Nifanyeje nizoeane na majirani?

Nifanyeje nizoeane na majirani?

TheChoji

JF-Expert Member
Joined
Apr 14, 2009
Posts
5,771
Reaction score
17,849
Tangu nimehamia hapa mtaani ni takribani mwaka sasa umekatika. Mtaa ninaoishi ni nje kidogo ya mji ambapo watu wamejenga nyumba zao wamezungusha fensi na mageti. Pia wengi (pamoja na mimi) ni wafanyakazi ambapo mara nyingi ni watu wa kutoka asubuhi na kurudi jioni wakiwa ndani ya magari yao.

Sasa leo nimekaa nikatafakari, nikagundua kuwa zaidi ya majirani niliopakana nao upande wa kushoto na kulia, hakuna jirani mwingine ambaye walau hata namjua kwa jina. Hakuna mawasiliano ya aina yoyote kati yangu na majirani zangu, hakuna tukio lolote linalotukutanisha na hata ikitokea mtu akapata tatizo, sidhani kama kuna mtu atajitokeza kusaidia.

Mimi naona kama hii hali sio nzuri ila nashindwa kujua nifanyeje ili kujenga ujirani mwema, hasa kwa hawa majirani wa mbali kidogo nyumba ya tatu ya nne huko?
 
Ukisha chagua kuweka uzio huwa ni ngumu sana kuwa karib na majirani. Mfano rahis angalia zile nyumba za kawaida ambazo hazina uzio kupata majiran huwa rahisi mno, mfano mtu anoashea vyombo nnje, kufulia nguo nnje. Mtu ukipita ukamkuta jiran yako mathalan anafua lazma mtasalimiana na mtapeana mbili tatu. Kila jambo katika maisha huwa na faida na hasara mkuuu.
 
Tangu nimehamia hapa mtaani ni takriban mwaka sasa umekatika. Mtaa ninaoishi ni nje kidogo ya mji ambapo watu wamejenga nyumba zao wamezungusha fensi na mageti. Pia wengi (pamoja na mimi) ni wafanyakazi ambapo mara nyingi ni watu wa kutoka asubuhi na kirudi jioni wakiwa ndani ya magari yao...
Nilipohamia sehemu flani Yule jirani wa karibu nilienda kumsalimia.

Gonga hodi salimiana acha upuuzi
 
Mkuu kama wewe ni mkristu jitahidi uwe unasali jumuiya na kwenda church huko utafahamiana na baadhi ya majirani zako mnaosali pamoja.

Pia jitahidi uwe unahudhuria shughuli za kijamii za mtaani kwako kama misiba au hata sherehe za harusi,kipaimara,kumunio zinazotokea hapo mtaani unapoishi.lazima tu utafahamiana na majirani zako.

Pia siku ukiwa off jitahidi utumie hata mda mchache kujimix mtaani,kama kufanya manunuzi kwenye maduka ya mtaani unapoishi, kaa kwenye vigrocery vya mtaani unywe hata Maji Kama sio mtumiaji wa alcoholic drinks, jitahidi uwe unakaa hata kwenye vijiwe vya mtaani sikumojamoja na pia uwe unasalimia watu wa mtaani hata Kama unagari na pia uwe unawapa lift ukikutana nao.

Kibongobongo ni hatari sana unapoishi bila kufahamu majirani zako.
Jirekebishe haraka
 
Tangu nimehamia hapa mtaani ni takribani mwaka sasa umekatika. Mtaa ninaoishi ni nje kidogo ya mji ambapo watu wamejenga nyumba zao wamezungusha fensi na mageti. Pia wengi (pamoja na mimi) ni wafanyakazi ambapo mara nyingi ni watu wa kutoka asubuhi na kirudi jioni wakiwa ndani ya magari yao...
Jilipue weka ka party alika majirani wote wale na wanywe kana kwamba una birthday
 
Kama hakuna kakioski hapo nje na ww hunywi basi itazidi kuwa ngumu sana.

Labda ujitoe muhanga weekend moja jpili ufanye tour kwa mmoja hadi mwingine. Matokea yaweza kuwa hasi na chanya.

Kingine hamnaga hata vikao vya mtaa?

Kama unasali jumuia pia huwo ndio wasaa utakutana nao huko.
 
Kind of life I like

Pambana mkuu utoe toe salamu upate namba, ucoment status zao na mtajikuta mmezoeana.

Ila kwa upande wangu nachagua kujitenga
Ni bora kabisa kujitenga. Kadri unavyokuwa mbali na wengi,ndivyo unavyokaa mbali na matatizo. Kadri unavyokuwa na marafiki wengi ndivyo unavyokaribia kupata matatizo mengi
 
Ila yote kwa yote kwani hata hao kwa hao ulipohamia ulikuta/umeona kuna mazoea ya kusalimiana?

Huyu jirani yangu upande wa kushoto yeye hajaweka fensi na yupo muda kidogo hapa mtaani, kama miaka minne mitano ivi. Juzijuzi nilienda kumsalimia maana bado ni kijana kijana tukawa tunabadilishana mawazo.

Aisee nilishangaa jinsi anavyofahamiana na kila mtu, watu wakipita (kuna barabara kwa mbele, kama mita 20 - 30 kutoka ilipo nyumba) lakini wanasalimia, wanapunga mikono nk. Wenye magari wanapiga honi, wanashusha vioo wanapunga mikono... kwakweli nilisikia wivu sana.
 
Don't pretend like you're alone in this world, you're not alone at all. Na kuna maana yake ya wewe kuumbwa miongoni mwa wanadamu wenzio.
Compatibility!!!
Binaadamu tumeumbwa tuishi kijamii na nature imewekwa tukae hivo. Hakuna mtu asiyemuhitaji mwenzie hadi uone kua majirani si kitu au ushindwe kuingiliana nao.

Trust me nature inaweza kukupiga tukio moja tu hadi wewe mwenyewe ukarudi kwenye mstari... Mtoa mada kabla nature haijachukua njia zake get out na usalimiane na watu usije jutia. Tumeumbwa kama vidole vya mkono kidole kimoja hakiwezi jitenga pekee yake halafu kiseme kinaweza kutengeneza ngumi.

Kidole gumba ni kikubwa ila kinategemea vidole hivi vidogo kushirikiana ilie watengeneze ngumi imara. Hata kama una uwezo mkubwa mate hado hao watu wa chini unawahitaji kuliko kawaida.

Nashukuru mkuu, hili na mimi nimeliona sema sasa changamoto ni jinsi ya kujizoesha kwa watu usiowafahamu. Ningekua mtu wa ulabu labda ingesaidia maana wengi ningekutana nao ila sasa mimi ni mzee wa nyuki.
 
Kama hakuna kakioski hapo nje na ww hunywi basi itazidi kuwa ngumu sana.
Labda ujitoe muhanga weekend moja jpili ufanye tour kwa mmoja hadi mwingine. Matokea yaweza kuwa hasi na chanya.
Kingine hamnaga hata vikao vya mtaa?
Kama unasali jumuia pia huwo ndio wasaa utakutana nao huko.

Kioski kipo mbali sana na mimi sio mnywaji napiga fanta ki purplypurply. Hilo la kujiunga jumuia ni la msingi ngoja nifanyie mchakato👍
 
Back
Top Bottom