Ni yupi aliyekuwa wakala wa kifo & ulemavu kabla ya kuja kwa bodaboda?

Ni yupi aliyekuwa wakala wa kifo & ulemavu kabla ya kuja kwa bodaboda?

KISIWAGA

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2015
Posts
8,022
Reaction score
16,563
Ni ukweli ulio wazi kuwa kwa sasa bodaboda ndio wanaongoza kwa kuua watu kwenye ajali plus kuwatia vilema

Je, kabla ya ujio wa hawa bodaboda ni akina nani waliokuwa wakishika nafasi ya uwakala wa kifo
 
Kuna mambo basi tu umasikini na labda ubishi na ujinga.

Maana kuna sare za kuendeshea hivyo vyombo kuanzia kofia, glavu, koti, buti, viviko, magoti gadi. Nadhani yangefuatwa hayo yote ingewezekana kupunguza madhara.

Lakini jiulize bodaboda wangapi 'watajipamba' kikamilifu hivyo - Umasikini

Na wateja wangapi watakubali kupambwa hivyo? rejea kipindi kile suala la helmenti za abiria - Ubishi na Ujinga.

Hata hivyo kimsingi hivi vitu vyote vinabebana, kila mtu angemiliki walau ka gari kadogo bodaboda isingekuwa public transport. Kwanza cheki public gani ya wasafiri wawili wawili??

Kujibu swali kako ntasema hakuna kilichobadilika, adui zetu ni walewale wa tangu na tangu UMASIKINI, UJINGA NA MARADHI

Na ili tuendelee, tujikwamue hapo tutahitaji ARDHI, WATU, SIASA SAFI NA UONGOZI BORA. Hakuna mchawi hapo
 
Siasa.Angalia kwa mapana,utaona jinsi watu wanavyoua na kutiwa vilema.
 
Back
Top Bottom