Ni ubatili na ukandamizaji kuwaongezea posho ya Tsh. 130,000 wenye mishahara mikubwa na Tsh. 20,000 wenye mishahara midogo

seems hukijui unachoongea,
watu washapandishwa madaraja kitambo, na mafao/madeni yao washalipwa
 
seems hukijui unachoongea,
watu washapandishwa madaraja kitambo, na mafao/madeni yao washalipwa
Inawezekana sijui ...sijakupinga
Ninachofahamu Kuna ambao wamepandishwa na Kuna wengine wanaendelea kupandishwa na Kuna walojaza form za malimbikizo Bado kupata na Kuna waliopata ...sidhani km spidi hiyo ya kupandishwa imekava zaidi ya asikimia 60. Ya wanaostahili.
Kwa ustarabu gap la posho ni kubwa mno kati ya watu wa chini na WA juu.sitapenda wawashushe wa juu Ila ningependa. Wawaongezee wa chini
 
Kwa kifupi acha mvua inyeshe tuone panapovuja, then wafanyie kazi,
 
Sasa kama ni hivyo mkuu, watetezi (wapinzani) wapo kwa ajili ya nini? Au kwa ajili ya matumbo yao wao na familia zao?
Wapinzani si watetezi watetezi ni wananchi wenyewe, mbona kila siku mahakama zinalalamika kwa watu kutokwenda mahakamani kutoa ushahidi.
Watanzania tunashindwa kwa kuamini eti wapinzani ni watetezi, nchi zote wananchi bila kujali itikadi huingia mitaani kudai haki zao ndiyo maana wanasonga mbele.
 
Kawaida mzee haiwezekani kuwa sawa kama vidole tu
 
Ok nimekuelewa mkuu.
 
Si mlisema Mama anaupiga mwingi Hadi unamwagika acha aupige mwingi
 
Mshahara kima Cha chini nyongeza 23% wakati posho ambazo mara nyingi zinawahusu wakubwa zimepandishwa kwa zaidi ya 100% .jambo hili ni dhihaka kwa watumishi wa ngazi za chini.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Ila serikalini kila kitu wanaangalia salary grade, kwenye taasisi za kueleweka posho za kujikimu hasa hizi za safari zipo sawa kuanzia Dereva mpaka wale kina "top manyota", kwa sababu tayari wameshatofautiana mishahara kutokana na elimu na uzoefu na mambo mengine, sasa kuna sababu gani na kwenye posho za safari kuwatenganisha wakati ugumu wa maisha wa ugenin wote wanaupata sawa. Ajabu dereva anakabidhiwa VIETEE alafu anapewa 80,000 na anafikia sehemu ya hovyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…