Nifah: Rasmi, Mimi & The Bold tumeachana

Nifah: Rasmi, Mimi & The Bold tumeachana

View attachment 2858656

Mapenzi kama yalivyo mambo mengine yana mwanzo na mwisho pia. Ni wachache waliobarikiwa na wenye bahati katika mapenzi huishia pamoja kwa kudumu milele hadi kifo kuwatenganisha, Huku wengi wakiishia njiani na hakuna ubaya katika hilo. Ndio maisha na mapenzi…. Ni safari isiyotabirika.

Miaka kadhaa iliyopita nilipata kuingia katika mapenzi yaliyofahamika na wengi hapa jamvini.
Hivyo basi, kwa kuwa mapenzi yale hayapo tena, imeniwia vyema kurudi tena hapa kuweka hilo wazi.

Tulikuwa na malengo ya kufika mbali, lakini kutokana na kutofautiana katika mambo mengi tulishindwa hata kufikia hatua za kuyarasimisha mahusiano yetu kuwa halali.

Tulitengana rasmi mwezi August mwaka huu 2023, na kutokana na hilo pengine huenda yakawa ndio mahusiano yangu ya mwisho kuyaweka wazi.

Mapenzi ya wazi hapa yamenipa wakati mgumu kujibu mamia ya wanachama waliokuwa wakihoji endapo bado tupo pamoja, na ndio sababu kuu naweka uzi huu kuwafahamisha wote kwa pamoja, hatupo tena katika mahusiano.

Tumeachana kwa amani, na kwa dhati kabisa namtakia kheri katika maisha mapya bila ya uwepo wangu kwa aliyekuwa mwenzangu.

Nifah

Duuuh haya wakuu hongereni
 
Nasema uongo [emoji1783][emoji1783]??? Uzuri weee wamuda humuu hahahaha... tangu enzi hizo watu tunabambaa Humu hahaha..
Yaaani, nakumbuka zile bato humu za zamani

Kikubwa ukisha opoa Jimbo jf unalihamisha kwenda uraiani. Utaishi Kwa Amani sana.

Ila kwakweli nimefadhaishwa na huu Uzi. Ila ni muhimu kuheshimu mawazo ya watu.

All the best Nifah
 
Yaaani, nakumbuka zile bato humu za zamani

Kikubwa ukisha opoa Jimbo jf unalihamisha kwenda uraiani. Utaishi Kwa Amani sana.

Ila kwakweli nimefadhaishwa na huu Uzi. Ila ni muhimu kuheshimu mawazo ya watu.

All the best Nifah
Kweli bato zilianza muda humu kitambo sana watu wanapigwa vita
.Nimependa hapo pa kuhamishia uraiani.
Msalimie sana Mama P
 
Back
Top Bottom