Hii imenikumbusha kampala, kuna kijiclab kinavuma sana kinaitwa top club! Kuna machangudua balaaa! Basi nimefika pale ili nipate nyama choma na nile bear adhaa, ile natoka mida ya saa 7 hivi, kuna kahaba moja akajidai kanikubali, akawa ananipapasa papasa hivi, mara nikahisi ameingiza mkono kwenya mfuko wa mbele wa kijipensi changu, kuhamaki akazama mfuko wa nyuma na kuibuka na walete, aki pombe zilikata! Alivyogeuka sikutegemea, alitoka nduki kuelekea kwenye danguro lao, mimi nyuma mbio, kufika getini akachomoa hela iliyokuwa kwenye waleti na kirusha kwenye kingo ya ngazi, yeye akapotea na waleti haina kitu, kumbe mimi nimeona, kufika nikawahi zile pesa km zilivyo! Wenzake km 13 hawakujua ni nini nimechukuwa kwenye ngazi, walinidaka juujuu, nilihisi ndio mwisho wangu! Ila nilikukuruka kwa nguvu zangu zote, nikawszidi kisha nikaongoza kumfuata yule kahaba juu ghorofani, kufika kule watu wakawa wananishaangaa tu, nawaeleza jamani nimeibiwa, hawanielewi, kuna kahaba mmoja akanifuata akaniuliza, unataka wallet yako hutaki, nikamwambia nataka, ok basi toka nje utapata wallet yako, nikatoka nje, kweli ile nashangaanikaona waleti inarushwa toka gorofani, nikaichukuwa nikasepa kurudi hotelini. Uzuri hawakuchuwa hata senti tano, toka siku hiyo nimeapa top club sikanyigi!