Nifanyeje ili niwaamini tena TBS, TFDA na wathibiti ubora wengine maana kila nikijaribu kuwaamini inashindikana

Nifanyeje ili niwaamini tena TBS, TFDA na wathibiti ubora wengine maana kila nikijaribu kuwaamini inashindikana

dmkali

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2014
Posts
11,793
Reaction score
22,552
Naombeni ushauri namna ya kuongeza imani yangu kwa haya mashirika wadhibiti ubora!

Yamkini wanafanya kazi nzuri sana lakini imani yangu kwao ilishakufa kabisa!
Yaani ni mara mia uniambie hiki kitu ni bora kwa reference zingine tofauti na haya mashirika ya ubora tz!.

Kila nikiona nembo ya udhibitisho wa TBS, au TFDA Huwa nakosa amanj kabisa yaani!

Hata nikitumia bidhaa tajwa basi huwa natumia kwasababu hakuna mbadala wake lakini siyo kwa imani kwamba bidhaa hiyo ni bora!

Chanzo cha kukosa imani kwa TBS na washirika wake wengine wa viwango Tanzania!
  • Ni vile ninashuhudia bidhaa lukuki kama nondo,flat bar, pipes n.k huko madukani hazijafikia viwango stahiki na zinauzwa ( mfano standard ya nondo futi 40 lakini utakuta madukani zimejaa futi 37 tu)
  • Waya za umeme ukisoma size mm then ukaamua kupima unaona kuna upungufu wa 0.5mm~1 mm na zipo madukani na zina nembo ya tbs
  • Vyakula na vinywaji vingi vinaleta kansa lakini vimebandikwa nembo ya TBS kwa kipimo kipi.
  • Unga wa mahindi na vyakula kibao vingine/ vinywaji vinaandaliwa too local na kusambazwa na vina nembo ya TBS
Kwa mambo haya machache kama hayo napata wapi imani ya kuwaamini tbs jamani?

Juzi kati kuna poda ya watoto ya Jonson Jonson nayo tumeambiwa ina madhara!

Na ina nembo ya TBS! je ilibandikwaje nendo hadi bidhaa imeingia kwa walaji?

Kwanini uchunguzi wa TBS huwa unakuja baada ya kungundulika bidhaa ina mapungufu?

Kuna bidhaa ngapi hatari zimo inchini kwa style hii ya TBS?

Huenda wanafanya kazi vizuri lakini naona kabisa hawana tofauti na stika ya enenda kwa usalama barabarani !
Mwenye pesa anabandika hata kama gari bovu!
Je TBS inazingatia ubora kwa kiasi gani au almradi stika tu!
 
Asante kwa taarifa. Zitafanyiwa kazi
 
Kiukweli kwa upande wa viwanda vya ndani vinavyozalisha na kufungasha bidhaa ya chakula ni kama imekosa msimamizi kabisa. Hawa TBS ni kama wamezidiwa,, eti mtu unaomba usajili mtandaoni na unapewa usajili bila hata ya kujua hali ya jengo na vigezo lukuki vinavyotakiwa ili kuzalisha na kufungasha chakula kilicho salama
 
TFDA haipo sasa, kuna TMDA....ambao wanadhibiti Dawa, vifaa tiba na diagnostics.....hawapo tena kwenye udhibiti wa Chakula wala vipodozi.....hivyo vyote vipo TBS......
 
TFDA haipo sasa, kuna TMDA....ambao wanadhibiti Dawa, vifaa tiba na diagnostics.....hawapo tena kwenye udhibiti wa Chakula wala vipodozi.....hivyo vyote vipo TBS......
Ni Majina tu lakin watu ni walewale
 
Kiukweli kwa upande wa viwanda vya ndani vinavyozalisha na kufungasha bidhaa ya chakula ni kama imekosa msimamizi kabisa. Hawa TBS ni kama wamezidiwa,, eti mtu unaomba usajili mtandaoni na unapewa usajili bila hata ya kujua hali ya jengo na vigezo lukuki vinavyotakiwa ili kuzalisha na kufungasha chakula kilicho salama
Uozo mtupu
 
Kiukweli kwa upande wa viwanda vya ndani vinavyozalisha na kufungasha bidhaa ya chakula ni kama imekosa msimamizi kabisa. Hawa TBS ni kama wamezidiwa,, eti mtu unaomba usajili mtandaoni na unapewa usajili bila hata ya kujua hali ya jengo na vigezo lukuki vinavyotakiwa ili kuzalisha na kufungasha chakula kilicho salama
 
Naombeni ushauri namna ya kuongeza imani yangu kwa haya mashirika wadhibiti ubora!

Yamkini wanafanya kazi nzuri sana lakini imani yangu kwao ilishakufa kabisa!
Yaani ni mara mia uniambie hiki kitu ni bora kwa reference zingine tofauti na haya mashirika ya ubora tz!.

Kila nikiona nembo ya udhibitisho wa TBS, au TFDA Huwa nakosa amanj kabisa yaani!

Hata nikitumia bidhaa tajwa basi huwa natumia kwasababu hakuna mbadala wake lakini siyo kwa imani kwamba bidhaa hiyo ni bora!

Chanzo cha kukosa imani kwa TBS na washirika wake wengine wa viwango Tanzania!
  • Ni vile ninashuhudia bidhaa lukuki kama nondo,flat bar, pipes n.k huko madukani hazijafikia viwango stahiki na zinauzwa ( mfano standard ya nondo futi 40 lakini utakuta madukani zimejaa futi 37 tu)
  • Waya za umeme ukisoma size mm then ukaamua kupima unaona kuna upungufu wa 0.5mm~1 mm na zipo madukani na zina nembo ya tbs
  • Vyakula na vinywaji vingi vinaleta kansa lakini vimebandikwa nembo ya TBS kwa kipimo kipi.
  • Unga wa mahindi na vyakula kibao vingine/ vinywaji vinaandaliwa too local na kusambazwa na vina nembo ya TBS
Kwa mambo haya machache kama hayo napata wapi imani ya kuwaamini tbs jamani?

Juzi kati kuna poda ya watoto ya Jonson Jonson nayo tumeambiwa ina madhara!

Na ina nembo ya TBS! je ilibandikwaje nendo hadi bidhaa imeingia kwa walaji?

Kwanini uchunguzi wa TBS huwa unakuja baada ya kungundulika bidhaa ina mapungufu?

Kuna bidhaa ngapi hatari zimo inchini kwa style hii ya TBS?

Huenda wanafanya kazi vizuri lakini naona kabisa hawana tofauti na stika ya enenda kwa usalama barabarani !
Mwenye pesa anabandika hata kama gari bovu!
Je TBS inazingatia ubora kwa kiasi gani au almradi stika tu!

Unacho eleza ni kweli kabisa,hizi taasisi hazifanyi kazi zao ipasavyo,siasa ndio imetawala….na hili ka vyakula litatufanya watanzania wengi tuwe na magonjwa ua ajabu ajabu….wewe angalia asali zinazo uzwa madukani nilizonzalishwa hapa nchini yaani hata hazieleweki zimechanganywa na nn,hatari sana.
 
Kama huwaamini na maisha yanaendelea, hiyo ni tahadhari bora kabisa. Usihangaike na kutaka kuwaamini, uko upande salama.
 
Unacho eleza ni kweli kabisa,hizi taasisi hazifanyi kazi zao ipasavyo,siasa ndio imetawala….na hili ka vyakula litatufanya watanzania wengi tuwe na magonjwa ua ajabu ajabu….wewe angalia asali zinazo uzwa madukani nilizonzalishwa hapa nchini yaani hata hazieleweki zimechanganywa na nn,hatari sana.
Yaani kila sehem sumu tupu na hawajali
 
Ndo maana huwa nasema watu wasile ugali maana mashine nyingi sio wasafi
 
Ndo maana huwa nasema watu wasile ugali maana mashine nyingi sio wasafi
Hahah wale mihogo! Sema waaandae mahidi wenyewe kwa usahihi na usafi wakasagishe
 
Naombeni ushauri namna ya kuongeza imani yangu kwa haya mashirika wadhibiti ubora!

Yamkini wanafanya kazi nzuri sana lakini imani yangu kwao ilishakufa kabisa!
Yaani ni mara mia uniambie hiki kitu ni bora kwa reference zingine tofauti na haya mashirika ya ubora tz!.

Kila nikiona nembo ya udhibitisho wa TBS, au TFDA Huwa nakosa amanj kabisa yaani!

Hata nikitumia bidhaa tajwa basi huwa natumia kwasababu hakuna mbadala wake lakini siyo kwa imani kwamba bidhaa hiyo ni bora!

Chanzo cha kukosa imani kwa TBS na washirika wake wengine wa viwango Tanzania!
  • Ni vile ninashuhudia bidhaa lukuki kama nondo,flat bar, pipes n.k huko madukani hazijafikia viwango stahiki na zinauzwa ( mfano standard ya nondo futi 40 lakini utakuta madukani zimejaa futi 37 tu)
  • Waya za umeme ukisoma size mm then ukaamua kupima unaona kuna upungufu wa 0.5mm~1 mm na zipo madukani na zina nembo ya tbs
  • Vyakula na vinywaji vingi vinaleta kansa lakini vimebandikwa nembo ya TBS kwa kipimo kipi.
  • Unga wa mahindi na vyakula kibao vingine/ vinywaji vinaandaliwa too local na kusambazwa na vina nembo ya TBS
Kwa mambo haya machache kama hayo napata wapi imani ya kuwaamini tbs jamani?

Juzi kati kuna poda ya watoto ya Jonson Jonson nayo tumeambiwa ina madhara!

Na ina nembo ya TBS! je ilibandikwaje nendo hadi bidhaa imeingia kwa walaji?

Kwanini uchunguzi wa TBS huwa unakuja baada ya kungundulika bidhaa ina mapungufu?

Kuna bidhaa ngapi hatari zimo inchini kwa style hii ya TBS?

Huenda wanafanya kazi vizuri lakini naona kabisa hawana tofauti na stika ya enenda kwa usalama barabarani !
Mwenye pesa anabandika hata kama gari bovu!
Je TBS inazingatia ubora kwa kiasi gani au almradi stika tu!
Hizo mashine za kupimia ubora zimetengenezwa na muuza bidhaa unazotaka kubaini ubora wake.
Wewe kula tu, mengine tutajua huko mbeleni
 
Nikitizama kanzi data yangu hapa, sioni shirika likiitwa TFDA hapa nchini.
 
Back
Top Bottom