NIDA: Wenye Vitambulisho vilivyochapishwa chini ya Kiwango wavirejeshe

NIDA: Wenye Vitambulisho vilivyochapishwa chini ya Kiwango wavirejeshe

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida) imeanza kuchapa upya vitambulisho vilivyochapishwa chini ya kiwango, hivyo imewataka wenye navyo kuviwasilisha katika ofisi zake zilizo karibu nao vichapwe upya.

Hayo yamesemwa leo Alhamisi Julai 4, 2024 na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Nida, Geofrey Tengeneza alipozungumza na Mwananchi.

Amesema hatua hiyo imetokana na malalamiko kutoka kwa wananchi wa mikoa mbalimbali kuhusu ubora hafifu wa baadhi ya vitambulisho hivyo.

"Tumekuwa tukipokea malalamiko kutoka kwa baadhi ya wananchi wa mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Morogoro Dar es Salaam na mingine, kuwa vitambulisho walivyopewa vimefutika picha na majina," amesema.

Baada ya kufanya utafiti na kubaini ukweli juu ya changamoto hiyo na Nida imeamua kuvikusanya kutoka kwa wananchi ili kuvichapisha upya.

"Napenda kuchukua nafasi hii kuujulisha umma wa Watanzania kwamba yoyote mwenye kitambulisho kilichofutika picha na maandishi akirejeshe kwenye ofisi za kata yake, au ofisi za Nida zilizopo karibu naye ili achapiwe kipya ndani ya muda mfupi," amesema.

MWANANCHI

Pia Soma:NIDA: Ruksa kubadili Vitambulisho vilivyoisha muda au vyenye ukomo kwa Tsh. 20,000
 
Mimi sina hamu na NIDA! Nilipoteza kitambulisho nikafuata taratibu zote kama walivyonielekeza ikiwemo na kulipa sh.20 elfu wakaniambia subiri kitambulisho tu.
Niliporudi sasa kuja kupata kitambulisho nikaambiwa sijalipia sh.20 elfu walipotafuta vizuri wakaiona stakabadhi.
Kwa kweli nilikata tamaa kabisa nilipoambiwa subiri tena!
 
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida) imeanza kuchapa upya vitambulisho vilivyochapishwa chini ya kiwango, hivyo imewataka wenye navyo kuviwasilisha katika ofisi zake zilizo karibu nao vichapwe upya.

Hayo yamesemwa leo Alhamisi Julai 4, 2024 na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Nida, Geofrey Tengeneza alipozungumza na Mwananchi.

Amesema hatua hiyo imetokana na malalamiko kutoka kwa wananchi wa mikoa mbalimbali kuhusu ubora hafifu wa baadhi ya vitambulisho hivyo.

"Tumekuwa tukipokea malalamiko kutoka kwa baadhi ya wananchi wa mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Morogoro Dar es Salaam na mingine, kuwa vitambulisho walivyopewa vimefutika picha na majina," amesema.

Baada ya kufanya utafiti na kubaini ukweli juu ya changamoto hiyo na Nida imeamua kuvikusanya kutoka kwa wananchi ili kuvichapisha upya.

"Napenda kuchukua nafasi hii kuujulisha umma wa Watanzania kwamba yoyote mwenye kitambulisho kilichofutika picha na maandishi akirejeshe kwenye ofisi za kata yake, au ofisi za Nida zilizopo karibu naye ili achapiwe kipya ndani ya muda mfupi," amesema.

MWANANCHI

Pia Soma:NIDA: Ruksa kubadili Vitambulisho vilivyoisha muda au vyenye ukomo kwa Tsh. 20,000
Wahangaike na sisi ambao hatujapata kabisa, since 2017 kweli?
 
Nida na serikali yake haipo serious na hivi vitambulisho
 
Wanakosea majina yetu makusudi ili tukienda kuhariri taarifa zetu watupige hela vizuri,kwenye R anaandika L, kwenye M anaandika N,yaani shida tupu
 
Back
Top Bottom