Kama uko dar nenda Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto kitengo cha usajili wa NGO watakuelekeza. Kama upo mkoani kwa ufupi unatakiwa upitishe maombi yako kwenye halmashauri ya wilaya then mkoani. Baada ya hapo unaandika barua ya maombi ukiambatanisha na Katiba (nakala 3), majina ya waanzilishi na sahihi zao, muhtasari wa kikao cha kupitisha katiba, cv za watu watatu na passport size 2(Mwenyekiti, Katibu na Mtunza Hazina) pamoja na Form Na 1 iliyojazwa na kuwekwa stamp duty. Then utalipia usajii kutokana na ukubwa wa eneo inalohudumia NGO yako.