Ni ugaidi Jeshi kupiga Wananchi wasio na hatia kisa wanaonesha hasira za mwenzao/wenzao kudhuriwa na mtu/kikundi fulani

Ni ugaidi Jeshi kupiga Wananchi wasio na hatia kisa wanaonesha hasira za mwenzao/wenzao kudhuriwa na mtu/kikundi fulani

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
NI UGAIDI JESHI KUPIGA WANANCHI WASIO NA HATIA KISA WANAONYESHA HASIRA ZA MWENZAO/WENZAO KUDHURIWA NA MTU/KIKUNDI FULANI.

Anàandika, Robert Heriel
Kamanda wa Tibeli.

Kuna ile tabia ambayo sasa nadhani imezoeleka ya kulichafua jeshi letu au baadhi ya wanajeshi wasiowaadilifu kuchafua kazi ya uanajeshi kwa kufanya matendo ya kidhalimu, matendo yasiyo ya haki. Jambo ambalo kwa sisi Watibeli halikubaliki, na tunalipinga kwa kinywa kipana pasipo kumung'unya maneno kuwa tabia hizo ni mbaya na lazima zikemewe na watu wote waungwana na waadilifu.

Moja ya tabia hizo ni pamoja na tabia ambayo nimeihusisha na ugaidi.
Tabia ya kupiga na kudhuru wananchi wasio na hatia kisa na mkasa ati kulipa kisasi cha kijinga baada ya mwanajeshi kupigwa au kudhuriwa na Rais fulàni au kikundi fulani cha Watu.

Yaani ati mimi leo niingie kwenye mgogoro na jirani yangu mjeshi, au nipo Bar nipo kwenye ishu zangu za starehe mara nimeingia mgogoro na mjeshi tukazichapa na nikampiga au kumdhuru. Ati kinachofuata ni eneo hilo au mtaa ninaoishi kupokea kichapo hata kwa wasiohusika. Huo ni ugaidi, ukatili, na udhalimu.

Wanajeshi tunajua wazi kuwa nidhamu na uadilifu ndio kanuni zinazotuongoza. Nidhamu ni kujiheshimu, kuheshimu muda, kuheshimu Watu wakubwa kwa wadogo. Uadilifu ni kutenda mambo kwa weledi na kwa Haki.

Mwanajeshi halisi na muadilifu hawezi kupiga raia asiye na hatia ati kisa kulipa kisasi cha mtu au kikundi fulani kilichomdhuru mwanajeshi mwenzake. Huo sio uadilifu. Huo sio uanajeshi.

Hiyo kasumba iondoke. Hiyo tabia ikemewe. Wanajeshi ni Vijana wetu, Baba zetu na wajomba zetu, Dada, mama na shangazi zetu. Heshimuni maadili ya kazi yenu. Hiyo ndio namna ya kulifanya jeshi letu lipendwe na lilinde heshima yake.

Najua wapo wanajeshi waungwana na waadilifu ambao wanaelewa kile ninachokizungumzia.

Mwanajeshi lazima uelewe kuwa unapokuja huku uraiani wewe ni raia tuu kama raia wengine. Lazima ufuate sheria za nchi na uheshimu Watu ili na wewe uheshimiwe.

Tena Raia huwapa upendeleo kwa sababu wanajua umuhimu wa kazi yenu. Lakini tabia ya kulazimisha upendeleo na heshima ndio inayoleta matata na changamoto huku mitaani.
Unaleta ubabe na dharau kwa kinga ya jeshi. Yaani unalitumia jeshi vibaya. Huo sio uadilifu.

Niheshimu uheshimiwe. Elewa kuwa utakapoingia kwenye mgogoro na mtu utaingia wewe kama wewe na sio jeshi. Kulitumia jeshi kwenye shughuli zisizoza kiadilifu ndiko kunakolichafua jeshi.

Tabia hiyo ikemewe. Na wenye tabia hizo wachukuliwe hatua kali naza dhahiri ili iwe fundisho katika nchi.

Nipumzike sasa.
Sabato njema.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Nasikia uko kawe ni kipigo kinatembea mkuu.

Wakati mtuhumiwa wa tukio aliemuua kanali muro kashakamatwa ila wanapiga wananchi na watu ambao wapo kwenye Ile bar kanali aliyokuwa anakunywa.
 
Nasikia uko kawe ni kipigo kinatembea mkuu.

Wakati mtuhumiwa wa tukio aliemuua kanali muro kashakamatwa ila wanapiga wananchi na watu ambao wapo kwenye Ile bar kanali aliyokuwa anakunywa.

Huo ni upuuzi. Unadhalilisha jeshi letu
 
Wapumbavu wapo jeshini japo ni wachache sana, lakini ndio huharibu sifa ya jeshi.
 
NI UGAIDI JESHI KUPIGA WANANCHI WASIO NA HATIA KISA WANAONYESHA HASIRA ZA MWENZAO/WENZAO KUDHURIWA NA MTU/KIKUNDI FULANI.

Anàandika, Robert Heriel
Kamanda wa Tibeli.

Kuna ile tabia ambayo sasa nadhani imezoeleka ya kulichafua jeshi letu au baadhi ya wanajeshi wasiowaadilifu kuchafua kazi ya uanajeshi kwa kufanya matendo ya kidhalimu, matendo yasiyo ya haki. Jambo ambalo kwa sisi Watibeli halikubaliki, na tunalipinga kwa kinywa kipana pasipo kumung'unya maneno kuwa tabia hizo ni mbaya na lazima zikemewe na watu wote waungwana na waadilifu.

Moja ya tabia hizo ni pamoja na tabia ambayo nimeihusisha na ugaidi.
Tabia ya kupiga na kudhuru wananchi wasio na hatia kisa na mkasa ati kulipa kisasi cha kijinga baada ya mwanajeshi kupigwa au kudhuriwa na Rais fulàni au kikundi fulani cha Watu.

Yaani ati mimi leo niingie kwenye mgogoro na jirani yangu mjeshi, au nipo Bar nipo kwenye ishu zangu za starehe mara nimeingia mgogoro na mjeshi tukazichapa na nikampiga au kumdhuru. Ati kinachofuata ni eneo hilo au mtaa ninaoishi kupokea kichapo hata kwa wasiohusika. Huo ni ugaidi, ukatili, na udhalimu.

Wanajeshi tunajua wazi kuwa nidhamu na uadilifu ndio kanuni zinazotuongoza. Nidhamu ni kujiheshimu, kuheshimu muda, kuheshimu Watu wakubwa kwa wadogo. Uadilifu ni kutenda mambo kwa weledi na kwa Haki.

Mwanajeshi halisi na muadilifu hawezi kupiga raia asiye na hatia ati kisa kulipa kisasi cha mtu au kikundi fulani kilichomdhuru mwanajeshi mwenzake. Huo sio uadilifu. Huo sio uanajeshi.

Hiyo kasumba iondoke. Hiyo tabia ikemewe. Wanajeshi ni Vijana wetu, Baba zetu na wajomba zetu, Dada, mama na shangazi zetu. Heshimuni maadili ya kazi yenu. Hiyo ndio namna ya kulifanya jeshi letu lipendwe na lilinde heshima yake.

Najua wapo wanajeshi waungwana na waadilifu ambao wanaelewa kile ninachokizungumzia.

Mwanajeshi lazima uelewe kuwa unapokuja huku uraiani wewe ni raia tuu kama raia wengine. Lazima ufuate sheria za nchi na uheshimu Watu ili na wewe uheshimiwe.

Tena Raia huwapa upendeleo kwa sababu wanajua umuhimu wa kazi yenu. Lakini tabia ya kulazimisha upendeleo na heshima ndio inayoleta matata na changamoto huku mitaani.
Unaleta ubabe na dharau kwa kinga ya jeshi. Yaani unalitumia jeshi vibaya. Huo sio uadilifu.

Niheshimu uheshimiwe. Elewa kuwa utakapoingia kwenye mgogoro na mtu utaingia wewe kama wewe na sio jeshi. Kulitumia jeshi kwenye shughuli zisizoza kiadilifu ndiko kunakolichafua jeshi.

Tabia hiyo ikemewe. Na wenye tabia hizo wachukuliwe hatua kali naza dhahiri ili iwe fundisho katika nchi.

Nipumzike sasa.
Sabato njema.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
JWTZ inapaswa kuwa jeshi la wananchi kivitendo na siyo nadharia

Haya maushubwada yanayoendelea yamefanikiwa kwa hisani ya CCM

Amiri Jeshi Mkuu hawezi kuguswa wala kustushwa na matendo maovu ya wanajeshi dhidi ya raia. Seems atastushwa siku mwanafamilia wake akipewa kichapo na hao wanajeshi wake
 
Wasikemewe wachukuliwe hatua.
Wafikishe mahakama ya kijeshi na kufukuzwa kazi.
Hao ni wahuni tu waliokosa sifa za kuwa askari wa jeshi lenye kuheshimika.

Msingi wa majeshi ni nidhamu, kuvunja sheria ni ukosefu wa nidhamu.
Kama wakati wa Kikwete na Mwamunyange alidhibiti tabia hizi kwa kufukuzwa kazi wahuni kama hao basi na sasa inawezekana.
 
1. Je! Hi story inavyotanda mnauhakika nayo, mmefanya uchunguzi?

2. Wewe robert tukio lililotokea inawezekana hiyo ni ambush kupata wahusika. Maana kawe ni eneo la jeshi. Na ni haki kulinda eneo maana linatumika na raia. Kupotezea tu, kunaweza leta maafa kwa jamii inayozunguka hapo, siku za usoni.
Ambush is a must. Haswa kwenye mauaji ya kushtukiza kama hayo tena Kwa Mkuu wa jeshi wa nafasi ya huyo bwana jeshini.

Zaidi bado naona kama blunders tu, maana hakuna real story mbele yangu bado
 
NI UGAIDI JESHI KUPIGA WANANCHI WASIO NA HATIA KISA WANAONYESHA HASIRA ZA MWENZAO/WENZAO KUDHURIWA NA MTU/KIKUNDI FULANI.

Anàandika, Robert Heriel
Kamanda wa Tibeli.

Kuna ile tabia ambayo sasa nadhani imezoeleka ya kulichafua jeshi letu au baadhi ya wanajeshi wasiowaadilifu kuchafua kazi ya uanajeshi kwa kufanya matendo ya kidhalimu, matendo yasiyo ya haki. Jambo ambalo kwa sisi Watibeli halikubaliki, na tunalipinga kwa kinywa kipana pasipo kumung'unya maneno kuwa tabia hizo ni mbaya na lazima zikemewe na watu wote waungwana na waadilifu.

Moja ya tabia hizo ni pamoja na tabia ambayo nimeihusisha na ugaidi.
Tabia ya kupiga na kudhuru wananchi wasio na hatia kisa na mkasa ati kulipa kisasi cha kijinga baada ya mwanajeshi kupigwa au kudhuriwa na Rais fulàni au kikundi fulani cha Watu.

Yaani ati mimi leo niingie kwenye mgogoro na jirani yangu mjeshi, au nipo Bar nipo kwenye ishu zangu za starehe mara nimeingia mgogoro na mjeshi tukazichapa na nikampiga au kumdhuru. Ati kinachofuata ni eneo hilo au mtaa ninaoishi kupokea kichapo hata kwa wasiohusika. Huo ni ugaidi, ukatili, na udhalimu.

Wanajeshi tunajua wazi kuwa nidhamu na uadilifu ndio kanuni zinazotuongoza. Nidhamu ni kujiheshimu, kuheshimu muda, kuheshimu Watu wakubwa kwa wadogo. Uadilifu ni kutenda mambo kwa weledi na kwa Haki.

Mwanajeshi halisi na muadilifu hawezi kupiga raia asiye na hatia ati kisa kulipa kisasi cha mtu au kikundi fulani kilichomdhuru mwanajeshi mwenzake. Huo sio uadilifu. Huo sio uanajeshi.

Hiyo kasumba iondoke. Hiyo tabia ikemewe. Wanajeshi ni Vijana wetu, Baba zetu na wajomba zetu, Dada, mama na shangazi zetu. Heshimuni maadili ya kazi yenu. Hiyo ndio namna ya kulifanya jeshi letu lipendwe na lilinde heshima yake.

Najua wapo wanajeshi waungwana na waadilifu ambao wanaelewa kile ninachokizungumzia.

Mwanajeshi lazima uelewe kuwa unapokuja huku uraiani wewe ni raia tuu kama raia wengine. Lazima ufuate sheria za nchi na uheshimu Watu ili na wewe uheshimiwe.

Tena Raia huwapa upendeleo kwa sababu wanajua umuhimu wa kazi yenu. Lakini tabia ya kulazimisha upendeleo na heshima ndio inayoleta matata na changamoto huku mitaani.
Unaleta ubabe na dharau kwa kinga ya jeshi. Yaani unalitumia jeshi vibaya. Huo sio uadilifu.

Niheshimu uheshimiwe. Elewa kuwa utakapoingia kwenye mgogoro na mtu utaingia wewe kama wewe na sio jeshi. Kulitumia jeshi kwenye shughuli zisizoza kiadilifu ndiko kunakolichafua jeshi.

Tabia hiyo ikemewe. Na wenye tabia hizo wachukuliwe hatua kali naza dhahiri ili iwe fundisho katika nchi.

Nipumzike sasa.
Sabato njema.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Jeshi lenye watu waoga waoga ndiyo huwa lina tabia za namna hiyo.
Wakati wa Mwendazake waliufyata, walipigwa biti na hadi Makondakta wa daladala na wengine nauli walilipishwa, walipomuona Bashite walichanganyikiwa na ili kujipendekeza walimkimbilia kupiga naye selfie.

Kama kipindi kike waliufyata, sasa hayupo ndiyo wanaibuka na matukio ya namna hiyo ili tujue na wenyewe wapo, tafsiri yake ni moja tu hapo kuwa tuna watu waoga-waoga ambao hujipima kwa kuumiza raia.

Wanajeshi wenzao wapo huko kwenye misheni ngumungumu za kuliweka taifa salama, hawa wafyeka majani kambini ndiyo wanabaki uraiani kudharirisha na kuumiza raia.
Tunaishi kwenye dunia ya kidigitali, sura zao wengi zimeshanaswa na camera, ni jukumu la Polisi kuanza kuwatafuta hao waharifu wanaojificha kwenye kivuli cha JW na kuanza kuwadaka mmoja baada ya wengine na kuwafikisha Mahakamani.
Hii poa ni kwa usalama wao, maana raia wanaweza pia na wao wakaanza kuwatafuta mmoja mmoja huko mitaani kitu ambacho kamwe si afya kwa taifa.
Akari halisi ni yule asimamae kwenye kanuni na maadali. Askari mwenye maadili na mafunzi hawezi akatumia uaskari na Mafunzo yake kuumiza na kudharirisha raia. Hao waliofanya hayo wamejithibitisha kuwa hawakuiva kimafunzo.
Ningeunga mkono kama mharifu angekuwa hajapatikana, lakini mtu yupo mikononi mwa Polisi wao wanaenda kupiga raia mitaani. Kama wao ni Askari kweli si watafute kituo cha Polisi anachoshikiliwa huyo mtuhumiwa wakakivamie na kumtoa huko? Au wanawaogopa Polisi?
 
Huo ni upuuzi. Unadhalilisha jeshi letu
Ni mamlaka tu ndizo zinazolinda upuuzi huo!! Ndio maana unaona kila mala hayo kutokea japo yamepungua sana miaka hii!! Kutokana na watetezi wa haki za binadamu!! Tunazidiwa hata na DRC, kila siku utasikia mjeda amejichanganya amehukumiwa kifo!! Kama tukio hilo la juzi pongezi ni kwa polisi kama wangemkabidhi huyo kijana kwa wao, wangumuua, na hakuna kitu wangefanywa!! Yaani nch hii mjeda anataka kuchukuliwa kama Malaika!!
 
Back
Top Bottom