Ni sawa kumficha mme/mke wako kiasi cha mshahara wako?

Tangopori

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2012
Posts
1,628
Reaction score
1,285
Wanajf tujadili hili.
Kwa upande wangu mimi naona wanawake wanakuwaga sensitive sana na pesa so akijua kiasi cha mshahara wako atakuwa anafuatilia kila senti inapokwenda hata ukikutana na rafiki zako mkachoma nyama basi lazima ahoji hizo hela zimeenda wapi. So hatakiwi kujua.
 
Inategemea na makubaliano yenu kama hutaki ajue mshahara wako na wewe usitake kujua wa kwake,simple and clear!
 
mmh..sasa mkifichana then mtapangaje budget za nyumban,na mipango mingine ya siku za usoni ya maisha yenu...kwa ajili ya watoto n mengineo..
 
inategemea na malengo yenu kwenye maisha, kama mpo mpo tu mradi liende mfiche, ila kama mnataka kupanga kesho yenu kioa mmoja kipato chake kijulikane na mkubaliane mchango wenu utakua vipi
 
Si vizuri kufichana vipato vyenu
 
Kama huna "magendo" it is okay.... haya ya kuchoma nyama kwani kila siku?? itakuwa tabu kama home kila siku RB (Rice & Beans) ..... Hapo patakuwa na shida but if it is for some few days in a month na pia home mambo safi mie sioni tabu ya yeye kuujua mshahara wangu na pia nyama nitachoma tu.
 
ila kusema ukweli kwa mwanamke /mwanaume anaeficha mshahara wake hana fikra za kimaendeleo na mwenza wake..
 
ajue asijue for me it doesnt matter, jasho ni la kwangu so nitatumia hela yangu vile nataka, tuna hobbies tofauti so kila mtu ataspend hela yake vile anavopenda...
 
Hiyo ni tabia ya mke wako, Sio wote Wapo hivyo, jibu la hili swali ni "inategemea na Mwanamke"

 
nimeshashuhudia jamaa amekufa na mke na watoto wanashindwa kujua na kufatilia masalia ya mme/baba yao

kama unaishi na mtu ndani na kila kitu mnashare inakuwaje mfichane mambo ya kimaisha kam a hayo?
 
Mkeo kujua kipato chako sio vibaya. Ila kibaya ni huyo mwanamke kutawala hicho kipato chako, Utashindwa hata kukaa na washikaji kunywa Castle lite.
 
kama tunafichana mapato, haina haja ya kuishi pamoja, ni kutalikiana ndio suluhisho pekee.
 
Mkeo kujua kipato chako sio vibaya. Ila kibaya ni huyo mwanamke kutawala hicho kipato chako, Utashindwa hata kukaa na washikaji kunywa Castle lite.


Kweli kabisa.....maaana wengi wanatabia hiyo ya kuutawala mshahara wa mwanaume......ila mishahara yao hujifanya wamelipia deni kwa muuza nguo,kaendea salon......
 
Mara kunapokuwa na deficit za apa na pale home ndo hayo mambo ya kujua viapato vya wenza huingia.
Kama kila kitu kinaenda shwari kudeclare vipato haitakiwi kuwa issue.
Kuna watu wanapanga mambo ya maendeleo ya kila mmoja hajui kipato cha mwenzake
 
Pesa yangu ni yake, na yake ni yake...wanaume hutupendi pesa tusizo zitolea jasho.

Mimi huwa namuwachia kabisa wife card ya bank.
 
Inategemea kwa sababu wengi huingia ndani ya ndoa bila uhakika wa kuishi Tugeza Foreva ndo maana kwao vipato vyao ni siri kwa wenzi wao...Ila sisi wenye mapenzi mema na ndoa Huwa tunashare hizo taarifa...Its just money when u die u wont go with it. Kwanza kama mwanaume majukumu ya ndoa unayajua vizuri ni lazima mkeo ajue mshahara wako and likewise because a wife belongs to the husband and the husband belongs to the wife...
 
hongera sana fazaa, wanawake hatuko hivyo vile mnafikiri nyie. mbona ukiacha sh 1000 nyumbani unakuta umepikiwa chakula kizuri mbona huulizi nimeacha pesa kidogo lakini nakula vizuri??
 
mambo ya kupanga budget na future za watoto ni ya baba (kichwa cha nyumba). anaweza kunihusisha nimsaidie akitaka. mimi za kwangu nitamuongezea inapobidi hivyo hana sababu ya kujua income yangu, japo kwa mapenzi yangu naweza kumwambia income yangu, hapaswi kunilazimisha kama sitaki. yeye akiniambia ya kwake ni vizuri ili nijui naziba pengo wapi kama lipo la kuziba.

mmh..sasa mkifichana then mtapangaje budget za nyumban,na mipango mingine ya siku za usoni ya maisha yenu...kwa ajili ya watoto n mengineo..
 
Kiukweli ni muhimu sana kimaendeleo wenzi kuweka kipato mezani na kutekeleza mipango yao ya maendeleo kila mwisho wa mwezi.Bila kufanya hivi kila mmoja atakuwa na priority zake mfano kusaidia kwao n.k. Hivyo basi ile take home ni vyema kabisa ikawa wazi. ijapokuwa mafanikio ya kufanya hivi inategemea sana insight na enthusiasism ya wote wawili kwani maisha ni kuchagua. Kwa ushauri ni vema zile pesa zinazotokana na dili mbalimbali nje ya mshahara ndo sehemu yake zilie bata otherwise kazi ipo. Hata mshahara si mbaya kutoa 50% kwa matumizi na 50% nyingine maendeleo.Ahksanteni.
 
Kweli mimi pia sipendi kuulizwa kuna wanaume wengine wakijua kipato hasa kikiwa kikubwa wanachukua advantange. Joint account ni bora kutatua matatizo ya nyumbani or any other future plans. Kila mtu anajua kiasi gani anachangia kwahiyo any spending should not come from joint account, I won't intefere.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…