Ni ubatili na ukandamizaji kuwaongezea posho ya Tsh. 130,000 wenye mishahara mikubwa na Tsh. 20,000 wenye mishahara midogo

Ni ubatili na ukandamizaji kuwaongezea posho ya Tsh. 130,000 wenye mishahara mikubwa na Tsh. 20,000 wenye mishahara midogo

Subira the princess

JF-Expert Member
Joined
Mar 3, 2018
Posts
3,474
Reaction score
3,744
Wasalaam.

Katika Serikali ya awamu ya 4 chini ya Jakaya Kikwete posho ya kujikimu safarini kima cha chini ilikua elfu 80 na cha juu ilikua 120,000 tofauti ilikua elfu 50.

Katika awamu ya tano chini ya Magufuli yeye hakuongeza wala hakupunguza aliacha kama ilivyo japo alitamani kuzifuta kabisa na kuzipeleka kwenye miradi ya maendeleo.

Katika awamu ya sita chini ya mama Mamia ameongeza kima cha chini kutoka 80 mpaka 100,000 na kima cha juu kutoka 120,000 mpaka 250,000 tofauti badala ya kupungua imepanda 130,000

Ukichunguza hivyo viwango unaona Serikali ya awamu ya 6 imeamua kufanya ukatili mkubwa kwa Watumishi wa Umma walio wengi na kuwaneemesha wachache wenye mishahara mikubwa, yaani mwenye nacho anaongezewa na asie nacho ananyonywa damu.

Inashangaza mwenye mshahara mdogo anaongezwa 20,000 na yule mwenye mshahara mnono anaongezwa 130,000 huu ni ubatili na ukandamizaji.

Hitimisho
Mtumishi wa Umma au raia anaeshangilia usanii na udhalimu huu akapimwe akili.
 
Mwenyekiti kaishaunga juhudi mkono ndomaana hauwezi kusikia yeye kama kiongozi wa upinzani na genge lake wanaongea upuuzi huu. Sasa chawa bado mnaendeleza siasa za kupinga pinga kila jambo, sijui safari hii nani atawalipeni!


images (68).jpeg
 
Mama kwa Sasa haupigi mwingi Bali anaubutua, binafsi namkubali sana, maana ndani ya mwaka wake mmoja wa utawala mshahara wangu umepata ongezeko la sh 200,000+ ,

Itoshe tu kusema kwamba mama atawale milele, kinachoniuma Ni kuwa siku hizi zile kelele za tubadilishe katiba atawale milele hazipo tena, Ila kati ya watu ambao wanafaa kutawala milele huyu ndo wa Kwanza.

Long live mama samia
 
Amenyekiti kaishaunga juhudi mkono ndomaana hauwezi kusikia yeye kama kiongozi wa upinzani na genge lake wanaongea upuuzi huu. Sasa chawa bado mnaendeleza siasa za kupinga pinga kila jambo, sijui safari hii nani atawalipeni!
Kwa hiyo unatakaje?
 
Hii ni motisha kwa watumishi wa chini, wasome na wafanye kazi kwa bidii, ili nao wasogee sogee
 
Back
Top Bottom