Ni shida nimetembelea kijijini hukooo ndani ndani,alooo !

Shocker

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2012
Posts
1,958
Reaction score
3,890
Nilikuwa nikae mwezi lakini yamenishinda,kuoga kisimani kwenda haja kubwa au ndogo ni kwenye machaka unakuta hakuna chaka ni minazi mitupu ,usiku ukitaka kwenda haja ndio kindende.

Nimetaka kuwachimbia choo wakasema arzi yao ina maji,hivi mpo mmezoea hii hali wakiti mkitoka mjini au ulaya.
 
Kuna vijijin kila ikifika wakati wa kutaka kuoga au kunya unawaza sana,mazingira hayaruhusu
 
Kuna vijijin kila ikifika wakati wa kutaka kuoga au kunya unawaza sana,mazingira hayaruhusu
Hilo ni tatizo nimekumbana nalo nilivumilia lakini uzungu ulinishinda nikajiunga na ushamba ,siku iliyofuata majembe,ahh mambo ya kuelekea kusikojulikana na bilika la maji.
 
Daaaahhhhhu

Huo ndio uchumi wa kati wanaounadi akina Kalemani na Or. Palamagamba kabudi
 
Ujumbe happo Ni ukosefu wa vyoo kwa baadhi ya familia.. lakini Dah nilichogundua Ni Kwamba huyu mshikaji ndo wale wakataa kwao... Choo Ni muhim ulisahau Kwamba maskani hamnaga choo umeamua kuwachora?
Nb. Mkisoma mkafanikiwa japo kidogo jengeni kwenu nyumba, vyoo nk. Kifo hutokea Kila siku ikitokea umeitwa na mola marafiki zako wasikung'ong'e Kwamba ulikua unaigizA ujanja hata choo hakunaga, hata kijumba Cha maiti hakuna..
aibu! Aibu
 
Daah kwa hali hio unabaki kujiuliza wanaishije hapo
 
Utumie choo kwan wew ni mwanamke!?😃😃
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…