kwenye utawala wa sheria katika zama hizi za upotoshaji wa kimtandao “misinformation era” Teuzi na tenguzi au maTangazo ma kubwa yanayohusu mustakabali wa nchi tunajulishwa kwa barua za msemaji, binafsi nilitegemea liwe Tangazo la serikali “government notice” yaani GN nambari ….ikiwa inaelezea mfano kwa mamlaka aliyopewa na Katiba ya JMT Ibara fulani anatengua au Ana teua, wasomi ni wengi watusaidie Kama zile barua zinazosambaa instagram usiku huwa zina mamlaka kamili ya kuteua au kutengua, tumeona pia kwenye “viclip” kuhusu kufanya ukomo wa muda wa vitambulisho wa taifa Hilo ni Tangazo kubwa na muhimu kwani vitambulisho vilivyotoka awali vilikuwa na ukomo wa muda yaani EXPIRE DATE na vilitoka kwa mujibu wa sheria ya utambulisho wa taifa sasa sidhani Kama ni sahihi sana kutengua chochote kwa kutumia “vi-clip” nategemea ujumbe huu Wenye lengo la kujenga kusambaa na kufika kwa wahusika Kisha kufanyiwa kazi