Serendipity
JF-Expert Member
- Jan 24, 2009
- 486
- 43
Zanzibar combined ni sawa na jimbo moja tu la kigamboni lililopo huko Tanganyika! Wazanzibari msiwe wangasem! Kwanza zanzibar sio nchi ni kama wilaya tu.....
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hoja yako ni nyepesi na inaweza kupuuzwa kirahisi tu.
Ukweli ni kuwa hoja yako si rahisi ina mantiki kubwa sana kama wznz wanavyofikiri.
Siku zote nimekuwa nasema kazi ya mznz ni kudai vyeo na madaraka.
Nimesema kuwa hata bunge la katiba wamekuja wakiwa na fomu za ubalozi, ukurugenzi, ukatibu mkuu, uwaziri umakamu na urais.
Hutasikia mznz hata mmoja akiongelea gharama na kama yupo basi ujue ni mwendawazimu.
Mznz mwenye akili timamu haongelei gharama kwasababu ni wajibu wa Mtanganyika.
Ndivyo iunavyoonekana katika hoja yako unapotaka spika au mwenyekiti achaguliwe kutoka znz wakati wajumbe wote wanalipwa posho bila SMZ uweka hata senti tano.
Ungeuliza gharama zinalipwa na nani halafu ndipo suala la nchi huru sawa lije.
Kama znz hawataki gharama maana yake hawataki usawa!
Hakuna usawa usio na wajibu isipokuwa kwa wapuuzi tu.
Fikra za mznz ni nafasi za ubalozi na vyeo baasi, anajua huduma za vitu hivyo huteremeka wakati wa mvua za masika.
JokaKuu GHIBUU takashi Nonda Mchambuzi Bongolander Bobwe
Bunge la Katiba sio sawa na Kijiwe cha Ghahawa pale Kibanda-Maiti au sio sawa na mkusanyiko wa kuchukua Tende,Haluwa au Urojo pale Mwanakwerekwe,bali Bunge la Katiba linahitaji Mtu mweledi,busara,msimamo,mkomavu,mstahmilivu,mstaarabu,hekima na anaejua nini cha kufanya kwa muda na wakati muafaka,na watu wa pande hizo mnakosa hizi sifa.
Unazungumzia bunge la katiba au la bunge la muungano? Katiba inasemaje, kuna zamu za kutoa spika? Huko Zanzibar, Mtanganyika gani amewahi kuwa spika? Acha upuuzi
Huyu jama kanywa UROJO mpaka KAVIMBIWA KALEWA..... SPIKA atoke ZAA NZI BALAA? huu sasa ni wendawaziu mkubwa sana. tuachen masikhara katika mambo ya maana zile mada za kwenye vijiwe pale MCHAMBA WIMA au MWANAKWEREKWE tuachaneni nazo, turudi kujadili mambo ya maana sasa. aaalaaahhh.
Zanzibar combined ni sawa na jimbo moja tu la kigamboni lililopo huko Tanganyika! Wazanzibari msiwe wangasem! Kwanza zanzibar sio nchi ni kama wilaya tu.....
wazanzibar tusionewe ,tanzania ni muungano wa nchi mbili zilzokuwa huru.wote wana haki sawa.
na watanganyika tunaonewa pia, iweje tangu muungano hajawahi kutokea mtanganyika kushika wadhifa wowote katika serikali ya mapinduzi ya zanzibar? lakini tanganyika yetu ndiyo imekuwa shamba la bibi kwa wapemba na wa unguja kuanzia na mwinyi, sheni, jumbe na bilali serikali tatu ndiyo suluhisho!
siongelei nafasi za zanzibar au tanganyika naongelea zile za tanzania.katiba ni ya tanzania na bunge ni la tanzania sio tanganyika .kama mnataka kama sisi anzisheni serikali yenu kwani mmekatazwa?
Basi atapewa mama ako muuza gongo au bibi yako ngariba ngawa we . Mijitu ambayo ina mama mmoja lakin baba 25 utaijua tu. Iv we punda umeshawah kumuliza mama ako kwanini huna baba?
kwa kuwa tangu uhuru hajawahi tokea spika wa bunge la muungano kuwa mzanzibar.sasa ni wakati muafaka kwa zanzibar kupewa kit hicho bunge la katiba,
katungwe kautaratibu katakako hakikisha wajumbe wote wanaochuana kwa nafasi hiyo wawe wazanzibar.
Mkuu Joka Kuu, muungano wetu ni kama ndoa, kuna mume na mke, jukumu la kutunza familia ni la mume ambaye ndie father figure na kichwa cha nyumba!. Mume ndie hugharimia kila kitu kikuu cha uendeshaji wa nyumba!. Hata kama mume amemfungulia biashara mkewe, hivyo mkewe nae ana kipato, bado jukumu la kugharimia uendeshaji wa nyumba ni la mume, fedha za biashara za mke, hutumika kusaidia mahitaji madogo madogo ya mkewe kama hina, wanja, ubani, na nguo za ndani!, huku mume akimtimizia mahitaji mengine yote as a responsibility!.