Nifanyeje ili niweze kupata pesa ya kuanzishia biashara?

nyahinga

Member
Joined
Dec 18, 2016
Posts
45
Reaction score
23
Habari mwanaJF natumaini umzima wa afya njema kabisa.

Leo napenda kuomba ushauri wako kuhusu biashara yangu niliyopanga kuianzisha hapo baadae, kiukweli wazo langu la biashara ni zuri sana ni itakuwa biashara ya kudumu endapo nitafanikiwa kuianzisha.

Kwaleo naomba ushauri wako maana najua wewe ni mmja ya wapambanaji kama Mimi. Mimi nimefanikiwa kuanzisha wazo la biashara kama hatua ya kwanza kabisa, lakini sasa nimeshindwa kuianzisha hii biashara kwa changamoto kubwa hasa ya swala zima la pesa. Yaani sina pesa ya kufanikisha kutekeleza wazo langu la biashara, hivyo naomba ushauri wako nifanyeje ili niweze kupata pesa, kukopa siwezi maana sina dhamana yoyote.
Nawasilisha.
 
Hadi sasa hivi una mtaji kiasi gani?
 
Kama unawazo la biashara ni vizuri, inategemea na ukubwa wa biashara unayotaka kuanzisha chukua hatua moja kati ya zifuatazo:
  • Omba ndugu,jamaa na marafiki wa karibu wakusaidie au kukukopesha pesa.
  • Tafuta one business partner mwenye mtaji mshirikiane kwenye biashara kwa yeye kuwa mmiliki pia.
  • Tafuta washirika wawili wenye pesa na mmoja kati yao awe na uzoefu pia wawe wamiliki wa biashara.
  • Unapokua na changamoto ya mmtaji fikiri sana " How you structure your business pia uwezekano wa biashara yako kuweza kuwa scalable kulingana na capability na suitability ya operation.
Muhimu kama wazo lako ni exceptional unapowashirikisha watu ambao si ndugu zako unaweza wasainisha non disclosure agreement ili kulinza wazo lako. Pia ningependa kujua wazo lako linahusu sector gani na umekadiria initial cost kiasi gani?
 
From zero to hero. All the best
 
Ukitaka usaidiwe inatakiwa uwe wazii na sio kufichaficha mambo...ungeweka mchanganuo mzima wa biashara yako watu wangekusaidia ushauri otherwise labda unaogopa watu ku copy idea zako
 
Ukitaka usaidiwe inatakiwa uwe wazii na sio kufichaficha mambo...ungeweka mchanganuo mzima wa biashara yako watu wangekusaidia ushauri otherwise labda unaogopa watu ku copy idea zako
Yah watu watakopi aiseee ila kama una nafasi ya kumsaidia ni vema ukamfuata chemba mkapiga stories huko.
Mfano mi nina wazo zuri sana nashindwa kulifanikisha tatizo ni pesa ya mtaji. Ni kiasi cha 470,000/= tu nahitaji. Pia kwa kuanza nimeuza simu yangu 150,000/=
Na nilijaribu kuuza kiwanja lakin nilikosa wateja hii yote maana yake tayar nmeanza hatua ya kutafuta pesa hiyo
 
Safi
 
Fata huu ushauri hapa. Hata mimi naona utanifaa.
Cha kutia moyo tu ni kwamba wengi tuna mawazo lakini tunakutana na changamoto kama yako.
 
Kama kweli unahitaji mafanikio kama unavyoihitaji pumzi, mtaji sio tatizo...!! Tatizo lenu hamna dhamira ya kweli kutaka mafanikio...!!
 
Kama kweli unahitaji mafanikio kama unavyoihitaji pumzi, mtaji sio tatizo...!! Tatizo lenu hamna dhamira ya kweli kutaka mafanikio...!!
Ukiona mtu anaomba ushauri maana yake ameshahangaika sana na ameshindwa, na inawezekana pia hana maarifa kama ambayo wewe unayo. Unachopaswa ni kumshauri in a positive way. Hakuna mtu ambae hana dhamira ya mafanikio. Tumetofautiana katika kipato hata uwezo wa kufikiri pia
 


Atafute kwanza complete knowledge na sio ushuri wa sentensi mbili...!! Mf. akasome vitabu vya waliofanikiwa...!! Atafute maarifa kwa hali na mali (Invest in you first b4 hujaiweka hata mia chini, thats shuld be yur first investment).....!! No shortcuts to success...!!
 
demi mtu ambae hawezi kutafuta mtaji huyo sio mjasiliamali.Mjaliamali ni mtu ambae hata ukimpa laki moja or elfu hamsini anaweza kuikuza nakuipeleka kwenye main project aliyokusudia.Mimi kipindi naanza ujasiliamali nilianza na laki tatu na elfu 52,nikadunduliza ilipofika laki sita na 70,nikabadili aina ya biashara,nilipigana kwa jasho na damu kupambana na changamoto lakini mpaka kufikia leo mtaji wa million mbili/Tatu kwangu sio tatizo na nafanya hayo yote nikiwa bado shule.

Ukisubili watu wakupe au wakuwezeshe mtaji basi wewe utakufa na ndoto zako,binadamu wenye uwezo wakusaidia watu mtaji niwachache sana na nadra kuwapata.Jambo la msingi nikujikomiti kwa kukuza kidogo ulichonacho kiwe kikubwa,Ukishakuza mtaji watu wenyewe watakuja kuomba mshilikiane nao.

Mfano mimi kuna project naifanya itaghalimu kama 5.3M na bado kama asilimia 10 ikamilike.Lakini kuna watu kadhaa wamekuja kuniomba tuunganishe nao nguvu nikakataa.Lakini pia yupo mmoja alitaka anipe 10.5M nimuachie project yangu yote nikakataa(ingawa bado haijaisha).Kwa sababu najua ndani ya miezi minne mpaka sita fedha yangu yote itakuwa imesharudi nantaanza kupata faida nzuri tu.

Kwahiyo mkuu juhudi na jitihada zako inabidi zionekane kwa kukuza kidogo kilichopo ili kiwe kikubwa
Mtaji ni janga. I face the same problem mpaka nakata tamaa.
 
 
Hicho ndio ulipaswa kumshauri tangu mwanzo. Thanx
 
Asante umenifungua akili kidogo. Kuna watu ni wajasiriamali lakini elimu ya kupat huo mtaji ndo issue, tunahitaji elimu kama hii uliyonipa na zaidi. Asante ubaririkiwe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…