Ni zaidi ya mwaka sasa tukiwa na kodi ya uzalendo

Ni zaidi ya mwaka sasa tukiwa na kodi ya uzalendo

OLS

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2019
Posts
426
Reaction score
685
Nimemaliza kusoma andiko lililochapisha Review of African Political Economy likizungumzia Tanzania's Solidarity Tax, yaani kodi ya uzalendo ambayo ilianzishwa mwaka 2021 robo ya tatu.

Mtafiti katika andiko hilo ameweka sababu nyingi ya kuwa Tanzania haihitaji kuwa na tozo ya uzalendo, zifuatazo ni baadhi ya hoja alizoweka mtafiti.

1. Kodi ya Uzalendo huwa in muda wa kuisha
Kodi ya uzalendo huwa inaenda kwa muda fulani na huondolewa baada ya muda huo kuisha. Kodi hii inaweza kutozwa kwa muda wa mwaka au muda wowote uliokuwa allocated. Suala liko tofauti kwa Tanzania ambayo haijasema kodi hiyo itaisha lini.

2. Kodi hii hutumiwa wakati wa dharura
Nchi zote zilizotumia kodi hii zilifanya hivyo wakati wa dharura. Hata hivyo kwa Tanzania kodi hiyo ilitajwa kwenda kujenga madarasa na zahanati jambo ambalo linaweza kuwa plannned sio dharura. Dharura ingeweza kuwa COVID-19 lakini haiwezekani kwa kuwa wakati ule nchi ilipokea fedha za dharura kutoka IMF

3. Tanzania inapoteza fedha nyingi kwa mifumo hovyo ya kodi
Kila mwaka Tanzania hupoteza zaidi ya trillioni kutokana namifumo mibovu ya kodi, misamaha isiyo na tija na mambo mengine kama hayo. Mtafiti ameshauri kuiimarisha mifumo ya kodi ili kuweza kupata fedha yote ambayo kwa sasa inapotea. Kiuhalisia bado mapato mengi yanapotea ndio sababu ya kuwa na ratio ndogo ya kodi kwa GDP.

Kusoma andiko hilo bofya Tanzania’s solidarity tax
 

Attachments

This is Tanzania.. huenda kodi hiyo muda wake ushaisha ila pesa inatosa kwa manufaa ya mtu
 
Tanzania inapoteza fedha nyingi kwa mifumo hovyo ya kodi
Kila mwaka Tanzania hupoteza zaidi ya trillioni kutokana namifumo mibovu ya kodi, misamaha isiyo na tija na mambo mengine kama hayo. Mtafiti ameshauri kuiimarisha mifumo ya kodi ili kuweza kupata fedha yote ambayo kwa sasa inapotea. Kiuhalisia bado mapato mengi yanapotea ndio sababu ya kuwa na ratio ndogo ya kodi kwa GDP.
 
Watanzania walipofikia sasa, yaani wamewekwa mtu kati
 

Attachments

  • 1671395537605.jpg
    1671395537605.jpg
    39.6 KB · Views: 2
Binafsi nilikosa imani na Mwigulu, tangu siku ya kwanza tu alipoteuliwa kwenye hii Wizara.

Ningekuwa mimi ndiyo Rais, ningempa Wizara ya Muungano na mazingira.
 
Binafsi nilikosa imani na Mwigulu, tangu siku ya kwanza tu alipoteuliwa kwenye hii Wizara.

Ningekuwa mimi ndiyo Rais, ningempa Wizara Muungano na mazingira.
Huyo mtu kupewa Wizara nyeti kama hiyo kwa maendeleo ya Watanzania walichemka sana sana na madhara yake kwa Nchi masikini hawawezi kupiga hesabu ila ni hasara kubwa...
 
Back
Top Bottom