Habari wana Jamvi.
Nna Mtoto wa Kiume Umri miaka miwili na nusu 2.5 sijamfanyia tohara na niliacha kumfanyia mapema kulingana na mila na desturi za kwetu maana mie Baba ake nilifanyiwa nikiwa kidato cha pili.
Sasa leo mtoto amenishtua kidogo ametoka kuogeshwa akamwambia Mama ake
''Mama nataka kukata dudu yangu"
tukatafsiri kuwa majirani wanaomzunguka a watoto anaocheza nao wote wamekatwa yaani wamefanyiwa tohara tukahisi labda watoto wenzake wamemwambia lazima akatwe.
je akiendelea kuachwa hivyo hivyo hakuna siku tunaweza pata amejikata dudu yake?
je Umri sahihi kiafya ni upi hasa?
Kwa faida ya wanajamvi.
Kwa kawaida mtoto akizaliwa tu kama hana tatizo lolote la kiafya inashauriwa kumtahiri baada ya Massa 24 hadi siku 60 or 8wks
Faida mojawapo za Kumfanyia tohara mapema ni kama vile;
kidonda kupona haraka (ndani ya siku 7-14)baada ya kufanyiwa
Maumivu yake yatakua kidogo au kw muda mfupi tofauti na mtoto aliye kua
Ni rahisi kumfanyika pia damu inakua kidogo au isiwepo kabisa kulinganisha na mtotot aliekua kwa sababu mishipa ya damu bado haijakomaa na kua mingi .
Mtoto haitaji kushonwa nyuzi yoyote tofauti na aliye fikisha miezi mingi.
Ni rahisi sana kwa mama kumshika na kumuhudumia baada ya procedure
Inaepusha sana magonjwa ya UTI kwa mtoto
Mda mzuri wataalaam wanashauri mpaka mtoto anafikisha miaka miwili ni vizuri zaidi akafanyiwa circumcision.!
Lakini kw ushauri zaidi jaribu kumpeleka mwanao Hosp wao watakueleza vzuri maana bado mtoto yupo kwene umzuri.!
Zipo faida nyingi kupita maelezo