Ni zip Tofauti kati ya VRN na TIN,je kunafaida gani ya kuwa na VRN?

Ruhazwe JR

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2011
Posts
3,402
Reaction score
925
Wasalamu,
hizi ni terminology za TRA.nafahahamu TIN lakin VRN sifahamu wala sijui faida za kuwa nayo wala hasara za kutokua nayo.naomba kupewa shule jaman!
 
VRN-VAT Registration Number,
Hii anakua nayo yule alieandikishwa kulipa VAT tu, jua kua sio kila business person analipa VAT.

TIN-Taxpayer Identification Number.
Hii anakua nayo mlipakodi yoyote hata kama halipi VAT. Sasa basi hata yule pale juu kwakua VAT ni kodi so anatakiwa pia kua na hii.

Note;
Kwenye neno yoyote hapo juu, naomba mfanyakazi usimuweke ingawa analipa kodi.
Kwanini? SIJUI!!!!
 
VAT nakumbuka inachajiwa kwa wafanyabiashara wenye mapato/mtaji ya zaidi ya mil20(Civics ya form One) kama sijakosea(mwanzo walikua wanatoza 20% now ni 18%)
 
VAT nakumbuka inachajiwa kwa wafanyabiashara wenye mapato/mtaji ya zaidi ya mil20(Civics ya form One) kama sijakosea(mwanzo walikua wanatoza 20% now ni 18%)

Mapato yanayozidi 40,000,000 kwa mwaka.......VAT 18%
 
Shark kwa hiyo,kama unanzisha kampuni yako si lazima uwe nayo na hasa kama mapato yako ni chini?na kama ukiwanayo nini faida za kuwa nayo
 
Last edited by a moderator:
Wasalamu,
hizi ni terminology za TRA.nafahahamu TIN lakin VRN sifahamu wala sijui faida za kuwa nayo wala hasara za kutokua nayo.naomba kupewa shule jaman!

TIN - hii ni muhimu kwa kila mlipa kodi kwa kuwa ni reference number yako kwa TRA. Hata ukitafuta leseni/au ku-import gari unapaswa kuwa na TIN ili kodi unayolipa iwe na reference. hii kila mlipa kodi anayo na pia hutolewa bure na TRA.

VRN ni kwa walipakodi wanaojihusisha na biashara inayohusisha kodi ya VAT. Ikiwa unafanya biashara yenye kodi ya VAT unapata/tarajia kupata mapato ya tzs 40m kwa mwaka au zaidi unapaswa kujisajili na VAT ili upate VAT regustration number.

Faida:


  • Ukiwa kama mfanyabiasha unayejihusisha na biashara yenye uwepo wa kodi ya VAT, basi ni muhimu kwa kuwa utakuwa unatii sheria hivyo kupeuka faini na matatizo na idara husika;


  • Unapokuwa na VRN unaweza ku-claim VAT ulizolipa katika manunuzi yako na hivyo hiyo VAT kuwa sio gharama yako bali ya mtumiaji wa mwisho;


  • Kama biashara yako inahusisha kampuni kubwa, kampuni hizi hupendelea kushiriki biashara na watu wenye VRN kwakuwa wataweza kurejesha kiasi cha VAT walichotozwa kwenye hawala zao na pia wanatii sheria kwa kujishughulisha na mtu ambae ni mtii sheria pia; na
  • Unasaidia nchi kukusanya kodi na kuwapa kwa VAT unazotoza katika biashara yako.

Hasara/Challenges:


  • Gharama kubwa za kuweka rekodi zako za kibiashara katika mfumo unaokubalika na TRA ikiwa ni pamoja na kuwa na accounting department etc (compliance burden); na
  • Gharama za kuandaa na kupeleka ripoti za VAT kila mwezi katika TRA na kulipa VAT ulizokusanya.

NB: Ikiwa umetimiza vigezo vya kuwa na VRN inapswa kuipata maramoja, kinyume na hapo ni kosa kisheria linalopelekea faini.
 
wehoodie tunashukuru sana kwa kuja na maelezf mazur ya kina,natumai mleta mada atakua amepata majibu,labd nikuulize swali la nyongeza,mfano nimesajil kikampuni changu cha kazi mchanganyiko kulingana na memart itakavyokua inaeleza na nina TIN tayari naanza na kabiashara kamtaji wa ml3 kastationary ka kawaida,Lakini marengo yangu ni kupanua mtaji,na kuweza kuwekeza ktk majumba,mahotel na ukandarasi,je ni lin ntajitambua kuwa kwa sasa nimekua natakiwa kujisajir na VRN?nauliza hivyo kwakua naweza kuwa na mtaji Umekuwa had ml20 naenda kuomba tenda za mli 50 au 30 Je nili ntatakiwa kujijua kua nimequlify kwa na VRN?Je nikisajilir VRN wakati mtaji wangu ni ml3 Kuna tatizo?
 
Last edited by a moderator:

Mkuu Ruhazwe, unatakiwa kujisajili pale ambapo umepata aua unatarajia kupata pato (sales/revenue/turnover) ya TZS 4Om kwa kipindi cha miezi 12 mfulullizo (mwaka 1) au tzs 10 kwa kipindi cha miezi mitatu. Hivyo pale ambapo umepata hiyo tenda ambayo unajua malipo yake yanazidi hizo benchmark unatakiwa katika kipindi cha siku 30 ujiandikishe na VRN.

VRN inaangalia mapato na sio mtaji, sijui kama kuna uhusiano wa karibu kati ya pato na mtaji.
 
Mkuu wehoodie nimekupata vilivyo.ahsante sana kwa sasa sina swali
 
Last edited by a moderator:
Shark kwa hiyo,kama unanzisha kampuni yako si lazima uwe nayo na hasa kama mapato yako ni chini?na kama ukiwanayo nini faida za kuwa nayo

Wazungumzia ipi sasa Madabhali Jnr ??
TIN ni lazima uwe nayo so long as unafanya biashara.

But VRN ni kama mauzo yako (sio faida) yanafikia 40Million kwa mwaka, au kuna miezi mitatu ambayo hua yanafikiaga 10Million.
 
Habari wapendwa.

Ni mahitaji gani yanahitajika ili kuweza kujisajili na VRN ukiachilia la kufikisha mapato zaidi ya million 50 kwa miezi sita au million 100 kwa mwaka?
 
TIN ni Taxpayer Identification Number. Hii ni namba maalum ya mlipa kodi ambayo anasajiliwa kwa muktadha wa iwapo analipa kodi basi ndiyo inakuwa namba yake maalum ya uwasilishaji wa kodi.

VRN ni VAT Registration number. VAT ni kodi ya ongezeko la thamani ambayo mlaji anayotozwa na mfanyabiashara aliesajiliwa kwa mujibu wa sheria (VAT Act 2104) kwenye mauzo ya bidhaa na huduma zinazostahili kutozwa VAT. Namba maalum iliyosajiliwa kwa ajili ya kutoza na kuwasilisha hii kodi ya ongezekonla thamani ndiyo VRN.

Wanaostahili kusajili VAT kwa mujibu wa sheria ya ongezeko la kodi ya thamani ni pamoja na:-
1. Biashara yenye mauzo ya au yanayozidi mil 100 kwa mwaka

2. Watoaji huduma za kitaalam wanatakiwa kusajili VAT pasina kujali mauzo yao madogo au makubwa kiasi gani. Hii ina maana biashara yyt ya kitaalam km engineering, consultant, lawyer, wahasibu et al ni lazima kusajili VAT

3. Serikali na taasisi zake zinazofanya shughuli za kiuchumi za kujipatia kipato nje ya kazi zao za msingi hutakiwa kusajili

Nitasajili vipi VAT
1. Kuwa na namba ya utambulisho wa mlipakodi (TIN)
2. Kuwa na kiwango cha mauzo yanayostahili kutozwa VAT kwa mwaka kwa biashara
3. Kujaza fomu za maombi ya kusajiliwa kwa mujibu wa maelekezo

Faida za kusajiliwa VAT
1. Kuchangia pato la Taifa
2. Kiasi cha VAT kinachodaiwa na mfanyabiashara kinaweza kufidiwa na VAT kwa miezi inayofuata au mfanyabiashara ataomba kurejeshewa kwa kuzingatia marejesho ya kodi (Endapo VAT kwenye manunuzi ni kubwa kuliko kwenye mauzo)

(Sheria ya KODI YA VAT nimeambatanisha hapo chini waweza soma zaidi)

NawasilishaView attachment THE VALUE ADDED TAX ACT, 2014.pdf
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…