Ni wakati muafaka sasa kwa ACT (Zanzibar) kuachana na Zitto

Ni wakati muafaka sasa kwa ACT (Zanzibar) kuachana na Zitto

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Ukweli ulio wazi ni kuwa Zitto kwa sasa hana mchango wowote kwenye siasa za upinzani za kutaka mageuzi hapa Tanzania, zaidi anachopambania ni maslahi yake binafsi kupitia serikali ya CCM chini ya utawala wa mama Samia. Jambo hilo sio afya kwa mustakabali wa malengo ya ACT hususani kwa upande wa Zanzibar.

Ni kweli Zitto ni muasisi wa ACT na ndio aliwakaribisha wafuasi wa CUF kuhamia ACT na kuifanya ACT kuwa na nguvu upande wa Zanzibar na hapo hapo CUF kufa kifo cha mende kisiasa. Kwa kifupi sana kifo cha CUF zanzibar kimeinufaisha ACT na kifo cha CUF Tanzania bara kimeinufaisha zaidi CHADEMA.

Kama zilivyo siasa za Zanzibar ambapo mipango huweza kubadili kila wakati lakini malengo hayajawahi kubadilika milele, kwa muelekeo huo wa Zitto kutaka kujikomba kwa utawala wa mama Samia, wafuasi wa ACT kwa upande wa Zanzibar wanaweza wasiwe na mwisho mzuri ikiwa wataendelea kupelekeshwa na siasa za Zitto zenye malengo binafsi ya kujipendekeza kwa watawala.

Kwa mfano leo hii Zitto hawezi tena kutamka chochote kuhusu kudai katiba mpya. Mtu wa namna hii ana msaada gani kwa siasa za mageuzi kwa upande wa Zanzibar?

Kupitia bandiko hili ninapenda kuwapa ushauri na angalizo muhimu wafuasi wa ACT kwa upande wa Zanzibar kuanza kuwa makini dhidi ya Zitto na siasa zake. Siasa zake kwa sasa zina mlengo wa kuunga mkono harakati zote za CCM kupitia serikali ya mama Samia, na nyingi katika hizo harakati zina mchango hasi katika siasa za mageuzi kwa aina ya upinzani Zanzibar.

Heri nusu shari kuliko shari kamili.
 
Ukweli ulio wazi ni kuwa Zitto kwa sasa hana mchango wowote kwenye siasa za upinzani za kutaka mageuzi hapa Tanzania, zaidi anachopambania ni maslahi yake binafsi kupitia serikali ya CCM chini ya utawala wa mama Samia. Jambo hilo sio afya kwa mustakabali wa malengo ya ACT hususani kwa upande wa Zanzibar...
UMESEMA NENO LA MAANA
 
CDM wamelala, Zanzibar ni fursa adhimu sana kwao. Waunde CDM Zanzibar yenye autonomy, iwe na maamuzi kwenye mambo mengi kama nominations za wagombea upande wa Zanzibar n.k. iwape wazanzibari ownership.
 
Ukweli ulio wazi ni kuwa Zitto kwa sasa hana mchango wowote kwenye siasa za upinzani za kutaka mageuzi hapa Tanzania, zaidi anachopambania ni maslahi yake binafsi kupitia serikali ya CCM chini ya utawala wa mama Samia. Jambo hilo sio afya kwa mustakabali wa malengo ya ACT hususani kwa upande wa Zanzibar.

Ni kweli Zitto ni muasisi wa ACT na ndio aliwakaribisha wafuasi wa CUF kuhamia ACT na kuifanya ACT kuwa na nguvu upande wa Zanzibar na hapo hapo CUF kufa kifo cha mende kisiasa. Kwa kifupi sana kifo cha CUF zanzibar kimeinufaisha ACT na kifo cha CUF Tanzania bara kimeinufaisha zaidi CHADEMA.

Kama zilivyo siasa za Zanzibar ambapo mipango huweza kubadili kila wakati lakini malengo hayajawahi kubadilika milele, kwa muelekeo huo wa Zitto kutaka kujikomba kwa utawala wa mama Samia, wafuasi wa ACT kwa upande wa Zanzibar wanaweza wasiwe na mwisho mzuri ikiwa wataendelea kupelekeshwa na siasa za Zitto zenye malengo binafsi ya kujipendekeza kwa watawala.

Kwa mfano leo hii Zitto hawezi tena kutamka chochote kuhusu kudai katiba mpya. Mtu wa namna hii ana msaada gani kwa siasa za mageuzi kwa upande wa Zanzibar?

Kupitia bandiko hili ninapenda kuwapa ushauri na angalizo muhimu wafuasi wa ACT kwa upande wa Zanzibar kuanza kuwa makini dhidi ya Zitto na siasa zake. Siasa zake kwa sasa zina mlengo wa kuunga mkono harakati zote za CCM kupitia serikali ya mama Samia, na nyingi katika hizo harakati zina mchango hasi katika siasa za mageuzi kwa aina ya upinzani Zanzibar.

Heri nusu shari kuliko shari kamili.
Chadema walikuwa sahihi sana kumfukuza huyu jamaa maana ana price tag,hana uwezo wowote wa kuongelea mageuzi hasa katiba mpya,mdini sana na mbinafsi.
 
CDM wamelala, Zanzibar ni fursa adhimu sana kwao. Waunde CDM Zanzibar yenye autonomy, iwe na maamuzi kwenye mambo mengi kama nominations za wagombea upande wa Zanzibar n.k. iwape wazanzibari ownership.

cdm wamefail completely kwenye suala la Zanzibar.
 
CDM wamelala, Zanzibar ni fursa adhimu sana kwao. Waunde CDM Zanzibar yenye autonomy, iwe na maamuzi kwenye mambo mengi kama nominations za wagombea upande wa Zanzibar n.k. iwape wazanzibari ownership.
Hii pointi nzuri tatizo ni nature ya politics zetu, mara nyingi inakuwa influenced na eneo (geographically) na aina ya watu wake (dini na kabila).

Kwa nje inaonekana kama jambo rahisi kuingia eneo husika, lakini kwa ndani watu hawajali itikadi au sera ya chama unachopeleka, wao wataangalia kama wewe ni mwenzao, au kama una vinasaba vya kufanana nao? kinyume na hapo hawatakukubali hata kama utaonesha matatizo waliyonayo na utakuwa tayari kuwapigania.

Kama tungeweza kubadili hii mentality naamini siasa zetu zingepiga hatua kubwa sana. Kwa mtazamo wangu sasa hivi Zanzibar hakuna upinzani, inatawaliwa na CCM na upinzani vibaraka wao kama ACT na ADC.

Wale wananchi hasa wapemba hawana wakuwasemea tena, unasubiriwa wakati wa uchaguzi wakadanganywe tena na wanasiasa wapigwe mabomu waumizwe then wanasiasa wakakae mezani na CCM wapewe vyeo at the expense of wahanga wa uchaguzi, waendeshwe kwa v8 maisha yaendelee.

Wasipoamka kwa kuangalia sura za wanasiasa au dini na kabila wataendelea kutumikishwa kwa muda mrefu sana.
 
cdm wamefail completely kwenye suala la Zanzibar.
Zanzibar kuna udini sana,wanataka m/kiti wa taifa awe muislam ndipo wajiunge,aka kanchi tungeachana nako ni chukizo na kujidhalilisha maana tuna ardhi ya kutosha,we are better without Zanzibar
 
Zanzibar kuna udini sana,wanataka m/kiti wa taifa awe muislam ndipo wajiunge,aka kanchi tungeachana nako ni chukizo na kujidhalilisha maana tuna ardhi ya kutosha,we are better without Zanzibar

Haya ndio moja ya matatizo yenu CHADEMA
 
Hii pointi nzuri tatizo ni nature ya politics zetu, mara nyingi inakuwa influenced na eneo (geographically) na aina ya watu wake (dini na kabila).

Kwa nje inaonekana kama jambo rahisi kuingia eneo husika, lakini kwa ndani watu hawajali itikadi au sera ya chama unachopeleka, wao wataangalia kama wewe ni mwenzao, au kama una vinasaba vya kufanana nao? kinyume na hapo hawatakukubali hata kama utaonesha matatizo waliyonayo na utakuwa tayari kuwapigania.

Kama tungeweza kubadili hii mentality naamini siasa zetu zingepiga hatua kubwa sana. Kwa mtazamo wangu sasa hivi Zanzibar hakuna upinzani, inatawaliwa na CCM na upinzani vibaraka wao kama ACT na ADC.

Kama kawaida yenu CHADEMA, kujiona nyinyi pekee ndio wapinzani wa kweli
 
Back
Top Bottom