Ni Samatta au nimsubiri mwingine?

Samatta anasumbuliwa na Majeraha. Na ndio ametoka kurecover soon! Ameshaanza mazoezi ya kuchezea Mpira!

Pale alipofika sio pa kubeza. Na bado ana nafasi ya kwenda MBELE zaidi ya pale! Anaweza asifike EPL, lakini La Liga ama Ligue 1 anaweza kutusua!
 
Samata hafiki EPL,la liga wala bundesliga umri ushaenda yule. Pale alipo amerudisha miaka sita nyuma.

Hii Afrika kurudisha miaka nyuma ishakuwa mazoea sio kwenye mpira tu hata makazini na mashuleni watu wana umri wa kwenye vyeti na umri wa kuzaliwa.
 
Kusema kweli samatta naona kama kutusua mpk epl,la liga au bundesliga inaanza kuwa ngumu
 
Acheni roho za husda, Mbwana msimu huu amekuwa na injury, kacheza games 14 kati ya 21. Lakini bado ni mmoja wa top players kwenye timu.

He is only 25; kama Mboma alitusua on his 30s, akina Drogba wametamba on their late 20s na early 30s, why not Mbwana?
 

Attachments

  • 1E18313B-D938-4BBD-92C6-10BB2ABAF5E8.jpeg
    31.5 KB · Views: 37
Tuna zile Roho zetu zile!
 
Kwahiyo unataka kusema nini?
Ataweza kufanya yale ninayotarajia?
 
Atafikia kiwango cha kina sadio mane au m salah
ngoja tusubiri tuone....
 
ndio nakwambia me nimecheza nae mtaani tangu mpaka mbagala market,kwa rika ni kakaangu na mimi hapa nina 28 now jiulize yeye atakuwa na mingapi
Hata wachezaji WA west Africa ndio tabia yao..kushusha umri..Kumbuka Michael Essien,nwakno kanu,Pius ndiefi nk
 
Akiwa nje ya majeraha ya mda mrefu bado naona ana nafasi ya kusonga mbele zaidi.

Majeraha ya mda mrefu hua yanaua kabisa ndoto chanya za wanamichezo.

Kwakua unakua unaanza kupoteza ile grip uliyokua nayo,confidence inashuka,unapoteza washabiki na wanaokufuatilia wanaanza kuvunjika mioyo.

Binafsi namuombea awe fiti muda wote,naamini Samatta akiwa fiti bado anamuendelezo mzuri.
 
ndio nakwambia me nimecheza nae mtaani tangu mpaka mbagala market,kwa rika ni kakaangu na mimi hapa nina 28 now jiulize yeye atakuwa na mingapi
kwani kucheza na mtu ndo kulingana umri? hoja yako haina mashiko
 
hata hapo alipo ni mafanikio makubwa sana kwa kijana ambaye hakuwa kwenye misingi madhubuti ya soka utotoni, ni juhudi tu ndo zimempa mafanikio, nidhamu kubwa na usikivu...siyo kama kama akina kichuya anatolewa anaweka earphone as if amekuwa cr7.
 
kwani kucheza na mtu ndo kulingana umri? hoja yako haina mashiko
unajua tofauti ya maneno RIKA na UMRI au kwa sababu una smartphone na bundle basi unajiona mjuaji. Shithole!!!
 
Sana
Hata wachezaji WA west Africa ndio tabia yao..kushusha umri..Kumbuka Michael Essien,nwakno kanu,Pius ndiefi nk
Ni kawaida Yao hao,angalia Ile timu ya vijana u17 waliocheza Na serengeti yaani kuanzia kipa hadi striker wote vijeba.
 
Ataweza kufanya yale ninayotarajia?
Unayotarajia wewe kama nani? Wewe ni Samatta?
Yaani watu bwana!! Yaani mtu hata hajafanikisha lolote kumfikisha Samatta alipo leo, halafu anasema hata “ataweza kufanya yale ninayotarajia”?!?
 
Hata Yesu alitanguliwa na Yohana mbatizaji.

Inabidi aende mtu kufungua njia kwanza, huyo kazi yake itakuwa kufungua njia tu, wakija wengine wakiulizwa "mnatoka wapi?" waweze kusema "Tanzania, kwao Mbwana Samatta".

Sio mtu unaulizwa unatoka wapi,unasema Tanzania, watu wanakuuliza "Tasmannia? Australia au wapi?

Kwa hiyo Smatta kafungua njia, Hashimu Thabit kafungua njia.

Hawa wameiweka Tanzania kwenye ramani, wengine wafanye kweli.
 
Step by Step
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…