Ni wakati gani unatakiwa kulipa kodi TRA? Ni kila baada ya miezi mitatu mitatu au kila mwaka?

KRISTIAN P

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2013
Posts
352
Reaction score
57
Jamani naombe msaada wenu kuhusu hili,mimi ni mfanya biashara ndogo ndogo,nina ofisini yangu nimeisajili tra na nina leseni ya biashara,nina huwezo wa kuingiza laki nne hadi sita kwa mwezi je ni kiasi gani inabidi nilipe ushuru tra na je icho kinalipa kwa kila baada ya miezi mitatu mitatu hau kwa mwaka naombeni msaada
 
Kodi? Ipi? Income tax? Paye? Withholding? Provisional? Au import duty?

Fafanua?
 
biashara yako ni sole proprietorship au limited company?
 
Kodi ziko za aina gani kutegemea na muundo wa business yako, jaribu kuwafuata ofisin mwao kitengo cha elimu kwa walipa kodi hawana shida watakupiga shule ya kodi na baadae watakupa vitabu vingi sana vya maswala ya kodi
 
income tax mm ni mfanya biashara ndogo ndogo na ofisini yangu yenye huwe wa kuingiza laki nne hadi sita kwa mwenzi tatizo lina kuja sijui ni procent ngap inabidi niwe natoa ambayo napeleka TRA kwa mfano ni ki ingiza laki nne hau sita ushuru kiasi gan na lipa na je ichi kiwango ni kwa nwaka hau kila baada ya miezi mitatu..asante..
 
sole proprietorship ni ya mtu binafsi..
 
Kama nimekuelewa ulichosema, TRA kwa kawaida huwa wanaugawa mwaka katika robo nne, na wanashauri ulipe ndani ya kila robo ya mwaka. Kwa maana Jan-March ni robo ya kwanza, April-June ni robo ya pili, July-Sept ni robo ya tatu na Oct-Dec robo ya nne na ya mwisho, hivyo unatakiwa kulipa mara nne kwa mwaka na ukichelewa unaweza ukajikuta wanakupiga penalty, walitakiwa wakueleze siku umeenda kufuatilia TIN.
 
Nashukuru kwa msaada wako kaka tazito pale maelezo muda mwingine wana kuwa na dharahau alafu wakali,kingine kwa mfano kwa mwenzi naingiza laki sita na fanya biashara ndogo ndogo na ofisi yangu binafsi bei gan ambayo nitapaswa kuipeleka TRA ya ushuru kila baada ya huo muda uliyo niambia..
 
Sasa na wewe kilichokutuma kwenda kusajiri nini?mbona kama biashara yenyewe ni ndogo sana.maana hata VAT naona kama hujagualify kulipa.
Wewe ungewapiga fix mauzo yako ni chini ya laki tatu kwa mwezi
 
Tatizo biashara nayo fanya na eneo nilipo macho ya watu wengi ndio mana nikasajili kujihamii lisije kunigumia mana binadamu sio wote wanapenda maendeleo ya wengine
 
Sasa na wewe kilichokutuma kwenda kusajiri nini?mbona kama biashara yenyewe ni ndogo sana.maana hata VAT naona kama hujagualify kulipa.
Wewe ungewapiga fix mauzo yako ni chini ya laki tatu kwa mwezi

Msaada/Maelezo zaidi tafadhali:
inamaana mauzo yakiwa chini ya 300k haupo eligible kulipa VAT?
 
Daaah jamaa unataka kulipa kodi circulation ya hela yenyewe ndogo hivyo google hivi vitu tax avoidance and tax evasion
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…