Ni wakati muafaka watumishi kuvikataa vyama vya wafanyakazi nchini

Ni wakati muafaka watumishi kuvikataa vyama vya wafanyakazi nchini

Black Legend

Senior Member
Joined
Jul 28, 2015
Posts
174
Reaction score
301
Ni muda mrefu sasa watumishi nchini wamekuwa wakinyimwa haki zao ambazo zingine ni za kikatiba kabisa, kwa mfano kupewa nyongeza ya mishahara kila mwaka (annual incriment), upandaji wa vyeo, ulipwaji wa madeni na stahiki zingine, n.k.

Kutokana uwepo wa vyama vya wafanyakazi (trade unions) kama TUCTA, TUGHE, TAU, CWT n.k, watumishi wamekuwa wanakatwa kiasi cha fedha kutoka katika mishahara yao kama michango ya uendeshaji wa vyama hivi.

Katika kipindi cha miaka 10/15 watumishi wamekuwa wakinyimwa haki zao za kiutumishi na pia kupewa ahadi zisizotekelezwa.

Uwepo wa vyama vya wafanyakazi ingekuwa ndiyo kimbilio lakini vyama hivi kwa sasa vimekuwa mzigo na kero kubwa kwa watumishi kutokana na kushindwa kuishi malengo ya matarajio ya kutetea haki za watumishi.

Ni wakati muafaka watumishi waombe kuangalia upya uwepo wa vyama hivi. Kama inawezekana sheria ifute ulazima wa kuwa mwanachama wa vyama hivi.

Mnakaribishwa kwa mjadala.
 
Dr ulimboka wa madokta alimjaribu JK akaokotwa Mabwepande, Mwl Olochi wa CWT alimjaribu anklee mfalme wa Chato akafukuzwa ualimu.

Ni hatari sana kudai masirahi ya wafanyakazi kama wafanyakaz kama bongo wako tayari.
 
TISS ya mejaa humo hasa CWT kwa maslahi ya CCM!
 
Ni muda mrefu sasa watumishi nchini wamekuwa wakinyimwa haki zao ambazo zingine ni za kikatiba kabisaa, kwa mfano kupewa nyongeza ya mishahara kila mwaka(annual incriment), upandaji wa vyeo, , , , ulipwaji wa madeni na stahiki zingine, nk. Kutokana uwepo wa vyama vya wafanyakazi (trade unions) kama TUCTA, TUGHE, TAU, CWT nk, watumishi wamekuwa wanakatwa kiasi cha fedha kutoka katika mishahara yao kama michango ya uendeshaji wa vyama hivi.....Katika kipindi cha miaka 10/15 watumishi wamekuwa wskinyimwa haki zao za kiutumishi na pia kupewa ahadi zisizotekelezwa . Uwepo wa vyama vya wafanyakazi ingekuwa ndio kimbilio lakini vyama hivi kwa sasa vimekuwa MZIGO NA KERO kubwa kwa watumishi kutokana na kushindwa kuishi malengo ya matarajio ya kutetea haki za watumishi. Ni wakati muafaka watumishi waombe kuangalia upya uwepo wa vyama hivi.....kama inawezekana sheria ifute ulazima wa kuwa mwanachama wa vyama hivi. Mnakaribishwa kwa mjadara...
Hii point na iunga mkono 🤝 yaan wale wanaukata asilimia kadha kweny mshahara halaf mbambambaa n nyingi kazi n kukopeshan tu pesa za wanyonge bila hata ya huruma
 
TISS ya mejaa humo hasa CWT kwa maslahi ya CCM!
tiss kwenye ualimu looo!,UK imetoa upendeleo maalum kwa waalimu kutoka Zimbabwe 🇿🇼, South Africa, Nigeria 🇳🇬 na Ghana 🇬🇭 kuajiriwa kwa wingi hapo UK, sisi tuendelee kulalama humu na viajira uchwara
 
Dr ulimboka wa madokta alimjaribu jk akaokotwa mabwepande, mwl olochi wa cwt alimjaribu anklee mfalme wa chato akafukuzwa ualimu.

Ni hatari sana kudai masirahi ya wafanyakaz kama wafanyakaz kama bongo wakotayari.
Lakini mishahara ilipandishwa baada ya matukio yale.
 
Back
Top Bottom