Nichukue PCM au PCB, naomba ushauri wako

Nichukue PCM au PCB, naomba ushauri wako

Nimemaliza kidato cha nne hapo mwaka jana.
Ninapenda sana kuchukua PCM, But kwa uelewa wangu mdogo na maoni ya baadhi ya watu inasemekana kwamba PCM Haina ajira serikalini unless kwenye makampuni binafsi (ambako kuna nepotism)... Kama kuna ajira zaidi ya hizo nijulishe tafadhali.
HILI LINANIKATISHA TAMAA SANA NA KUNIFANYA NIHISI KWAMBA NIKISOMA PCM SIPATI AJIRA TOFAUTI NA UALIMU.
Kwa upande wa PCB, INASEMEKANA kuwa kuna ajira za moja kwa moja serikalini ama kwa kujiajili mwenyewe. Na mimi ninasoma ili nipate ajira niweze kujitegemea.
MAONI YAKO NDIYO YATAKAYONIFANYA NIWE NA MAAMUZI MAZURI.
Natanguliza shukrani zangu kwa mtakao nishauri...
Karibuni kwa ushauri....

Ajira zenyewe za serikalini unazodhani utapata ni za kisenge. Soma kozi unayoipenda na kuiweza. As long as unaiweza na utafaulu vizuri, ajira au kujiajiri kutakuja baadae.
Mi binafsi ni engineer. Nlichagua njia hii tangu form one. Advance nilichaguliwa kusoma PCB, nikakomaa kubadilisha kwenda PCM ingawa watu walinipa porojo kama hizo unazoambiwa kuhusu ajira. Nimeajiriwa na natengeneza millions (za kitanzania), na nina mpango wa kuachana na ajira na kuanza kufanya mambo yangu binafsi.
 
Kijana kwanza
angalia nini plan yako kwanza ikimaanisha unataka kozi gani baadae ili
usije kujiroga mwenyewe. Kisha angalia masomo gani unayamudu ili baadae
usije kujutia kwanini uliacha somo fulani. Kisha utaamua mwenyewe nini
ufanye baada ya kuangalia vigezo hivi.

ahsante..
 
Ajira zenyewe za serikalini
unazodhani utapata ni za kisenge. Soma kozi unayoipenda na kuiweza. As
long as unaiweza na utafaulu vizuri, ajira au kujiajiri kutakuja baadae.

Mi binafsi ni engineer. Nlichagua njia hii tangu form one. Advance
nilichaguliwa kusoma PCB, nikakomaa kubadilisha kwenda PCM ingawa watu
walinipa porojo kama hizo unazoambiwa kuhusu ajira. Nimeajiriwa na
natengeneza millions (za kitanzania), na nina mpango wa kuachana na
ajira na kuanza kufanya mambo yangu binafsi.

big up...!
 
Kijana kwanza angalia nini plan yako kwanza ikimaanisha unataka kozi gani baadae ili usije kujiroga mwenyewe. Kisha angalia masomo gani unayamudu ili baadae usije kujutia kwanini uliacha somo fulani. Kisha utaamua mwenyewe nini ufanye baada ya kuangalia vigezo hivi.

ahsante..!
 
Narudia tena pcb & pcm hizo kombi ukienda shule zaidi ya mzumbe,kibaha,taboraboys &ilboru lazma ufeli
 
mi wakat nachukua PGM wengi waliniponda et nitafeli au nitakosa kaz lkn now wote walioniponda ndo ninao wasaidia kwa sasa, kikubwa soma kwa malengo na wala c kwa kupata et kz kwa urahc kama future yako ipo kwenye pcm xoma iyo na kama ipo kwenye pcb xoma hiyo!!!
 
Narudia tena pcb & pcm hizo kombi ukienda shule zaidi ya mzumbe,kibaha,taboraboys &ilboru lazma ufeli


Kukariri kubaya sana.

Mbona darasa la MD la Muhimbili kuna wanafunzi kutoka zaidi ya hizo shule?

Acha unanga mkuu
 
Ndiyo maana tuna wasomi lakini hakuna output yoyote kwenye taaluma zao.

What's your dream young man??

Soma hata HKL kama ndiyo itakufikisha kwenye ndoto zako..otherwise utakuwa doctor lakini not self motivated koz ulisoma tu upate ajira kirahisi upate pesa not what u really wanted to do!

Think again why you want to study either of those!!!!
Mentor...
U r really a mentor.. Well said...
 
Last edited by a moderator:
aisee soma unachokiweza usifuate upepo,,, soma upite hapo suala la kazi ni mbele kwa mbele,,,, kuna jamaa zangu nilisoma nao na katika material yao ya kimasomo walikua wanaandika kazi zao za baadae(dr, eng) mwisho wa siku hawakufanya vizuri na wanachukua taaluma nyingine
 
Chukua PCK...ndio nzuri mkuu...


Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Kwa ushauri wangu,kama combinations zote unaziweza na kwa kuwa kilio chako ni kuajiriwa, go for PCB kwa sababu iwapo UTAFAULU VIZURI,utasoma kozi za afya ambazo ajira ni constant

This is according to your need

Kwa upande mwingine,kama ukiajiriwa kufanya kazi usioipenda,believe me hutokaa upate amani
 
unachosema kweli kabisa. kazi bila amani ni sawa na mkulima alieuza shamba akanunua mbegu .mtu unapoteza muda kuja kutumikia kitu ambacho kitakutesa ni mbaya sana
 
PCB hutajutia,kwanza ukisoma udaktari una uhakika wa gov sponsorship,pili ajira miaka 3 serikalini, PCM utasugua sana mtaani
 
Usiende kama bendera kaa ufikirie uwezo wako kama unahsi uko vzur in bios n u can handle stress kasome pcb
 
Back
Top Bottom