Ni Umri Gani Mwafaka Wa Kumfanyia Mtoto Tohara?

Ni Umri Gani Mwafaka Wa Kumfanyia Mtoto Tohara?

Duh! Mi niliganda nalo hadi namaliza shule ya msingi wala halijawahi kuniletea madhara yoyote
 
Habari wana Jamvi.

Nna Mtoto wa Kiume Umri miaka miwili na nusu 2.5 sijamfanyia tohara na niliacha kumfanyia mapema kulingana na mila na desturi za kwetu maana mie Baba ake nilifanyiwa nikiwa kidato cha pili.

Sasa leo mtoto amenishtua kidogo ametoka kuogeshwa akamwambia Mama ake

''Mama nataka kukata dudu yangu"

tukatafsiri kuwa majirani wanaomzunguka a watoto anaocheza nao wote wamekatwa yaani wamefanyiwa tohara tukahisi labda watoto wenzake wamemwambia lazima akatwe.

je akiendelea kuachwa hivyo hivyo hakuna siku tunaweza pata amejikata dudu yake?

je Umri sahihi kiafya ni upi hasa?
Kwa faida ya wanajamvi.
Kwa kawaida mtoto akizaliwa tu kama hana tatizo lolote la kiafya inashauriwa kumtahiri baada ya Massa 24 hadi siku 60 or 8wks
Faida mojawapo za Kumfanyia tohara mapema ni kama vile;

kidonda kupona haraka (ndani ya siku 7-14)baada ya kufanyiwa

Maumivu yake yatakua kidogo au kw muda mfupi tofauti na mtoto aliye kua

Ni rahisi kumfanyika pia damu inakua kidogo au isiwepo kabisa kulinganisha na mtotot aliekua kwa sababu mishipa ya damu bado haijakomaa na kua mingi .

Mtoto haitaji kushonwa nyuzi yoyote tofauti na aliye fikisha miezi mingi.

Ni rahisi sana kwa mama kumshika na kumuhudumia baada ya procedure

Inaepusha sana magonjwa ya UTI kwa mtoto

Mda mzuri wataalaam wanashauri mpaka mtoto anafikisha miaka miwili ni vizuri zaidi akafanyiwa circumcision.!

Lakini kw ushauri zaidi jaribu kumpeleka mwanao Hosp wao watakueleza vzuri maana bado mtoto yupo kwene umzuri.!

Zipo faida nyingi kupita maelezo
 
mie mwanangu sitamfanyia tohara,labda atajifanyia mwenyewe akikua
 
Kwa hiyo Mkuu unashauri nisubiri akue kwanza?wasiwasi wangu anaweza kudanganywa nikapata amekata dudu yake kama alivyosema jana
Habari yako mkuu, ushauri wangu ni kwamba kumfanyia tohara mapema ni bora zaidi,
Sababu utamwepusha na maambukizi hatokawia kupona na pia siku hizi jambo la maumivu limepungua sana kutokana na ukuaji wa teknolojia ya kitabibu.
 
Kwa maoni yangu.. Usimfanyie mtoto tohara akiwa Mdogo sana.. Maana hizo sehem ndo kwanza zinakuwa.. ! Na kama unavyojua kukata dudu (kama alivyosema dogo) kuna maumivu sana.. ! Kiasi kwamba husababisha kufa kwa cells ambazo ni muhimu kwa ukuaji wa dushe la mtoto, due to high stimulation ya nerves zake... Mwishowe mtoto huwa na kibamia... ![emoji41]
Upo sahihi sana
 
Back
Top Bottom